Naomba msaada nafikaje Mgololo kutokea Dar

Naomba msaada nafikaje Mgololo kutokea Dar

Inategemea utafika saa ngapi makambako Ila Kama utafika usiku inabidi ulale pale then asubuhi Kuna gari nyingi pale ,ukifika makambako ulizia stend ya zamani hapo ukiuliza mtu yeyote atakuelekeza gari za mgololo bei ni 4000 Hadi 6000 kutegemea utapanda coaster au Noah kuhusu gesti zipo gaharama ni 4000 Hadi 7000
Mmh 4k?
Hizi ni Lodge zina ubora gani?
 
Telemkia mafinga utachukua vile vigari vidogo vipo njiapanda ya kwenda jeshini na ndio njia ya kwenda mufindi. Mwambie dereva akushushe gogo beach. Pale kuna gest na lodge na sio mbali na kiwanda cha makartasi. Ukifika nitafute mie mwenyeji wako naitwa mzee lenad nyenza

Boss gogo beach si iko Nyangugulu? Huyu anaenda Mgololo..Kama unampoteza vile .lol..mwanyenza bwana😷
 
shuka mafinga next day panda coaster au panda tren-tazara moja kwa moja
 
Njia rahisi ni kushuka mafinga unalala halafu siku ya pili kuna mabasi ya moja kwa moja mpaka mgololo kiwandani. Kuna guest house nzuri tu na nyingine za kawaida, nimeishi maeneo hayo.
 
akifika njombe mwambie aulizie mabasi ya moronga, kisha mgololo
Mwambie konda akushushe sehemu inaitwa Igawa baada ya hapo utaingia Mbarali mpaka Iringa hapo utatokea Makambako then utaelekea Njombe na kutokea Mgololo
 
Makambako hawezi pata basi la mgololo, mwambie aunganishe hadi Njombe.. lodge nzuri ni Mama makinda Lodge and restaurant..
Inategemea utafika saa ngapi makambako Ila Kama utafika usiku inabidi ulale pale then asubuhi Kuna gari nyingi pale ,ukifika makambako ulizia stend ya zamani hapo ukiuliza mtu yeyote atakuelekeza gari za mgololo bei ni 4000 Hadi 6000 kutegemea utapanda coaster au Noah kuhusu gesti zipo gaharama ni 4000 Hadi 7000
 
Ushauri

Shuka mafinga kama umetokea dar.

Shuka makambako kama umetokea mbeya au songea.

Kwanini

Umbali kutoka mafinga hadi makambako ni km 84.

Umbali kutoka mafinga hadi mgololo ni km 85.

Umbali toka makambako hadi mgololo ni kma 71.

Sasa kamanumetokea dar ukishuka makambako.maana yake utatembea km 84+71 kwa sababu utaipita kwanza mafinga.

20200824_224848.jpeg
20200824_224902.jpeg
 
Shukia mafinga nenda njiapanda ya kuelekea jeshini hapo kila utakayemuuliza atakuonesha gari za kwenda mgololo. Hali ya mgololo ni joto tofauti na mafinga. Halafu ujue pale ni township wageni ni wengi wanaofuata mizigo ya karatasi hivyo gesti zipo ingawa ni za kawaida na kama utapitiliza basi shukia Makambako
 
Back
Top Bottom