Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Ni kweli mkuu watu wanapotosha kwa makusudi au kwa kutokujua....Mkuu Eiyer yawezekana wengi hatuelewi kwa haya mambo ya microchip na namba 666 ndio maana tumekuwa waamini wa kile tunachopotoshwa.
Sasa nimekuelewa!
Masuala ya unabii huu wa siku za mwisho unazidi kuwa rahisi kadiri tunavyokaribia...
Miaka ya 1500 huko walidhania mengi kuhusiana na unabii huu lakini hawakuwa sawa,imeendelea hivyo lakini leo hii mambo yanazidi kufunguka tu na ndiyo maana Danieli aliambiwa kuwa ayafunge maana ni ya wakati ujao,inawezekana tunaukaribia sana ndiyo maana watu wanaanza kuhisi hisi zaidi na kwa wingi lakini tuache maandiko yajifunue yenyewe....
Tufuatilie sana matukio yanayoendelea kutokea duniani na kusoma sana maandiko matakatifu yanayohusu unabii wa siku hizi ili tuweze kuelewa na kuepuka kupotoshwa kirahisi....