Karibu sana Mwakaleli, kwenye neema ya watu wakarimu, mito mingi, mvua nyingi na ardhi yenye rutuba. Kunastawi sana viazi, magimbi, chai, maparachichi na ndizi. Hali ya hewa safi na utulivu. Ni kama Lushoto, Amani (Muheza), Marangu, Machame, Rombo au Muleba, hususan Kamachumu.
Usafiri wa uhakika kuanzia alfajiri hadi jioni kila siku kuelekea Tukuyu, Mbeya au Kyela. Mitandao yote ya simu inakamata. Barabara ya kokoto na inapitika muda wote. Ila iko mbioni kuwekwa lami tokea Katumba kiasi cha km 35
Naweza kukuuzia ekari moja karibu na barabara, umeme wa REA umepita hapohapo pamoja na maji ya bomba. Karibu tena!