Mkuu nitakupa ushauri mdogo lakini unaweza kukusaidia
1. Jambo la kwanza kabisa kwa biashara hiyo, tafuta masoko yake ujirizishe nayo nje ya nchi.
2.Ukisha pata soko, sajili jina la biashara au kampuni ikiwa ni pamoja na TN n.k
3.Ukisha malizana na BRELA kusajili, nenda wizara ya viwanda na biashara kuomba lessen ya kusafirisha bizaa hiyo. Watakueleza ni mambo gan wanaitaji
4.Ukisha pata Leseni ya kusafirisha, na tayari una mziko unatakiwa kwenda nje, utatakiwa kwenda kwenye mamlaka husika hili kupata kibali cha kusafirishia kwa mfano kama unapeleka mazao kama dagaa, utatakiwa kuomba kibali cha kusafirisha kwa muda huo kwa mwanza kinatolewa pale nyegezi.
5.Kumbuka ikiwa unataka kusafirisha katika nchi za Africa mashariki, utatakiwa kujiandikisha kwenye ofic iitwayo chamber of commerce. hawa watakupa barua ya kuonyesha wewe ni mtanzania na bidhaa hiyo inatoka Tanzania. hii itakusaidia wewe unapo ingiza mzigo kwenye nch husika, hautaulipia ushuru badala yake utalipa vat, ya ongezeko la thaman tu ambayo ni 16% ya mali yako.
Yako mengi ila leo nakuchangia hayo mkuu ngoja wengine waje kukuongezea