Naomba kujua changamoto za kufunga Turbocharger kwenye gari

utapenda wakati inafungua turbo? turbo mda wote ipo on as long as gari imewasha sema haisikiki at lower rpm
Mkuu Hilux Surf zinazotumia engine ya 2L-TE ukiwa una accelerate RPM ikifika juu ya 2 kwenye dashboard inawaka taa ya kijani ilioandikwa turbo gia ikishabadilika vivyo hivyo inazima na ukiendelea ku accelerate kwenye speed zaidi ya hio Turbo inawaka..1KZ-TE yenyewe turbo yake ipo direct..kwenye dashboard hakuna alama ya turbo ipo on au off..unaweza ukaelezeaje hapo? Kuweka rekodi sawa kuna baadhi ya Prado II zinazotumia 2L-TE nazo zinazo hio alama ya kuonesha turbo imewaka au haijawaka...
 
1. Wakuu vipi kuhusu turbocharger kwenye magari ya 660cc mfano Suzuki K6A, Pajeeo mini.

2. Je gari yenye cc ndogo na turbo inaweza kwenda safari ndefu mfano 700km?

3. Je gari (660cc) yenye turbo na isiyo kuwa na turbo ipi itaweza kumudu safari ndefu bila madhara?
Yenye turbo ni bora zaidi, inaenda umbali huo ila usiwe na haraka
 
Back
Top Bottom