toccara
JF-Expert Member
- Apr 17, 2014
- 540
- 203
Naomba ndugu zangu mnisaidie juu ya hili tatizo la huyu mtoto, Mwaka 2008 nilikuwa najitolea katika kituo kimoja cha watoto yatima baada ya kumaliza masomo yangu ya kidato cha sita, pale nilifanya kazi kwa moyo wangu wote kwa kuwa napenda sana watoto. Aliletwa mtoto mmoja wa kiume ambaye mama yake alifariki akiwa na week mbili toka kuzaliwa na baba yake hajulikani aliletwa na mama yake mkubwa kwa kuwa nae alikuwa hajiwezi kutokamna na kuumwa ugonjwa wa kisasa, basi nilikapenda sana hako katoto. Alivyofikisha miezi sita yule mama mkubwa alifariki na pale hakuwahi kujitokeza mtu mwingine kama ndugu hivyo mimi nikawa ndugu wa hiyari. Alivyofikisha mwaka alinizoea kwa kuniita mama, naenda chuo nikirudi namuwahi mtoto kituoni, nilianza tuu kumtania tania sister mkuu wa hapo kuwa namtaka yule mtoto. Ni story ndefu kidogo lakini Mungu alisaidia nilipata yule mtoto akiwa na miaka miwili ndiyo nilikabidhiwa rasmi ni mtoto wa kiume na nilimpenda sana na mpaka sasa ninavyoandika hivi ninampenda sana, sasa hivi ana umri wa miaka sita yupo darasa la pili, licha ya sasa nina watoto wangu wa kuzaa lakini huyu namchukulia ni mtoto wangu wa kwanza na mume wangu anampenda pia huyu mtoto.
Tatizo limekuja mwaka jana na nilipojifungua watoto wangu, huyu mtoto amekuwa na vituko vya kila aina na ana utundu uliopitiliza kiasi siwezi kusema najuta ila kiukweli naumia maana sina pa kumpeleka ni wangu. kituko cha kwanza alianza kuchana magodoro anatoa ile cover ya juu mpaka apate godoro lenyewe then anakata vipisi vidogovidogo kwa kutumia mkono vinakuwa vinji vinajaa ndoo kubwa, anapenda sana kuua wadudu na kuwaweka kwenye mfuko anawazika( hili nililifuatilia nikakuta ameshazika kama mafungu manne) anaweza kuwang'ata watoto wote au kuwapiga makwenzi., ukisahau kufunga chumba anaingia anapuliza perfume zote mpaka ziishe hili la perfume amelirudia jana usiku. kwa kweli anavituko vingi sana na sijapunguza upendo kwake kiukweli tunampenda sana.
Naombeni msaada weni nimfanye nini ili aache hivi vituko?
Tatizo limekuja mwaka jana na nilipojifungua watoto wangu, huyu mtoto amekuwa na vituko vya kila aina na ana utundu uliopitiliza kiasi siwezi kusema najuta ila kiukweli naumia maana sina pa kumpeleka ni wangu. kituko cha kwanza alianza kuchana magodoro anatoa ile cover ya juu mpaka apate godoro lenyewe then anakata vipisi vidogovidogo kwa kutumia mkono vinakuwa vinji vinajaa ndoo kubwa, anapenda sana kuua wadudu na kuwaweka kwenye mfuko anawazika( hili nililifuatilia nikakuta ameshazika kama mafungu manne) anaweza kuwang'ata watoto wote au kuwapiga makwenzi., ukisahau kufunga chumba anaingia anapuliza perfume zote mpaka ziishe hili la perfume amelirudia jana usiku. kwa kweli anavituko vingi sana na sijapunguza upendo kwake kiukweli tunampenda sana.
Naombeni msaada weni nimfanye nini ili aache hivi vituko?