Nani yupo nyuma ya Mary Chitanda?

Gurtu

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,247
342
Arusha imechafuka na kuingia katika historia kwa sababu ya huyu mama. Kila siku tunasikia Mary Chitanda (wengine wanaita Chatanda). Ukisikia uchaguzi wa Meya umekwama Arusha utaambiwa kwa sababu ya Mary Chitanda.

Hivi huyu mama anaweza kuingia kwenye mkutano usiomhusu bila ridhaa ya watu wengine? Hivi anavyojieleza anautoa wapi ujasiri ule wa kifisadi kama siyo kuna mtu nyuma yake? Ukweli ni kwamba yeye ni mbunge wa kuteuliwa kuwakilisha mkoa wa Tanga amealikwa na nani kuhudhuria mkutano wa madiwani Arusha? Hivi angeenda Tanga kuhudhuria mkutano vile vile nani angemzuia na kwa vigezo gani? kwanini aje Arusha na asiende Tanga.

Nafasi aliyonayo Mary Chitanda pale Arusha ni ya kichama na utaratibu wa Chama ni tofauti na ule wa serikali za mitaa ambayo ndiyo inayoratibu shughuli za kanuni na utaratibu katika uwakilishi wa madiwani. Madai ya Mary Chitanda kwamba kila chama kinaamua kuwa mbunge wa vitu maaulum awakilishe eneo fulani ndiyo ulioamua yeye awakilishe mkoa wa Tanga, alikuja Arusha kufanya nini?

Tunaomba uongozi toka ngazi zinazohusika kwani jina la Mary Chitanda linatuumiza masikio. Huyo anayemtumia huyo mama akome kufanya ujinga huo. Watu wanauawa Arusha kwa sababu ya Mary Chitanda halafu wengine wanalaumu Chadema. Huyo mama aogopwe kama ukoma maana kuna shetani nyuma yake.
 
Huyu mama kaingia Arusha kaamua kupandisha bei za ofisi za CCM kwa asilimia 100. Then anajigamba yeye ni diwani wa Arusha ..Jamani

Bila shaka JK au Makamba , Mmojawapo ni chakula yake
 
Arusha imechafuka na kuingia katika historia kwa sababu ya huyu mama. Kila siku tunasikia Mary Chitanda (wengine wanaita Chatanda). Ukisikia uchaguzi wa Meya umekwama Arusha utaambiwa kwa sababu ya Mary Chitanda.

Hivi huyu mama anaweza kuingia kwenye mkutano usiomhusu bila ridhaa ya watu wengine? Hivi anavyojieleza anautoa wapi ujasiri ule wa kifisadi kama siyo kuna mtu nyuma yake? Ukweli ni kwamba yeye ni mbunge wa kuteuliwa kuwakilisha mkoa wa Tanga amealikwa na nani kuhudhuria mkutano wa madiwani Arusha? Hivi angeenda Tanga kuhudhuria mkutano vile vile nani angemzuia na kwa vigezo gani? kwanini aje Arusha na asiende Tanga.

Nafasi aliyonayo Mary Chitanda pale Arusha ni ya kichama na utaratibu wa Chama ni tofauti na ule wa serikali za mitaa ambayo ndiyo inayoratibu shughuli za kanuni na utaratibu katika uwakilishi wa madiwani. Madai ya Mary Chitanda kwamba kila chama kinaamua kuwa mbunge wa vitu maaulum awakilishe eneo fulani ndiyo ulioamua yeye awakilishe mkoa wa Tanga, alikuja Arusha kufanya nini?

Tunaomba uongozi toka ngazi zinazohusika kwani jina la Mary Chitanda linatuumiza masikio. Huyo anayemtumia huyo mama akome kufanya ujinga huo. Watu wanauawa Arusha kwa sababu ya Mary Chitanda halafu wengine wanalaumu Chadema. Huyo mama aogopwe kama ukoma maana kuna shetani nyuma yake.

Ushauri binafsi kwa huyu Mary Chitanda:
Kwa kuwa kabla ya kuteuliwa Mbunge alikuwa Katibu wa CCM Arusha na hivyo makazi yake kuwa Arusha, na kwa kuwa sasa hivi ameteuliwa kuwa Mbunge wa kuwakilisha Mkoa wa Tanga, na kwa kuwa pamoja na uongozi wa juu wa CCM kufahamu kuwa anawakilisha mkoa wa Tanga na wakaendelea kumwacha kama Katibu wa CCM Arusha namshauri aidha aombe uhamisho ili akahudumu mkoa wa Tanga kama Katibu wa CCM na hivyo aweze kuwawakilisha vyema kina mama waliomchagua.

Endapo ombi la uhamisho litashindikana basi aachie kazi ya Katibu wa Chama mkoa wa Arusha na kubaki na kofia moja ya Mbunge wa Kuwawakilisha kina mama wa Tanga. Kwa sasa hivi yeye kama Mbunge mambo yanayofanyika Arusha kwa mkono wake yanambomoa kisiasa na sidhani kama 2015 atakuwa na ujasiri wowote wa kutafuta ubunge wa jimbo lolote Tanga kwani tayari anaonekana mbele ya jamii kama amewatumia wamama wa Tanga kama ngazi tuu ya kupanda kisiasa na wala hana nia thabiti ya kuwatumikia wakazi wa Tanga
 
Naomba kwa wale wanaofahamu sheria wanipe tafsiri ya sheria ya serikali ya mitaa, Je inamuruhusu Mbunge wa viti maalum kutoka Mkoa fulani kuwakilisha wananchi wa mkoa mwingine???. Kwa kiswahili rahisi Mbunge wa viti maalum Dar es salaam anaweza kuwasilisha Jimbo au wilaya moja kati ya hizi Kinondoni, Ilala au Temeke!!! kwa kweli mie sijui kama Mbunge wa viti maalum kutoka Kigoma anaweza kuwakilisha wananchi wa Mkoa wa Shinyanga! Sijui hiyo sheria inasemaje kwa hapo na kama inaruhusu hivyo then Mary Chitanda kutoka Tanga na kuwakilisha wa watu wa Arusha mjini! Kwangu ingesound vizuri zaidi kama Merry Chitanda angekuwa anatoka sehemu mojawapo ya wilaya za Arusha na ingefaa kuwawakilisha watu hao, tofauti na hapo hoja hiyo inaleta utata mtupu!!!!.

Pia watu wangekuwa wepesi wa kusoma alama za Nyakati, Mabadiliko yatakuja tu na wala huwezi kuyazuia! wananchi wa leo hawatawaliwi na Mabavu bali hutawaliwa na Busara au Hekima za viongozi wanaowaongoza.
 
anavyoonekana hajui anafanya nini na kuna uwezekano mkubwa kuwa kaliwa na wote maana akili zake ni za kuvukia bara bara 2
 
wakuu,

Nimefafanua kwenye thread nyingine. Hakuna mbunge viti maalum anayewakilisha mkoa. nafasi kama hiyo haipo kikatiba wala NEC haina wabunge wa namna hiyo.

Kuchaguliwa kupitia mkoa ni utaratibu ndani ya CCM. Kama ambavyo CHADEMA walitumia vigezo vya elimu na ushiriki kwenye chama, CCM wanatumia makundi mbalimbali likiwemo hilo la mikoa, NGO, walemavu, vyuo vikuu nk.

Ikiisha uchaguzi ndani ya CCM hao wote wanapelekwa NEC majina yao na namba walizopewa hakuna cha kwamba huyu kapitia mkoa au NGO au vyuo vikuu.

Wakiteuliwa na NEC wanaitwa wabunge viti maalum CHADEMA au CCM au CUF.

Hilo la kwamba yeye ni mbunge wa viti maalum Tanga ni confusion ambayo imekuja kwasababu tu ndani ya CCM aligombea kundi la mkoa.

Kikawaida ungetegemea halmashauri akashiriki Tanga kwasababu angelikuwa anaishi huko au ana interests zaidi huko. Lakini huyu mama anafanya kazi Arusha, alikuwa anaishi Arusha hata kabla ya uchaguzi. Kweli mnaona ina make sense awe anasafiri kila wiki km zote hizo kwenda Tanga kuhudhuria vikao wakati kisheria anaruhusiwa popote?

Kama kuna wabunge viti maalum wanaowakilisha mkoa, nijulishe upande wa CHADEMA ni akina nani hao?

Hii sheria CHADEMA wenyewe wameitumia kule Hai sasa nashangaa kwanini wanaona hili suala la huyu mama ni tofauti?

Hii sheria ilitungwa wakati hakuna upinzani lakini kwa jinsi upinzani ulivyo sasa itabidi irekebishwe au iongezewe definition.
 
wakuu,

Nimefafanua kwenye thread nyingine. Hakuna mbunge viti maalum anayewakilisha mkoa. nafasi kama hiyo haipo kikatiba wala NEC haina wabunge wa namna hiyo.

Kuchaguliwa kupitia mkoa ni utaratibu ndani ya CCM. Kama ambavyo CHADEMA walitumia vigezo vya elimu na ushiriki kwenye chama, CCM wanatumia makundi mbalimbali likiwemo hilo la mikoa, NGO, walemavu, vyuo vikuu nk.

Ikiisha uchaguzi ndani ya CCM hao wote wanapelekwa NEC majina yao na namba walizopewa hakuna cha kwamba huyu kapitia mkoa au NGO au vyuo vikuu.

Wakiteuliwa na NEC wanaitwa wabunge viti maalum CHADEMA au CCM au CUF.

Hilo la kwamba yeye ni mbunge wa viti maalum Tanga ni confusion ambayo imekuja kwasababu tu ndani ya CCM aligombea kundi la mkoa.

Kikawaida ungetegemea halmashauri akashiriki Tanga kwasababu angelikuwa anaishi huko au ana interests zaidi huko. Lakini huyu mama anafanya kazi Arusha, alikuwa anaishi Arusha hata kabla ya uchaguzi. Kweli mnaona ina make sense awe anasafiri kila wiki km zote hizo kwenda Tanga kuhudhuria vikao wakati kisheria anaruhusiwa popote?

Kama kuna wabunge viti maalum wanaowakilisha mkoa, nijulishe upande wa CHADEMA ni akina nani hao?

Hii sheria CHADEMA wenyewe wameitumia kule Hai sasa nashangaa kwanini wanaona hili suala la huyu mama ni tofauti?

Una maana kuwa Mbunge yeyote awajibiki kwa lile kundi lilomchagua? Mfano Mbunge aliyechaguliwa na kinamama wa Kilimanjaro hawajibiki kupigania maendeleo ya kina mama Kilimanjaro? au Mbunge anawakilisha say Vyuo Vikuu hawajibiki kupigania maslahi ya vyuo vikuu?.

Kama jibu lako ni "NDIYO" then hakuna haja ya kuwa na wabunge wa aina hii kwani wako kwa maslahi yao binafsi - mishahara na posho za vikao mbalimbali
 
Mnalikuza tu jina la huyu mama. Yupo aliesimamia uchaguzi wa Meya wa Arusha ambaye ni Mkurugenzi wa jiji hilo. Yeye anawajibika kwa WN OWM TAMISEMI.
 
Ok,mwenyekiti,makamu mwenyekiti wa chama na katibu mkuu ndo waliopo nyuma yake...........mmmmhh,so what?whats the way forward?
Kwanini mnapata shida sana na huyu mama badala ya hao cowards walioko nyuma yake???Makamba vipi???Huyo mama anawajibika kwake...........
 
hivi huko tanga hakukuwa na wabeijing wa kuteua mpaka wamchukue mamluki huyo wa arusha?nafasi ya wanatanga ipo wapi..nadhani ni kupeana ulaji tu..utaratibu mboooovu huu
 
Una maana kuwa Mbunge yeyote awajibiki kwa lile kundi lilomchagua? Mfano Mbunge aliyechaguliwa na kinamama wa Kilimanjaro hawajibiki kupigania maendeleo ya kina mama Kilimanjaro? au Mbunge anawakilisha say Vyuo Vikuu hawajibiki kupigania maslahi ya vyuo vikuu?.

Kama jibu lako ni "NDIYO" then hakuna haja ya kuwa na wabunge wa aina hii kwani wako kwa maslahi yao binafsi - mishahara na posho za vikao mbalimbali

Mkuu,

Sijasema huyo mama hawajibiki kwa hao waliompa nafasi. In fact inabidi awajibike kwa wanawake wote.

Nikuulize swali kama lako, kwasababu wabunge wa viti maalum wa CHADEMA walichaguliwa kwa vigezo vilivyotayarishwa na Kitila, wanawajibika kwa Kitila? Au kwasababu walichaguliwa kwa vigezo vya elimu, wanawajibika kwenye elimu zao? Kwa maana yako kwasababu wabunge wa CHADEMA hawakuchaguliwa na wanawake wenzao, basi hawawakilishi wanawake wenzao?

Hawa wabunge wote wanaongozwa na sheria ile ile moja. Hawajali wamepata uteuzi kwa njia ipi, wakiteuliwa na NEC wanakuwa na sifa sawa kama wabunge viti maalum. Kwenye majina yao hakuna cha mkoa au jimbo au kundi. Unaweza kwenda hata website ya bunge ukaangalia.

Hata katiba ya CCM ambayo ndio imepanga kundi la mkoa. Kwenye vikao vyao hakuna wabunge wa viti maalum wa mikoa. Wanatumia wabunge wa viti maalum wanaoishi kwenye mkoa au wilaya husika.
 
Mkuu,

Sijasema huyo mama hawajibiki kwa hao waliompa nafasi. In fact inabidi awajibike kwa wanawake wote.

Nikuulize swali kama lako, kwasababu wabunge wa viti maalum wa CHADEMA walichaguliwa kwa vigezo vilivyotayarishwa na Kitila, wanawajibika kwa Kitila? Au kwasababu walichaguliwa kwa vigezo vya elimu, wanawajibika kwenye elimu zao? Kwa maana yako kwasababu wabunge wa CHADEMA hawakuchaguliwa na wanawake wenzao, basi hawawakilishi wanawake wenzao?

Hawa wabunge wote wanaongozwa na sheria ile ile moja. Hawajali wamepata uteuzi kwa njia ipi, wakiteuliwa na NEC wanakuwa na sifa sawa kama wabunge viti maalum. Kwenye majina yao hakuna cha mkoa au jimbo au kundi. Unaweza kwenda hata website ya bunge ukaangalia.

Hata katiba ya CCM ambayo ndio imepanga kundi la mkoa. Kwenye vikao vyao hakuna wabunge wa viti maalum wa mikoa. Wanatumia wabunge wa viti maalum wanaoishi kwenye mkoa au wilaya husika.

Nilitaka jibu tuu na wala haina maana niko upande mwingine wa sarafu. Hoja yangu ilikuwa hakuna haja ya kuwakusanya watu wamchague mtu ambaye hatakuwa na impact yeyote kwa maendeleo ya waliomchagua.
 
Huyu mama kwa taarifa kazaa na JK lkn mkamba alikuwa anapata tigo miaka ya nyuma ndio maana leo hii anaenda kugombea ubunge tanga,kwani anayoyafanya ni kichefuchefu
 
Naona hapa viongozi wa juu bado wake uzingizini. Mji wa Arusha ni kitovu cha utalii nchi, eneo hili linalingizia Taifa fedha nyingi kupitia utalii. Pia kitovu cha Afrika. Vyote hivi vingewasukuma viongozi wetu kuona umuhimu wa kushughulikia migogoro kabla mambo kuharibika. Kama hivi sasa. Huyu ametumwa na makamba kuisambaratisha SiSiEmu.
 
Nilitaka jibu tuu na wala haina maana niko upande mwingine wa sarafu. Hoja yangu ilikuwa hakuna haja ya kuwakusanya watu wamchague mtu ambaye hatakuwa na impact yeyote kwa maendeleo ya waliomchagua.

Sawa mkuu. Hilo la impact sijui maana anaweza akawa anawasaidia hao wanawake kwa njia zingine. Namfahamu mama mmoja viti maalum CCM kutoka mkoa wa Ruvuma, anasaidia NGO za wanawake karibu mikoa yote ya kusini mpaka Mbeya.

Chatanda akiwatelekeza waliompa kura atawajibishwa nao 2015. Huwezi kujua, labda 2015 atagombea kupitia mkoa wa Arusha au kupitia makundi mengine?

Si umeona mama Mlaki kakimbia kwenye jimbo la Kawe na akaamua kugombea kupitia NGO.

Nafikiri utaratibu mzuri ni kwa hawa viti maalum wasiwe wajumbe wa baraza la madiwani. Madiwani wabaki kuwa madiwani wa kuchaguliwa, madiwani wa kuteuliwa na mbunge wa jimbo.

Tatizo la Tanzania ni kukosekana watu wengi ambao wanaielewa katiba yetu vizuri ili kusaidia kuelemisha umma. Watu wametumia wiki kadhaa kubishana jambo ambalo ofisi ya mwanasheria mkuu au katibu ya bunge inaweza kulitolea ufafanuzi kwa urahisi sana. Vinginevyo mahakama ingeliweza kutolea ufafanuzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom