Ndugu wana JF naomba kufahamishwa kuhusu upatikanaji wa passport ya kusafiria kwenda nje ya nchi kama South Afrika. kwa muda gani naweza kupata passport na vip gharama zake zinakuaje? Kwa anaefahamu tafadhari anijulishe kwa hili.
Usi pm mtu yoyote. na usitoe rushwa hhata elfu moja kwani utakayempa hela hahusiki na pp. Nenda pale Kurasini uhamiaji. jaza fomu. lipa elfu hamsini na ndani ya siku saba za kazi utapata pasport halali. Jiepushe na walaghai utapewa pp pori. any problem please ni PM mimi nimuwashie mtu moto hatakaa aausahau mapema
Kama unacheti cha Daktari kwamba unakwenda kutibiwa au kusindiiza mgonjwa au barua yoyote ya kionyesha dharula hata ndani ya siku moja unapata PP. Idara ya uhamiaji imejirekebisha mno mkuu. na ukimpa mtu rushwa pale Kurasini nakuhakikishia atawatonya TAKUKURU pale pale.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.