Nanyaro ateuliwa kuongoza CHADEMA Arusha mjini

Nanyaro ateuliwa kuongoza CHADEMA Arusha mjini

Mwan mpambanaji

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2008
Posts
482
Reaction score
131
Ndugu wanaJf
Habari za uhakika kutoka kwenye baraza la uongozi la chadema mkoa,lililokaa kwa siku mbili mfululizo,kujadili hali halisi ya kisiasa Arusha mjini,limegundua makosa mengi ya kiuongozi ngazi ya wilaya,na mara baada ya majadiliano kamati tendaji yote ya wilaya ikaamua kujiuzulu kwa hiari, ili kupisha viongozi wapya.

Hivyo Nanyaro ambaye ni diwani wa Levolosi na mmoja wa vijana wenye ushawishi mkubwa wa siasa za upinzani Arusha mjini, kuteuliwa kuongoza task force ya wilaya,yenye lengo la kuimarisha chama, na kuratibu zoezi la uchaguzi wa wilaya.

Hata hivyo mwenyekiti wa mkoa amesisitiza kuwa CHADEMA ni imara,na Nanyaro ameteuliwa kwa kuwa ni mmoja wa viongozi wanaokijua chama Arusha kwa undani,na mwenye rekodi nzuri ndani ya chama
 
Tunamtakia Nanyaro afya njema, aweze kulisongesha gurudumu vema..!
 
Ndugu wanaJf
Habari za uhakika kutoka kwenye baraza la uongozi la chadema mkoa,lililokaa kwa siku mbili mfululizo,kujadili hali halisi ya kisiasa Arusha mjini,limegundua makosa mengi ya kiuongozi ngazi ya wilaya,na mara baada ya majadiliano kamati tendaji yote ya wilaya ikaamua kujiuzulu kwa hiari, ili kupisha viongozi wapya.

Hivyo Nanyaro ambaye ni diwani wa Levolosi na mmoja wa vijana wenye ushawishi mkubwa wa siasa za upinzani Arusha mjini, kuteuliwa kuongoza task force ya wilaya,yenye lengo la kuimarisha chama, na kuratibu zoezi la uchaguzi wa wilaya.

Hata hivyo mwenyekiti wa mkoa amesisitiza kuwa CHADEMA ni imara,na Nanyaro ameteuliwa kwa kuwa ni mmoja wa viongozi wanaokijua chama Arusha kwa undani,na mwenye rekodi nzuri ndani ya chama

Hivi utaratibu ukoje ndg zangu? kikao kilichokaa jana kilikuwa cha kamati tendaji ya mkoa, imekuwaje ikajadili suala la wilaya ya arusha peke yake? vipi kuhusu wilaya zingine?

Hata hivyo napongeza zoezi hilo kutokana na kwamba kulikuwa hakuna mawasiliano mazuri ya chama kutoka wilaya kwenda mkoani, na kutoka wilaya kwenda kata. hongereni sana
 
Hivi utaratibu ukoje ndg zangu? kikao kilichokaa jana kilikuwa cha kamati tendaji ya mkoa, imekuwaje ikajadili suala la wilaya ya arusha peke yake? vipi kuhusu wilaya zingine?

If not broken don't fix it
 
Ukitaka kula asali fuata nyuki hongera Nanyaro hayo ni matunda ya uaminifu.
 
hivi cdm huwa hawana matawi? mbonasijasikia wakifanya chaguzi!!
 
Mh. Nanyaro nakuheshimu sana na nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya kwa ajili ya chama.Na kitu kingine kinachonifurahisha ni kutokujiona we bora na mifano ni jinsi we na madiwani wengine wachache mlipoomba radhi kama mlivyotakiwa na uongozi wa taifa bila kinyongo.

Pia ni kwa jinsi unavyojitokeza humu jamvini kujibu maswali unayokuwa umeulizwa aidha shutuma na mambo mengine ya chama kwa wakati. Pia jinsi ulivyo na ushirikiano mzuri na wenzako hadi kupewa nafasi hizo nyeti mkoani na wilayani.

Nakuombea kwa Mungu akuzidishie.
 
Afanye kazi na kuondoa migogoro,tumechoka kelele jamani na kupewa jina la kuwa cdm ni wazee wa fujo.hongera.
 
Nawashukuru sana kwa pongezi zenu za dhati,natambua matarajio makubwa ya umma unaotamani migogoro ya chadema iishe, kimsingi kikao cha siku mbili kilikuwa cha baraza la mashauriano ya mkoa, kilizungumzia wilaya zote,na hali ya kisiasa kwenye wilaya zote za mkoa wa Arusha zinaendelea kutekeleza maazimio ya chama kama tulivyokubaliana kwenye baraza la 1april, kwa Arusha mjini baraza likagundua matatizo mbalimbali ya kiuongozi, ndipo kamati tendaji ikaridhia kujiuzulu ili kupisha uchaguzi wa watu watakaoweza kukiimarisha chama zaidi, hasa ikizingatiwa hali ya Arusha mjini ilivyo
Nashukuru kuwa viongozi wenzangu wamenipa heshima hii kubwa ya kuendeleza pale wenzangu walipofika.

Ni kweli chadema tuna misingi, matawi, na kata, hivyo moja ya majukumu yangu makuu ni kuhakikisha chama kinakuwa imara kuanzia ngazi ya chini kabisa,yaani msingi, hii ni pamoja na kuelekea kwenye uchaguzi wa wilaya
Mapambano yanaendelea
 
HONGERA Ubarikiwe mwanangu, sisi wazee hatupendi migogoro, hasa hasa kwenye chama mbadala Chadema. Dumisha amani na mshikamano. PEOPLE'S POWER!
 
Nawashukuru sana kwa pongezi zenu za dhati,natambua matarajio makubwa ya umma unaotamani migogoro ya chadema iishe,kimsingi kikao cha siku mbili kilikuwa cha baraza la mashauriano ya mkoa,kilizungumzia wilaya zote,na hali ya kisiasa kwenye wilaya zote za mkoa wa Arusha zinaendelea kutekeleza maazimio ya chama kama tulivyokubaliana kwenye baraza la 1april,kwa Arusha mjini baraza likagundua matatizo mbalimbali ya kiuongozi,ndipo kamati tendaji ikaridhia kujiuzulu ili kupisha uchaguzi wa watu watakaoweza kukiimarisha chama zaidi,hasa ikizingatiwa hali ya Arusha mjini ilivyo
Nashukuru kuwa viongozi wenzangu wamenipa heshima hii kubwa ya kuendeleza pale wenzangu walipofika.
Ni kweli chadema tuna misingi,matawi,na kata,hivyo moja ya majukumu yangu makuu ni kuhakikisha chama kinakuwa imara kuanzia ngazi ya chini kabisa,yaani msingi,hii ni pamoja na kuelekea kwenye uchaguzi wa wilaya
Mapambano yanaendelea
Hongera Nanyaro

Binafisi nilikuamini toka siku mlipobaki madiwani watatu wa CDM Arusha mliogoma kurubuniwa kwa siasa uchwara, uwe na moyo mkuu weka maslahi ya chama mbele ondoa moyo wa tamaa kama mwenzako Malah aliyegeuka na kuwa Yuda Iskariote kwa kuuza utu kwa vipande 30 vya pesa, pesa kitu gani bwana kama zipo zipo tu hakuna mtu wa kuzizuia, watu wanaoweka tamaa mbele hasa pesa na madaraka mara nyingi kwenye siasa huwa hawafiki mbali.
 
Mimi nafikiri tungebadilisha lugha, badala ya kusema mapambano. Tusema uhamasishaji na uelimishaji wa wananchi. Mapambano limekaa kimgomomgo/kunji/maandamano. We should find a good name on this.

Ningeshauri tupunguze kutumia nguvu kupita kiasi, jazba na hasira badala yake tuelimishe umma kujua haki zake and maove yanayoendelea ili kufanya uamuzi mzuri wa kuwapata viongozi waadilifu wa nchi hii iliyobarikiwa.
 
Nadhani Mungu ameona wanachadema Arusha wanataka kitu ambacho hakijachakachuliwa kwa namna yoyote ile NA HAYO NDIYO MATUNDA YA NIDHAMU YA KWELI NA KUSIKILIZA WANANCHI NA KUTII UONGOZI WA JUU KWA MASILAHI YA TAIFA kaka hongera sana na uendelee kwa uaminifu huo kwa ajili ya masilahi ya Taifa zaidi kuliko matakwa binafsi au chama na kundi la watu wachache
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom