Naomba ufumbuzi wa hili tatizo

the happiest man

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2016
Posts
253
Reaction score
218
Habari za muda huu waungwana wa jf

Niende straight kwenye mada...mimi ni kijana nnampenzi wangu(ke) ambaye nnampenda sana lakini tatizo anatoa harufu mbaya ukeni, kitu ambacho kinanifanya nikose raha natumai na yeye anakosa raha pia....tumeenda hospital lakini tatizo bado lipo....ameniomba nije jf kama naweza kupata ufumbuzi wa hili tatizo..sababu kubwa ya kulileta hili jambo huku jf kuna jamii kubwa ya watu, ambao pengine kwa namna moja au nyingine wameshakumbwa na tatizo hili na wakapata ufumbuzi........

sitegemei kutukanwa au kukejeriwa kwa namna yoyote ile..asante

I BLNG 2 JESUS CHRST
 
Poleni, wewe ni mstaarabu ngoja niwasaidie hivi
1. Ale punje za kitunguu swaumu kila siku asubuhi na jioni,azimeze.
2. Anywe Juice ya mananasi.
3. Atumie mchaichai,auloweke na maji ya moto yakipoa kabisa anawe kwa bibi ake,sio hukata harufu tu utaona na mengine pia mazuri.
4. Maji yaliyolowekewa sufuria ya ugali.
Kati ya njia hizo moja wapo huondoa kabisa tatizo.
 
Maserat shikamoo heshima yako nimekuelewa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee baba hongera kwa kumsaidia na kumjali demu wako,

Wanaume wengine wasingeweza haswa wale watoto wa mama, mayai mayai / mabishoo...

Big up bro
hebu tafuta kwa njia ya mtandao / Google / ujue tatizo ni nini....??
Na tiba yake ni ipi ......??
 
Nimepata somo hapa.
 
Mpeleke Ocean road wahi mapema asubuhi kama saa 06:00Hrs ulizia kwenye vipimo vya Kansa ya uzazi.

Baada ya vipimo tuombe Mungu kama hakuna tatizo hilo,mpeleke kwa daktari wa wanawake na watoto hospitali ya Dr KAIRUKI huyu anapatikana kila Jumamosi.

Vilevile zingatia ushauri mwngine uliopewa wa kujisafisha vizuri ikiwezekana tumia vagina wash japo ni ghali, Pima U.T.I kwenye hospital bora kwa maelekezo ya mkojo wa asubuhi ule wa kati.

Haya nimejaribu kukuelezea kutokana na hatua mbalimbali zilizompata mke wangu na hatua tuliofikia yy ilibainika uwepo wa bacteria Sugu wa UTI na ikashauriwa nami pia nipimwe mkojo.


Nilifanya hivyo ktk hospital nyingine sikuonekana na tatizo lolote.
 
Kwanza nimekupenda sana kwa kuwa na mpenzi wako bega kwa bega kwenye hilo tatizo haujamuacha huo ndio uanaume mwambie awe anajisafisha vizuri sana wengine wanashindwa kujisafisha vizuri
Kweli kabisa mkuu, mpe darasa kidogo basi maana ww unaweza saana kujisafisha
 
NB:
1.Azingatie usafi,ikiwemo kubadilisha Nguo ya ndani pichu,asikae nazo muda mrefu.
2.aache kutumia pichu za mpira atumie cotton.
3. Usafi katika kujisafisha yeye mwenyewe kwenye nyeti zake,asijafishe vizuri maji safi na Salama.
4. Kama kuna sabuni au kitu chochote cha kemikali au viunga vyovyote vya kubana Bibi ake aache,hivo pia vina sababisha kutoa harufu kali.
5. Hizo njia hapo juu ni za asili,dare her to use any chemical kwa bibi ake,ataoata madhara zaidi.
Hamjachelewa bado,mwambie atumie sana sana mchaichai kunawa na punje za vitunguu swaumu kumeza within a week tatizo litaanza kupungua. Mengine mkiona vitawasaidia leteni feedback but wengine ninao washauri hayo tatizo huwa zinakwisha kabisa.
 
Mwambie ajitahidi kijisafisha ila asitumie sabuni maana sabuni huuwa bacteria ambao wanalinda papuchi yke....jambo lingine kama ananywele nyingi apunguze bila kusahau ujitahidi kumwagia nje maana spam nazo hupelekea kutoa harufu kali
 
kuna mtu alikua na shida kama hii mikamshauri amfwate kaka mmoja ivi ambaye najua alinsaidia..
Sasa hivi naona wapo sawa tu
Kama hutojali njoo Pm kwa maelezo zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…