Nimewatazama wazee wangu pamoja na marafiki zangu ambao ni wazee, nimegundua miili yao haiongezeki zaidi ya kupukutika; ile minofu iliyokuwa inaficha mifupa inapotea.
Sasa najiuliza swali kwa hawa wazee wangu, kwa nini umri unavyozidi kusogea ndio miili yao inarudi utotoni/ inakuwa midogo?
Wanajitahidi kula vizuri, lakini bado nyama zinapukutika na mifupa kuonekana.
Kama uzee ndio unakuja na changamoto hizi, nini maana ya maisha sasa?
Mpaka sasa naogopa kuzeeka