Naomba kujua tafsiri ya ndoto hii

Mtuache

JF-Expert Member
Mar 12, 2021
251
638
Habari za muda huu wana JF

Mwenye elimu kuhusu haya mswala au mwenye uzoefu wowote Naomba kujua maana ya hii ndoto. Nitaandika vile ninavyovikumbuka, vinaweza visiwe na mtiririko mzuri lakini nitajitidi muweze kuielewa

Niliota nimepewa taarifa ya msiba wa mtu ambae niwa karibu yangu sana, mtu niliempenda sana, (mzazi wangu) . Cha ajabu sikustuka wala kulia. Tukiwa njiani kuelekea msibana mahali ambapo watazika nikakumbuka kuwa niliyeambiwa amefariki alishafariki miaka mingi iliyopita

Nikapata mstuko, nikamuuliza mtu aliyekaribu yangu "samahani mbona huyu tunaeenda kumzika leo alishafiriki miaka mingi, imekuaje?" akanijibu "hapana aliyefariki ni mwingine ila majina yanafanana tu"

Baada ya kujibiwa hivyo ghafla mwili wa marehemu ukawa umewasili wakaenda kuupokea na kufanya maandalizi ya kuaga pamoja na kuzika. Cha ajabu aliyefariki hakuwa mmoja kama nilivyodhani bali walikuwa watu wawili.

Muda wa kuaga ulipofika mimi nilikataa kwenda kuaga, nililazimishwa sana tena sana ila nikajikuta nakataa huku nikadai eti aliyefariki sikuwa namjua wala simfahamu ya nini nimuage. Watu walinishangaa na kuniacha

Nilipojaribu kuwaangalia kwa mbali wale waliofariki ambao watu wanasema wamefanana majina na yule niliedhani kafa muda mrefu, nilistuka sana kwa jinsi nilivyowakuta.

Kwanza majeneza yao yalikuwa tofauti na majeneza ya watu wengine, yalikuwa yanawaonesha mwili mzima. Alafu sasa mmoja kati ya wale marehemu wawili alikuwa amelala chali lakini mikono kaichanua huku na huko. Marehemu wa pili alilala kawaida kama marehemu wengine wanavyolazwa.

Cha ajabu yule alielala kawaida akaamka, lakini watu hawakustuka wala kukimbia ni kama hawakuona chochote. Mimi nilistuka sana, mpaka yule marehemu akaniona. Akaniuliza "wewe unaniona.?" nikamjibu ndio kwa kutikisa kichwa

Alikasirika sana, akakunja sura akaniuliza tena nikamjibi hivyo hivyo. Safari ya tatu akawa anamtikisa marehemu mwenzake na kumwambia "huyu anatuona, amka kuna mtu anatuona....." akawa anamwambia huku ananisogelea na sura kaikunja kwa hasira.

Nilipata hofu ya ajabu na ghafla nikastuka usingizini, nilikuwa nahema kwa nguvu moyo unadunda na natokwa jasho jingi.

Kiukweli hii ndoto nimeota muda kidogo kama miezi miwili hivi lakini mpaka leo inanitesa. Kila nikikaa mwenyewe naikumbuka. Nimeota ndoto nyingi za kutisha tena zaidi ya hii lakini hii nashangaa haitoki kichwani mwangu.

Naomba mwenye kujua maana yake, au anaemjua mtu anaeweza niambia maana yake amTag. Nahitaji kujua. ASANTENI
 
Mh, ngoja tuendelee kuwavutia subra wajuzi lkn nina uhakika kuna ujumbe wa wazi hapo unapewa uufanyie kazi.

Tangu niote nalishwa chura mbichi na siku nyingine kinyonga aliyekaushwa (ungua moto), na nilipoamka sikuwa sawa siku nzima (yaani tumbo limevurugika vibaya), nilijua kuwa ulimwengu si mchezo
 
Ndoto yenye ujumbe haiwezi kuwa ndefu hivyo...ninavyojua mimi ndoto yenye ujumbe mara nyingi huwa ni fupi sana... hivyo usisumbuke kutafuta tafsiri.. kibaya zaidi miaka ya Hivi karibuni watu wenye uwezo wa kutafsiri ndoto ni wachache sana
 
Nakushauri tu, ukiingia ndotoni usisahau kubeba video camera, ndoto nyingine ukizi film utapata pesa nyingi sana.

Tuweke utani kando, je unatoka ukoo wa namna gani? Je ni wankichifu, wa masherifu au wa kilokole?

Je wewe ni wa kwanza kuzaliwa? Nauliza hivi kwasababu kwanini Ile maiti haikumuuliza mtu mwingine kama wameonekana?

Muombe Mwenyezi Mungu akusaidie kukutafsiria ndoto yako, yeye peke yake ndiye mtatua mafumbo
 
Habari za muda huu wana JF

Mwenye elimu kuhusu haya mswala au mwenye uzoefu wowote Naomba kujua maana ya hii ndoto. Nitaandika vile ninavyovikumbuka, vinaweza visiwe na mtiririko mzuri lakini nitajitidi muweze kuielewa..
Kuna mazingatio hapo katika ndoto yako na ndiyo maana haikutoki kichwani...!Unganisha vipande katika ndoto zote unazoota mara nyingi na utafakari ni ndoto za namna gani,jibu utapata.
 
Nakushauri tu, ukiingia ndotoni usisahau kubeba video camera, ndoto nyingine ukizi film utapata pesa nyingi sana.

Tuweke utani kando, je unatoka ukoo wa namna gani? Je ni wankichifu, wa masherifu au wa kilokole?

Je wewe ni wa kwanza kuzaliwa? Nauliza hivi kwasababu kwanini Ile maiti haikumuuliza mtu mwingine kama wameonekana?

Muombe Mwenyezi Mungu akusaidie kukutafsiria ndoto yako, yeye peke yake ndiye mtatua mafumbo
Haya maswali niya muhinu ..
Wewe dini gan?
Pia na wewe to be honestly ni mshika dini ambae hujihusishi na mambo ya waganga wa kienyeji? Au unajihusisha/kwenda kwa waganga wa kienyeji (ushirikina?)
 
Me ndoto zangu huwa natafsiri mwenyewe, ingawa inanichukuaga muda mrefu Sana

Nakumbuka kuna ndoto niliwahi ota kuhusu mahusiano na binti mmoja niliyekua naye

Ile ndoto ilinionyesha Mimi na yule binti tupo kwenye kifaa kinachofanana na byke na aliyekuwa anaendesha niyule binti, chaajabu uendeshaji wake ulikuwa siyo wa kawaida yaani alikua ananipeleka kwenye Makorongo
Nakawa namwambia huku siko unakoenda akawa mbishi, hatimaye mi nikaruka nakumuacha aende

Chaajabu alitumbukia kwenye korongo lefu Sana, asa niliposhuka kwenda kumuangalia nilimkuta kavunjika vpande vpande na kile kifaa alichokua anaendesha kilivunjika Sana.

Amini usiamini haikupita mwaka me nayule binti mahusiano yalivunjika na muhanga alikuwa yeye kwani alikonda Sana kwa kuniwaza na kukosa huduma nilizokuwa Nampa.
 
Aiseee. Mm c mtalaamu wa kutafsiri ndoto ila nahisi baadhi ya mambo!

Kwanza. Ulipewa habari za msiba wa ndugu yako wa karb ila hukushituka--kitu kisichoshitua moyo ni ishara kuwa hakipo au si kweli/hakiwezi kikatokea.
Pili. Lakini ukakumbuka kuwa huyo mtu alishafariki muda mrefu---hii ndo mana hukushituka baada ya kusikia habr za kifo chake saizi na kiimani inamanisha huyo mtu alishaanguka muda mrefu/imani haipo na yawezekana huyo mtu kimwili alishafariki
Tatu. Ulikumbuka alishakufa na ukaambiwa ni kweli si yeye ila wanafanana majina--kiimani anguko alilolipata huyo uliyemwota pia ni anguko linaloenda kumtokea mtu wa karb yake mme/mke. Kwanini mume au mke? Hawa ni kitu kimoja kiroho hivyo ata kuitwa kwa jina moja ni sawa mana n mwili mmoja na hivyo wanafanana. Mungu hukupa mke/mume wa kufanana nawe.
Nne. Lakini ukaamua kushiriki mazishi ya mtu usiyemjua na kumbe siyo mmoja ni wawili---hii inamaana huyo ambaye amebeba maono ya ndoto yako ni ndugu wa karb ndiyo maana umehudhuria, lakini si mmoja n wawili inamanisha maelezo no tatu.
Tano. Majeneza yametofautiana---ni kwasababu mmoja ni me/ke
Sita. Yamefunuliwa yote---mazishi yao ni ya tofaut na mazishi ya kibinadamu wa kawaida.
Saba. Uligoma kwenda kuaga---ni kwasababu wewe n binadamu wa kawaida huwezi kushiriki uagaji wa maiti kwa watu wasio wa kawaida.
Nane. Ulivyomjibu unamuona alikuwa mkali--- huyu bila shaka ndiye aliyekuwa amefariki muda mrefu kwa kifo kisicho cha Mungu na anatumikishwa na watu wengine! Alikuwa mkali kwa maana hilo lilikuwa ni tukio lisilohusu binadamu wa kawaida ila wewe roho wa Bwana alikupanda ili kuvuruga hilo tukio na anataka hilo tukio lisitokee.
Tisa. Alianza kumwamsha mwenzake akidai unawaona na akawa mkali---ni kwasababu huyo aliyelala na hajui linaloendelea kwan alichukuliwa na huyo aliyekuuliza ikiwa unamwona, na hata angekuwa mkali kivipi ila asingeweza kukudhuru kwa maana wewe ww ulikuwa na roho wa Bwana.

Mwisho: kuna mtu wako wa karb alishafariki kimwili ila roho yake bado inatumikishwa/mlimzika kwa macho ya kawaida ila bado anaishi kwa macho ya kiroho/yasiyo ya kawaida(kichawi huyo n msukule), sasa huyo msukule ndiye anahitaji kumchukua mpendwa wake na mpaka hapo yupo hatua za mwisho kabisa. Hivyo wewe ndiye unatakiwa kuvuruga hiyo mipango kama ulivyoivuruga kwa jarbio la kwanza ila bado huyo msukule bado ataendelea kumhitaji mpendwa wake. Zidisha imani zaidi utafanikiwa.
 
Ndoto zina maana kubwa mkuu!! Usiipuze!!!
Njoo inbox nitakusaidia maana ya hiyo ndoto!! Ni maswala ya imani, uliyemuota Kafa mda mrefu, ni kweli alikufa mrefu sema alikufa kabla ya mda wake kufika!! Hivyo Roho yake bado ilikuwa inatangatanga duniani
 
Aiseee. Mm c mtalaamu wa kutafsiri ndoto ila nahisi baadhi ya mambo!

Kwanza. Ulipewa habari za msiba wa ndugu yako wa karb ila hukushituka--kitu kisichoshitua moyo ni ishara kuwa hakipo au si kweli/hakiwezi kikatokea.
Pili. Lakini ukakumbuka kuwa huyo mtu alishafariki muda mrefu---hii ndo mana hukushituka baada ya kusikia habr za kifo chake saizi na kiimani inamanisha huyo mtu alishaanguka muda mrefu/imani haipo na yawezekana huyo mtu kimwili alishafariki
Tatu. Ulikumbuka alishakufa na ukaambiwa ni kweli si yeye ila wanafanana majina--kiimani anguko alilolipata huyo uliyemwota pia ni anguko linaloenda kumtokea mtu wa karb yake mme/mke. Kwanini mume au mke? Hawa ni kitu kimoja kiroho hivyo ata kuitwa kwa jina moja ni sawa mana n mwili mmoja na hivyo wanafanana. Mungu hukupa mke/mume wa kufanana nawe.
Nne. Lakini ukaamua kushiriki mazishi ya mtu usiyemjua na kumbe siyo mmoja ni wawili---hii inamaana huyo ambaye amebeba maono ya ndoto yako ni ndugu wa karb ndiyo maana umehudhuria, lakini si mmoja n wawili inamanisha maelezo no tatu.
Tano. Majeneza yametofautiana---ni kwasababu mmoja ni me/ke
Sita. Yamefunuliwa yote---mazishi yao ni ya tofaut na mazishi ya kibinadamu wa kawaida.
Saba. Uligoma kwenda kuaga---ni kwasababu wewe n binadamu wa kawaida huwezi kushiriki uagaji wa maiti kwa watu wasio wa kawaida.
Nane. Ulivyomjibu unamuona alikuwa mkali--- huyu bila shaka ndiye aliyekuwa amefariki muda mrefu kwa kifo kisicho cha Mungu na anatumikishwa na watu wengine! Alikuwa mkali kwa maana hilo lilikuwa ni tukio lisilohusu binadamu wa kawaida ila wewe roho wa Bwana alikupanda ili kuvuruga hilo tukio na anataka hilo tukio lisitokee.
Tisa. Alianza kumwamsha mwenzake akidai unawaona na akawa mkali---ni kwasababu huyo aliyelala na hajui linaloendelea kwan alichukuliwa na huyo aliyekuuliza ikiwa unamwona, na hata angekuwa mkali kivipi ila asingeweza kukudhuru kwa maana wewe ww ulikuwa na roho wa Bwana.

Mwisho: kuna mtu wako wa karb alishafariki kimwili ila roho yake bado inatumikishwa/mlimzika kwa macho ya kawaida ila bado anaishi kwa macho ya kiroho/yasiyo ya kawaida(kichawi huyo n msukule), sasa huyo msukule ndiye anahitaji kumchukua mpendwa wake na mpaka hapo yupo hatua za mwisho kabisa. Hivyo wewe ndiye unatakiwa kuvuruga hiyo mipango kama ulivyoivuruga kwa jarbio la kwanza ila bado huyo msukule bado ataendelea kumhitaji mpendwa wake. Zidisha imani zaidi utafanikiwa.
Naomba na hii nichanganulie
Kuna siku nilila mahala Fulani ghafla ikaja picha ktk ndoto
Nikamuona ndg yangu wakike amekaa kwenye sofa akiwa kafunga kanga kuanzia kwenye matiti kushuka chini huku aking'ata vidole vyake.
 
Ndoto zina maana kubwa mkuu!! Usiipuze!!!
Njoo inbox nitakusaidia maana ya hiyo ndoto!! Ni maswala ya imani, uliyemuota Kafa mda mrefu, ni kweli alikufa mrefu sema alikufa kabla ya mda wake kufika!! Hivyo Roho yake bado ilikuwa inatangatanga duniani
Nimekuja inbox mkuu
 
Me ndoto zangu huwa natafsiri mwenyewe, ingawa inanichukuaga muda mrefu Sana

Nakumbuka kuna ndoto niliwahi ota kuhusu mahusiano na binti mmoja niliyekua naye

Ile ndoto ilinionyesha Mimi na yule binti tupo kwenye kifaa kinachofanana na byke na aliyekuwa anaendesha niyule binti, chaajabu uendeshaji wake ulikuwa siyo wa kawaida yaani alikua ananipeleka kwenye Makorongo
Nakawa namwambia huku siko unakoenda akawa mbishi, hatimaye mi nikaruka nakumuacha aende

Chaajabu alitumbukia kwenye korongo lefu Sana, asa niliposhuka kwenda kumuangalia nilimkuta kavunjika vpande vpande na kile kifaa alichokua anaendesha kilivunjika Sana.

Amini usiamini haikupita mwaka me nayule binti mahusiano yalivunjika na muhanga alikuwa yeye kwani alikonda Sana kwa kuniwaza na kukosa huduma nilizokuwa Nampa.
Duuuh
 
Wachana na hiyo me majuz tu niliota mtu katoa mimba ya mtu flani na WOTE nawafaham japo sikutarajia kuwa yule MDADA anaweza pata mimba na kuitoa na nikwel ikaja kungundulika
Pili niliota mtu wa kalibu yangu anawatoto wawili nje ya ndoa yake yaani kazaa na MWANAMKE mwingine na nilivyo ota hivyo niliuchuna chuu siku inakuja kugundulika me naangalia marudio ya movie yangu ila jaman duniani hakuna siri me huwaga nawaangaliaga tu watu wanavyo jifanya wana siri kumbe mwenzao naoteshwa kila kitu yafanyike kimwili ama kiroho ashukuliwe Mungu ananifundisha
 
Back
Top Bottom