wa hapahapa
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 7,460
- 4,402
Salamu zangu kwenu wote
Mwaka jana mwezi wa nne nilipata matatizo kazini na nikafukuzwa kazi. Baada ya hapo nikawa nafanya kazi yoyote inayotokea za kusaidia fundi sikuweza kufanya biashara kwakuwa sikuwa na mtaji na akiba ya pesa niliyokuwa nayo ilikuwa kidogo
Mwezi wa saba mwaka jana nikaachana na mwanamke niliyekuwa naishi nae tuligawana baadhi ya vitu, aliniachia mtoto niliyezaa nae nilishindwa kukaa nae kwakuwa ni mdogo hivyo nikampeleka kwa mama yangu
Baada ya hapo maisha yamezidi kuwa magumu upatikanaji wa kazi za ujenzi umekuwa mgumu, nadaiwa kodi na nimekuwa nasumbuliwa na vidonda vya tumbo
Naomba msaada kwa yeyote yule atakayeweza kunisaidia pesa au ushauri
Nina shida ya elfu kumi ambayo nitatumia kula leo na kesho na kesho kutwa
Yupo mtu ameniambia atakuja Jumatano kununua kitanda changu, natarajia kulipia leseni ya kuendesha bodaboda
Mwaka jana mwezi wa nne nilipata matatizo kazini na nikafukuzwa kazi. Baada ya hapo nikawa nafanya kazi yoyote inayotokea za kusaidia fundi sikuweza kufanya biashara kwakuwa sikuwa na mtaji na akiba ya pesa niliyokuwa nayo ilikuwa kidogo
Mwezi wa saba mwaka jana nikaachana na mwanamke niliyekuwa naishi nae tuligawana baadhi ya vitu, aliniachia mtoto niliyezaa nae nilishindwa kukaa nae kwakuwa ni mdogo hivyo nikampeleka kwa mama yangu
Baada ya hapo maisha yamezidi kuwa magumu upatikanaji wa kazi za ujenzi umekuwa mgumu, nadaiwa kodi na nimekuwa nasumbuliwa na vidonda vya tumbo
Naomba msaada kwa yeyote yule atakayeweza kunisaidia pesa au ushauri
Nina shida ya elfu kumi ambayo nitatumia kula leo na kesho na kesho kutwa
Yupo mtu ameniambia atakuja Jumatano kununua kitanda changu, natarajia kulipia leseni ya kuendesha bodaboda