Mama Sabrina
JF-Expert Member
- Jul 30, 2016
- 16,621
- 27,567
Jamani nikiona Agness amefariki akiwa mdogo nasikitika kiukweli,vifo vya vijana wadogo vinauma sana ,nikiona mwanae naumia kaachwa hana hata kaka au dada yake ,nikifikiria na mimi mtoto wangu yupo mwenyewe tu ikatokea nikafa atakimbilia kwa nani, Mungu nijaalie hata mwaka huu tu nibebe mimba nyingine ikiwezekana nizae hata mdogo wake au wadogo zake wawili hata wa kulia nao pamoja abaki nao,akipata hata shida awe na ndugu zake , mimi mwenyewe nikiwa na matatizo namlilia kaka yangu napiga simu nalia kweli au kama akiwa karibu nae namlilia mno ananibembeleza na kunifariji ananiambia mimi kaka yako nipo usilie,natamani iwe kwa mwanangu sijakata tamaa naamini ntapata tu ,maana mi nikifikiria akibaki mwenyewe naumia kweli maana najua hapa kwenye kifo hakuna kuchenga ,najua siku moja nami nitakufa japo naipinga sana hii roho lakin Mungu ndio mwenye kujua.
Na mnavyojua mkizaliwa tumbo moja kwa mama nyie ndio ndugu kabisa, sitaki kumuacha mwenyewe najua uzazi wangu wa ni shida sana sijui kama nitabeba mimba nyingine tena labda itatokea bahati nitabeba tena mpaka sasa alitakiwa hata wawe wawili tu ,ila malengo yangu kama siku nikibeba mimba ntazaa haraka wawili,malengo yangu ni kuwa na watoto watatu tu.
Mpaka mama yangu aliniambia siku moja hivi mwanangu utazaa kweli tena mbona hata sioni dalili ,japo nashukuru hata kwa huyu mmoja maana kuna wengine hawana hata huyu mimi nilienae, kwanin wengine kidogo tu wanazaa kama kuku anavyototoa na kwanini wengine ukishazaa ka moja tu ndio basi tena nna ndugu zangu kama watano hawajazaa na umri umeenda sidhan kama watazaa,nna mama yangu mkubwa nae ana mtoto mmoja tu hakuzaaga tena mpaka leo ana wajukuu tu
Najiulizaga ningetoa hii mimba ingekuwaje?ndio maana hata aniite single mother huwa siumii kabisa na sijali naonaga mnavyotunanga lakin wengine hatukutaka kuchoropoa mimba
Nashukuru mpenzi wangu G kuniambia hata nisipozaa ni sawa tu ananipenda nilivyo na hatoniacha kisa kuzaa. mwaka huu nitajaribu tena nione kama itaingia,ikiingia tu nazaa hata watatu haraka haraka
Mwanangu huwa ananiambia "mama nizalie mdogo wangu na mimi "yaan ananichoma ka moyoo akisema vile
Sawa basi hata nikiwa na haka ka moja tu niwepo tu kama mama yake Hamisa Mobeto,alimzaa hamisa peke yake tu lakin kamlea mpaka kapata wajukuu Mungu tuhurumie basi
Vifo vinaumiza sana hasa za vijana wadogo ambao ndio tegemeo la taifa ,Mola mkuzie huyo mtoto alieachwa na Masogange ampe ufariji nayahisi maumivu yake makali sana huyu mtoto ,Mungu angejuaga asingeweka vifo sijui alifikiria nini jamani anatuumiza sana tunapotelewa na watu wetu tunaowapenda .basi bana leo siku yangu mbaya kweli jamani ,kuna hii nyimbo huniliza sana ya Ambwene -Misuli ya imani yaan unafikiria wapendwa wako wote waliofariki
UPUMZIKE KWA AMANI AGNESS MASOGANGE
Na mnavyojua mkizaliwa tumbo moja kwa mama nyie ndio ndugu kabisa, sitaki kumuacha mwenyewe najua uzazi wangu wa ni shida sana sijui kama nitabeba mimba nyingine tena labda itatokea bahati nitabeba tena mpaka sasa alitakiwa hata wawe wawili tu ,ila malengo yangu kama siku nikibeba mimba ntazaa haraka wawili,malengo yangu ni kuwa na watoto watatu tu.
Mpaka mama yangu aliniambia siku moja hivi mwanangu utazaa kweli tena mbona hata sioni dalili ,japo nashukuru hata kwa huyu mmoja maana kuna wengine hawana hata huyu mimi nilienae, kwanin wengine kidogo tu wanazaa kama kuku anavyototoa na kwanini wengine ukishazaa ka moja tu ndio basi tena nna ndugu zangu kama watano hawajazaa na umri umeenda sidhan kama watazaa,nna mama yangu mkubwa nae ana mtoto mmoja tu hakuzaaga tena mpaka leo ana wajukuu tu
Najiulizaga ningetoa hii mimba ingekuwaje?ndio maana hata aniite single mother huwa siumii kabisa na sijali naonaga mnavyotunanga lakin wengine hatukutaka kuchoropoa mimba
Nashukuru mpenzi wangu G kuniambia hata nisipozaa ni sawa tu ananipenda nilivyo na hatoniacha kisa kuzaa. mwaka huu nitajaribu tena nione kama itaingia,ikiingia tu nazaa hata watatu haraka haraka
Mwanangu huwa ananiambia "mama nizalie mdogo wangu na mimi "yaan ananichoma ka moyoo akisema vile
Sawa basi hata nikiwa na haka ka moja tu niwepo tu kama mama yake Hamisa Mobeto,alimzaa hamisa peke yake tu lakin kamlea mpaka kapata wajukuu Mungu tuhurumie basi
Vifo vinaumiza sana hasa za vijana wadogo ambao ndio tegemeo la taifa ,Mola mkuzie huyo mtoto alieachwa na Masogange ampe ufariji nayahisi maumivu yake makali sana huyu mtoto ,Mungu angejuaga asingeweka vifo sijui alifikiria nini jamani anatuumiza sana tunapotelewa na watu wetu tunaowapenda .basi bana leo siku yangu mbaya kweli jamani ,kuna hii nyimbo huniliza sana ya Ambwene -Misuli ya imani yaan unafikiria wapendwa wako wote waliofariki
UPUMZIKE KWA AMANI AGNESS MASOGANGE