Naomba msaada nafikaje Mgololo kutokea Dar

Naomba msaada nafikaje Mgololo kutokea Dar

sintah

Senior Member
Joined
Aug 18, 2013
Posts
187
Reaction score
191
Habarin wanajamvi,

Kwa wale wajuvi wa kuzunguka nchi nawezaje kufika Mgololo nikitokea Dar? Je, Mgololo kuna sehemu za kulala kama lodge na guest house? nishukie Mafinga au Makambako na baada ya hapo usafiri upoje na ni wa muda gani? Na nauli zao zipoje.

Natanguliza shukrani.
 
Mwambie konda akushushe sehemu inaitwa Igawa baada ya hapo utaingia Mbarali mpaka Iringa hapo utatokea Makambako then utaelekea Njombe na kutokea Mgololo
mkuu mgololo ya mufindi namaanisha hko kwenye kiwanda cha karatasi
 
Inategemea utafika saa ngapi makambako Ila Kama utafika usiku inabidi ulale pale then asubuhi Kuna gari nyingi pale ,ukifika makambako ulizia stend ya zamani hapo ukiuliza mtu yeyote atakuelekeza gari za mgololo bei ni 4000 Hadi 6000 kutegemea utapanda coaster au Noah kuhusu gesti zipo gaharama ni 4000 Hadi 7000
Habarin wanajamvi,
kwa wale wajuvi wa kuzunguka nchi nawezaje kufika mgololo nikitokea dar? je mgololo kuna sehem za kulala kama lodge na guest house? nishukie mafinga au makambako na baada ya hapo usafiri upoje na ni wa mda gani? na nauli zao zipoje.

natanguliza shukran.
 
Inategemea utafika saa ngapi makambako Ila Kama utafika usiku inabidi ulale pale then asubuhi Kuna gari nyingi pale ,ukifika makambako ulizia stend ya zamani hapo ukiuliza mtu yeyote atakuelekeza gari za mgololo bei ni 4000 Hadi 6000 kutegemea utapanda coaster au Noah kuhusu gesti zipo gaharama ni 4000 Hadi 7000
asante sana mkuu me natoka dar na basi la mbeya kuna watu wanishauri nishukie.mafinga na wengine makambako kwa uzoefu wako wapi sehem sahihi kushukia na ntwahi kufika hko mgololo.
ikumbukwe basi.inaanza kufika mafinga ndo inaenda makambako
 
Unaweza shuka Mafinga au Makambako. Gari huwezi kukosa. Nyumba za wageni zipo ila usitegemee nyota 1,2,3,4 au 5. We ridhika na utakachopata. Ukifika wasalimie Mabaoni na Makungu
 
asante sana mkuu me natoka dar na basi la mbeya kuna watu wanishauri nishukie.mafinga na wengine makambako kwa uzoefu wako wapi sehem sahihi kushukia na ntwahi kufika hko mgololo.
ikumbukwe basi.inaanza kufika mafinga ndo inaenda makambako
Shukia makambako usafiri wa uhakika muda utakaofika mgololo ni saa 7-9
 
asante sana mkuu me natoka dar na basi la mbeya kuna watu wanishauri nishukie.mafinga na wengine makambako kwa uzoefu wako wapi sehem sahihi kushukia na ntwahi kufika hko mgololo.
ikumbukwe basi.inaanza kufika mafinga ndo inaenda makambako
Shuka mafinga...lala hapo asbh panda coaster za mgololo..koti na sweta na mzula usiache
 
mkuu mgololo ya mufindi namaanisha hko kwenye kiwanda cha karatasi
Telemkia mafinga utachukua vile vigari vidogo vipo njiapanda ya kwenda jeshini na ndio njia ya kwenda mufindi. Mwambie dereva akushushe gogo beach. Pale kuna gest na lodge na sio mbali na kiwanda cha makartasi. Ukifika nitafute mie mwenyeji wako naitwa mzee lenad nyenza
 
Mwambie konda akushushe sehemu inaitwa Igawa baada ya hapo utaingia Mbarali mpaka Iringa hapo utatokea Makambako then utaelekea Njombe na kutokea Mgololo
Una roho ya wajumbe 😀
🏃‍♂️ 🏃‍♂️ 🏃‍♂️

Everyday is Saturday.......................... 😎
 
Simu yako ina google map hata kuweka tu bundle alafu ufuatilie unakoenda huwezi eti?
 
Wakati nimefuata cheti changu cha form 4 kule Mbeya, nililala guest ya Tsh 5,000; Yanii, ni bora tu ningelala chini ya mwembe.
Usipende kulala guest house zilizo karibu na stand kuu za mabasi utaliwa na kunguni kinyama, wengine utarudi nao kwenu kama wa mbegu au zawadi ukapandikize .
 
Back
Top Bottom