Naomba Kupewa Profile ya Taasisi ya IPSOS

Naomba Kupewa Profile ya Taasisi ya IPSOS

Mugabe wa Bongo

Senior Member
Joined
Apr 14, 2012
Posts
145
Reaction score
73
Habari za majukum wana JF, Nimesikia kuna taasis inaitwa IPSOS ambayo ni taasis inayofanya research na kutoa majibu kuhusu usikivu na idadi ya wasikilizaji pamoja na ubora wa Vipindi na watangazaj wa Radio na TV.

Clouds Media naona wanajinadi wao ndio wameonekana kua bora kuliko vipindi vyote vya radio hapa Tanzania na watangazaji wake ndio watangazaji bora kuliko watangazaji wote Tanzania.

Je IPSOS profile yao ipoje, Mwenye kuifahamu naomba atujulishe vizuri kabla hatujaanza kuchambua ukweli kuhusu hayo majibu ya utafiti wao walioufanya!
 
katika nchi hii radio ninazosikiliza ni mbili tu,east African radio na kiss FM,nyingine sizijui..
 
wala..biggest radio ratings iko kwa Radio Free Africa,ebu wait niitafute proof yangu,nitaiscan hapa
 
Hawa jamaa huwa nina wasiwasi. Wametoa matokeo Almost kila kipindi na kila mtangazaji wa clouds radio kimeshika/kashika number moja.
 
Ni kama wameingia na nondo tu kwenye mtihani kisha majibu yakatoka wamefaulu wakaanza kujitangaza kuwa wao ni magenius
 
Mimi naijua Ipsos Synovate iliyoko Nairobi ambayo ni maarufu kwa kutoa Opinion polls haswa nyakati za uchaguzi mkuu
 
Clouds huwa hawana aibu kabisa!..ila wanajichoresha halafu inawapumbaza wenyewe especially kwa professionals wachache walio nao...akili kumkichwa...
 
Habari za majukum wana JF, Nimesikia kuna taasis inaitwa IPSOS ambayo ni taasis inayofanya research na kutoa majibu kuhusu usikivu na idadi ya wasikilizaji pamoja na ubora wa Vipindi na watangazaj wa Radio na TV.

Clouds Media naona wanajinadi wao ndio wameonekana kua bora kuliko vipindi vyote vya radio hapa Tanzania na watangazaji wake ndio watangazaji bora kuliko watangazaji wote Tanzania.

Je IPSOS profile yao ipoje, Mwenye kuifahamu naomba atujulishe vizuri kabla hatujaanza kuchambua ukweli kuhusu hayo majibu ya utafiti wao walioufanya!
Binafsi nimeshawahi kufanya kazi na SYNOVATE/IPSOS, kale kautaratibu kao ka-malipo kiduchu ya kinyonyaji huwafanya wakusanya takwimu wao [vibarua] kupika data. Ile menejimenti yao ya wakenya [iliyokuwepo miaka ya 2009] haikuwa vizuri sana. japo wana media monitoring room, sina uhakika na takwimu zao. Kusema kweli tangu nifanye nao kazi na kuwaelewa vizuri siamini tena tafiti zao Mugabe wa Bongo
 
Last edited by a moderator:
Makanjanja tu hao wanawalipa watu shilingi elfu 2 kwa siku utegemee utafiti sahihi?.Alafu sisi wabobezi kwenye tafiti na takwimu huwa tunaangalia maeneo na muda ulipofanyia utafiti wako lazima ukifanya utafiti kama huo lazima uwe na taswira ya nchi .Na pia hvo vipindi wanavyojidai kuwa vinaongoza vinasaidia nini kumsaidia mwananchi au ni kumwongezea ujinga
 
Utafiti wa hii tasisi umeniacha hoi sana yani mi naipenda sana Clouds Fm lakini si kweli kuwa wao ni bora kwa kila kitu na watangazaji wao ni bora kuliko wote na vipindi vyao ni bora kuliko vyote.
Yani washikirie namba moja kila kipindi na kwa kila mtangazaji kweli hapa Tanzania?

Nina mashaka na huu utafiti duu huwa nikisikia nacheka sana.
 
yaani mim nikisikia haya matangazo yao ya kujisifu naishia kucheka tu
 
Naipenda Clouds Fm kusikiliza baadhi ya vipindi ila kwa kusema eti kila kipindi wanashika namba moja hiyo ndo siamini ,,wanajiboost
 
Ukisikia mtu anajitengenya alafu anacheka mwenyewe ndo hii clouds ,wanatafuta sifa za kijinga.
 
Binafsi nimeshawahi kufanya kazi na SYNOVATE/IPSOS, kale kautaratibu kao ka-malipo kiduchu ya kinyonyaji huwafanya wakusanya takwimu wao [vibarua] kupika data. Ile menejimenti yao ya wakenya [iliyokuwepo miaka ya 2009] haikuwa vizuri sana. japo wana media monitoring room, sina uhakika na takwimu zao. Kusema kweli tangu nifanye nao kazi na kuwaelewa vizuri siamini tena tafiti zao Mugabe wa Bongo

Hivi Aggery Awori bado yuko...Honolata je..?....

Hawa jamaa zamani walikua wanajiita Steadman...baadae synovate...na sasa ipsoss
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom