The Great Haya
JF-Expert Member
- Apr 6, 2014
- 1,799
- 1,681
Habari za majukumu wakuu, ndugu zangu nimekuwa nasumbuliwa na tonsils za upande wa kulia mda mrefu. Nimetumia antibiotics hasa amoxicillin kwa muda mrefu lakini zinarudia mara kwa mara.
Nilishaacha hata kunywa vitu vya baridi lakini bado. Nina imani humu kuna wataalamu mbalimbali na wenye uzoefu naomba msaada wenu
===
Maoni ya mdau
Nilishaacha hata kunywa vitu vya baridi lakini bado. Nina imani humu kuna wataalamu mbalimbali na wenye uzoefu naomba msaada wenu
===
Maoni ya mdau
Bado kuna mambo mengu ya kuzingatia kabla ya maamzi sahihi:
1: Kupata historia yako kamili
Unaweza kuwa na matatizo ambayo binafsi hujayatambua ambayo haujayazingatia.
Mfano:
A:Unaweza kuwa na matatizo kama: Allergy/mzio(hivyo vumbi vyakula vya rangi isiyo asili ikawa ni chanzo).
B: Unaweza kuwa na tatizo la Reflux(Gastro Esophageal Reflux/GERD). Ambayo hurudi juu na kuathiri njia ya koo.
C: Tiba isiyotoshelevu ikihusisha kiasi cha dawa, aina ya dawa/?usugu na kiasi cha muda wa uchukuaji dawa.
2: Pia ni wakati wa kujua inatokea mara ngapi kwa mwezi au mwaka kwa wastani.
3: Kuangaliwa koo ili kuona mabadiliko yaliyopo kama kweli ni Tonsils au kuna kitu tofauti.
NB:
Kwa mazingiza haya, ni vyema kukutana na daktari bingwa wa koo(ENT) ili aweze kufanya majumuisho mazuri na tiba sahihi. Ukishindwa, pia daktari bingwa wa magonjwa ya ndani au daktari wa kawaida mwenye uzoefu mzuri anaweza kuwa msaada mkubwa kwako kwa kuanzia. Tiba njema.