'Naomba uje unisukume'

Mtanzanika

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
2,389
1,131
Jamaa flani alikuwa amelala na mkewe
saa nane za usiku wakaamshwa na
mtu akipiga hodi mlangoni kwao.
Wakabishana nani afungue....hatimaye
mume akaenda kufungua mlango
akiwa na usingizi mwingi,akamkuta
jirani yake mlevi mlangoni
JAMAA:"Nini tena mkubwa mbona
kuamshana saa hizi?"
MLEVI:"Naomba uje unisukume"
Jamaa akajua labda gari la huyu mlevi
limenasa kwenye tope,akamwambia "subiri
nivae viatu"
Baada ya kuvaa viatu akatoka na
kuanza kuandamana na mlevi.
Mlevi akaongoza njia mpaka kwenye
mabembea,akakaa kwenye bembea
moja,akamgeukia yule jamaa na
kumwambia "Okay nisukume"
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom