Habari zenu ndugu zangu, natumaini muwazima! Leo ningependa kushare na nyie hiki nilichokiona. Naimani kina ukweli ndani yake.
Je unapokuwa kwenye mtoko, wewe hutoa tip kwa muhudumu kwa huduma nzuri aliyokupatia? Je ni kiasi gani wewe hutoa ukilinganisha na bili yako? Kwanini wengi hutoa tip kwa warembo tu kwakuwa tunawataka? Je ni sawa kumuacha kaka au dada mtafutaji bila tip? Unafanyaje unapokuwa na mpenzi wako na unataka kutoa tip kwa mdada au mkaka ikiwa wewe ni jinsia tofauti na muhudumu bila kuonekana kuwa unamtaka? Sidhani kama unaweza kumuacha ndugu yako sehemu yeyote anafanya kazi ya kuhudumu bila kumpa tip, wengine hawawezi kuacha kumpa tip mtu anayemfahamu, anatoka naye mkoa au kabila moja au alisoma naye? Vilevile kwanini huyu aliyepewa tip asielewe tu kuwa ile ni tip isiyotaka ya ziada, maana utakaporudi utachangamkiwa zaidi na hata kupewa namba mixer kujirengesha hasa kwa wadada!? Hii imekaaje wakuu?
Je unapokuwa kwenye mtoko, wewe hutoa tip kwa muhudumu kwa huduma nzuri aliyokupatia? Je ni kiasi gani wewe hutoa ukilinganisha na bili yako? Kwanini wengi hutoa tip kwa warembo tu kwakuwa tunawataka? Je ni sawa kumuacha kaka au dada mtafutaji bila tip? Unafanyaje unapokuwa na mpenzi wako na unataka kutoa tip kwa mdada au mkaka ikiwa wewe ni jinsia tofauti na muhudumu bila kuonekana kuwa unamtaka? Sidhani kama unaweza kumuacha ndugu yako sehemu yeyote anafanya kazi ya kuhudumu bila kumpa tip, wengine hawawezi kuacha kumpa tip mtu anayemfahamu, anatoka naye mkoa au kabila moja au alisoma naye? Vilevile kwanini huyu aliyepewa tip asielewe tu kuwa ile ni tip isiyotaka ya ziada, maana utakaporudi utachangamkiwa zaidi na hata kupewa namba mixer kujirengesha hasa kwa wadada!? Hii imekaaje wakuu?

