Naomba kujuzwa fursa za kiuchumi,changamoto na na faida za kuishi Mkoa wa Katavi hasa Wilaya ya Mlele

Naomba kujuzwa fursa za kiuchumi,changamoto na na faida za kuishi Mkoa wa Katavi hasa Wilaya ya Mlele

Holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
6,716
Reaction score
13,702
Wakuu,

Mimi ni mwajiriwa natokea mkoa wa Manyara,nimehamishiwa kikazi mkoa wa Katavi wilaya ya Mlele.

Naomba mnijuze ni fursa gani naweza fanya ya kujipatia kipato nje na ajira yangu kada ya ualimu?

Je, kuna changamoto gani za kuishi katika mkoa huu?

Ninapokwenda huko nikajiepushe na mambo gani na nikafanye mambo gani ili nibaki safe?

Natanguliza shukrani na Watu wa katavi nipokeeni ktk mkoa wenu.
 
Kilimo, ufugaji na biashara.
Jiepushe na uchawi.
Karibu sana Mlele, Karibu Mpanda.
 
1. Kilimo cha mazao kama Tumbaku, karanga na mpunga.
2. Ufugaji (kuku na nguruwe), kwa sababu chakula kinapatikana kwa urahisi. Pia ufugaji wa nyuki.
3. Biashara ya nafaka.
4. Uwakala wa huduma za fedha na vifaa vya simu.
Fanya haya utatoboa! Mkoa wa Katavi na wilaya zake unakua kwa kasi sana,maeneo ni mengi bei mtelezo,ardhi ni very arable...kapambane upate maeneo ulime mpunga,Karanga,Tumbaku na mahindi unatoboa mzee
 
Wakuu,

Mimi ni mwajiriwa natokea mkoa wa Manyara,nimehamishiwa kikazi mkoa wa Katavi wilaya ya Mlele.

Naomba mnijuze ni fursa gani naweza fanya ya kujipatia kipato nje na ajira yangu kada ya ualimu?

Je, kuna changamoto gani za kuishi katika mkoa huu?

Ninapokwenda huko nikajiepushe na mambo gani na nikafanye mambo gani ili nibaki safe?

Natanguliza shukrani na Watu wa katavi nipokeeni ktk mkoa wenu.
Walimu hawahamishwi kirahisi mkuu kwanza serikali inakwepa gharama za uhamisho.
Wewe sema uliomba kuhama mwenyewe.
 
Mimi pia nahamia Mlele, sehemu inaitwa Ilunde. Nakwenda kuanzisha kiwanda cha kuchakata asali na nta. Nimefanya tafiti miaka miwili kule, kuanzia Uruwira, Utende, Inyonga mpaka Ilunde.
Kuna fursa nyingi, ukifika kama una kichwa chepesi utaziona mwenyewe na utachagua ipi itakufaa.
Karibu Mlele.
 
Mimi pia nahamia Mlele, sehemu inaitwa Ilunde. Nakwenda kuanzisha kiwanda cha kuchakata asali na nta. Nimefanya tafiti miaka miwili kule, kuanzia Uruwira, Utende, Inyonga mpaka Ilunde.
Kuna fursa nyingi, ukifika kama una kichwa chepesi utaziona mwenyewe na utachagua ipi itakufaa.
Karibu Mlele.
Mkuu habari kaka naulizia ivi haya madagaa na furu zinalika kweli huko mlale
 
Kaka Mimi ni mfanyabiashara wa dagaa na furu WAKAVU na WALIOKAANGWA kaka saizi masoko mengi ya huku Kanda ya ZIWA yamefurika natamani kuuingia huko nijaribu hususani kwenye maeneo ya wakulima na wafugaji WENGI hasa wasukuma tafadhali naomba kama una abc za mavijiji ya huko niambie
 
  • Thanks
Reactions: apk
Back
Top Bottom