mishahara ya watumishi wa mamlaka za maji inatofautiana kutoka mamlaka moja hadi nyingine.
Unatakiwa ufahamu pia hizi mamlaka za maji zimegawanywa kimadaraja kuna daraja A,B,C
Mamlaka za daraja A kama sijakosea ni DAWASCO,ARUWASA,MWAUWASA,DUWASA na mamlaka ya Tanga na Songea hizi zinaitwa daraja A kwa sababu hizi zina mapato mengi ya kutosheleza kulipa mishahara ya watumishi pamoja na kulipia gharama zote za uendeshaji, Bodi ya wakurugenzi wa mamlaka hizi ndio wanapanga mishahara ya watumishi jinsi wenyewe watakavyoona na jinsi mapato ya mamlaka husika yanavyojitosheleza na kuomba kibali kutoka kwa katibu mkuu Utumishi na Msajili wa hazina ili waweze kulipa hiyo mishahara wanayoitaka wao.
Mishahara inatofautiana kwa kila mamlaka za daraja A.
Mamalaka za Daraja B ni nyingi kidogo sina data zake kamili,ila nyingi ni za miji midogo kama Singida,Kilimanjaro, etc hizi nazo zinaweza kulipia gharama za mishahara na baadhi ya gharama za uendeshaji,ila zinapata pia ruzuku kutoka serikalini,hizi nazo zinajipangia zenyewe viwango vya mishahara ila si mikubwa kutoka hizi mamlaka hata makusanyo yao sio makubwa, na
Mamlaka za Daraja c nyingi na mamaaka za maji za miji midogo kama ni zile Mamalaka ya maji mji mdogo himo ,Mamlaka hizi ni zile zote ambazo kwa kiasi kikubwa zinaendeshwa na fedha kutoka Serikalini Katika kulipa mishahara, watumishi wa mamlaka hizi wengi unakuta ni watumishi wa halmashauri ya wilaya ya sehemu husika au watumishi wa wizarani ya maji hivyo mishahara yao ni ya TGS inategemea sasa na cheo chake.
Kwa kifupi hakuna uniformity ya mishahara kwenye hizi mamlaka