Naomba kufahamu mmiliki wa IFM (CHUO)

Naomba kufahamu mmiliki wa IFM (CHUO)

igulwibi

Member
Joined
Mar 21, 2012
Posts
56
Reaction score
9
Hiki chuo ni binafsi au kipo chini ya serikali? Inakuwaje hakitambui sherehe zinazotambuliwa na serikali kama nane nane? Eti kesho wanafunzi wapo masomoni. Naomba ufahamu wana JF
 
Una maswali mawili katika swali moja.Binafsi nakujibu moja:ni cha serikali.
 
ni cha serikali chini ya wizara ya fedha. Mbona kama kimefungwa au watu wa sapu nini!.
 
Hiki chuo ni binafsi au kipo chini ya serikali? Inakuwaje hakitambui sherehe zinazotambuliwa na serikali kama nane nane? Eti kesho wanafunzi wapo masomoni. Naomba ufahamu wana JF

Naona hapa unachanganya vitu viwili: umiliki wa chuo na utashi wa viongozi/watendaji wa chuo kuheshimu sikukuu za kitaifa. Kimsingi haya ni mambo mawili tofauti ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja. Tatizo hapa si nani anamiliki chuo, bali ni kwa nini uongozi wa chuo unashindwa kuheshimu sikukuu za kifaifa? Nafahamu IFM ni mali ya serikali chini ya wizara ya fedha. Sasa kwa nini mkuu wa chuo na management yake wameamua kesho muendelee na masomo ndio swali unaloweza kutafutia majibu kutoka kwenye uongozi wa chuo na sio JF
 
hiki chuo ni binafsi au kipo chini ya serikali? Inakuwaje hakitambui sherehe zinazotambuliwa na serikali kama nane nane? Eti kesho wanafunzi wapo masomoni. Naomba ufahamu wana jf

piga kitabu dogo hayo ni mapito tu mwisho wa siku ondoka na nondo yako maisha yanaendelea
 
Chuo kilikua Mali ya bank ya nbc. ..then serikali Chini ya wizara ya fedha wakakichukua....ni Mali ya serikali
 
Naona hapa unachanganya vitu viwili: umiliki wa chuo na utashi wa viongozi/watendaji wa chuo kuheshimu sikukuu za kitaifa. Kimsingi haya ni mambo mawili tofauti ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja. Tatizo hapa si nani anamiliki chuo, bali ni kwa nini uongozi wa chuo unashindwa kuheshimu sikukuu za kifaifa? Nafahamu IFM ni mali ya serikali chini ya wizara ya fedha. Sasa kwa nini mkuu wa chuo na management yake wameamua kesho muendelee na masomo ndio swali unaloweza kutafutia majibu kutoka kwenye uongozi wa chuo na sio JF

Hili jibu lilifaa kuifunga kabisa hii thread.
Shukrani chief yaani siku hizi vijana wanakurupuka tu kuanzisha mada jf,Iwapi jf ya 2005 kushuka chini,mods threads nyingine ni za kuzitupia shimoni.
Mtu kakurupuka from nowhere huyo kuanzisha thread hapa.
KINYAAA.
 
Activister. Usipende kukashifu hoja za wenzio. Kama huna jibu la hoja kaa kimya wenye majibu wajibu. Nawashukuru mliochangia hoja. Nimepata jibu.
 
Back
Top Bottom