Naomba msaada jinsi kuhairisha chuo

Naomba msaada jinsi kuhairisha chuo

pafuada

Member
Joined
Oct 1, 2015
Posts
41
Reaction score
3
Wakuu naomba kujua utaratibu wa kuhairisha chuo na gharama zake maana nimechaguliwa MIHAYO TABORA ila mkopo nimekosa, hivyo nataka kuhairisha ili mwaka kesho nisiangaike na TCU na mwaka huu niutumie kutafuta pesa ya kujisomesha.

NATANGULIZA SHUKURANI KWA ATAKAE NISAIDIA USHAURI.
 
Una uhakika gan kam umekosa mkopo?
Acha kukata tamaa dogo subir LOT nyngne HESLB waziachie.
 
Usikate tamaa kuwa umekosa mkopo, subiri HESLB watatoa bacth nyingine.
Lakini kwa kujibu swali lako, ukitaka kuhairisha mwaka wa masomo unatakiwa kuripoti chuoni na kulipa at least ada ya semister moja na then una andika barua ya kuomba kuhairisha mwaka.
 
Ukitaka kuhairisha chuo we andika barua ya kusitisha then peleka TCU but unatakiwa uandike sababu ya kusitisha ili mwakani usije kusumbuliwa.
 
Ukitaka kuhairisha chuo we andika barua ya kusitisha then peleka TCU but unatakiwa uandike sababu ya kusitisha ili mwakani usije kusumbuliwa.

Mh mbona wanasema unalipa part of ada chuoni na kuandika barua chuoni halafu chuo ndio kitawataarifu TCU baada ya kuwa kimukusajili kama mwanafunzi wao?
 
Mh mbona wanasema unalipa part of ada chuoni na kuandika barua chuoni halafu chuo ndio kitawataarifu TCU baada ya kuwa kimukusajili kama mwanafunzi wao?

kuna maelezo yananichanganya hapo juu. sijui nifuate kipi? barua kwenda tcu au kwenda chuoni?
 
kuna maelezo yananichanganya hapo juu. sijui nifuate kipi? barua kwenda tcu au kwenda chuoni?

Ili uweze kuhairisha mwaka wa masomo ni lazima kuwe na commitment kutoka kwako, na inapatikana kwa wewe kulipa ada ya angalau semister moja halafu unasajiliwa kbs ndipo unaandika barua kwa chuo husika kuomba kuhairisha mwaka wa masomo
 
sio kweli, andika barua peleka tcu, wakugongee muhuri wao wa kusitisha kwenda chuo. Ungekuwa umesoma hata semister moja, kisha ukaasitisha chuo, hapo ndio ungeandika barua chuo
 
Usikate tamaa kuwa umekosa mkopo, subiri HESLB watatoa bacth nyingine.
Lakini kwa kujibu swali lako, ukitaka kuhairisha mwaka wa masomo unatakiwa kuripoti chuoni na kulipa at least ada ya semister moja na then una andika barua ya kuomba kuhairisha mwaka.

sasa atalipa vipi ada ya semister moja wakati anaahirisha masomo kwa kukosa ada?!
 
Hapo haina haja hata ya kuandika barua kokote kwa kuwa bado haujajisajiri.

Mimi mwaka jana niliomba chuo kupitia TCU na sikuripoti kwa sababu zangu binafsi na mwaka huu nimeomba chuo kupitia mfumo huo huo na nimechaguliwa na admission letter nimepata.
Kikubwa usiwe umesajiriwa.
 
Kwanza nikupe pole ndugu, mm poa cjapata mkopo japo niliomba sasa nimeshindwa kuendelea na masomo yangu ya degree kutokana na wazazi kushindwa kulipa ada mana tangu certificate na diploma walinilipia. Ukitegemea kipato chao cha chin (kijijini)
 
Una uhakika gan kam umekosa mkopo?
Acha kukata tamaa dogo subir LOT nyngne HESLB waziachie.
Lakini kumbukeni kua japo mnamtia moyo asubiri je anaenda chuo au yupo home mana vyuo vimefunguliwa mda mrefu na vyuo vingine wanakaribia test one, hapo kuna kupitwa na masomo kwa ujumla ndo baadaye mwanafunzi anafanya vibaya kwenye masomo yake.
 
Usikate tamaa kuwa umekosa mkopo, subiri HESLB watatoa bacth nyingine.
Lakini kwa kujibu swali lako, ukitaka kuhairisha mwaka wa masomo unatakiwa kuripoti chuoni na kulipa at least ada ya semister moja na then una andika barua ya kuomba kuhairisha mwaka.
Kaahirisha masomo kutokana na kukosa ada na kutegemea atapata msaada toka board ya mikopo, sasa jaman mnampa ushauri wa kulipa ada yeye aipate wapi??
 
jamani heslb inakuwaje watu wazima Open university wanapata mkopo harafu watoto wa undergraduate kama hawa wanakosa??? Kuweni makini jaman izo mikopo zinavigezo kweli au ndo rondamly selection.... So sad...
 
jamani heslb inakuwaje watu wazima Open university wanapata mkopo harafu watoto wa undergraduate kama hawa wanakosa??? Kuweni makini jaman izo mikopo zinavigezo kweli au ndo rondamly selection.... So sad...
Yaan usiombe ya kakutokea ndugu its too sad, kuona unaacha kuendelea na masomo nawakati umepata GPA ya juu alafu unaacha school, I will never forget it in my life................ Never forget..... My Government.......
 
Back
Top Bottom