Nani Ndani Ya TRA Ananufaika na Kampuni Ya Yono Mart

Nani Ndani Ya TRA Ananufaika na Kampuni Ya Yono Mart

Hawa madalali watu wabaya sana..ukikaona kale kamama kanavyosema utafikiria kuna haki. Matunguli yana mwisho wake. Amuulize Majembe. Wasione raha kusumbua watu wasio na hatia.
Kwa umri niliyonayo kampuni yeyote inayojihusisha kupiga minada mali za watu hatimaye huwa zinafilisika. Iko wapi Majembe Auction Mart.
 
Yono ni madalali yaliyopewa kazi hadi ndani ya ccm. Inawaharass wapangaji wa ccm kisa 10% Kwa hiyo ina kibali cha ccm kabisa na TRA si ya ccm.? Nashauri kususia minada yao, ni ya dhuluma!!!!
 
Ungemjua mume wangu.. husingefikiria hata kidunchu kumwandika.

Lingine punguza wivu kwa unayemfikiria maana eeeeeh naona bado anawamaliza na yake mazuri sana katika uongozi wake.
Kwa jinsi ulivyo mpumbavu, sipati picha mumeo atakuwa wa aina gani..
Dizaini ni kama ya wezi wa vyeti vya taaluma vile.
 
Cha msingi ni kuisusia minada yao..ili wakise 10% inayowafanya kuwa na haraka na tamaa ya kuuza mali za watu hovyo...
 
Umenena vyema, TRA iwe kitengo cha serikali, waliostaarabika na kujua nini maana ya kudaiwa


kwa nini wanaodaiwa hawapewi fursa ya kulipa deni? hata kwa kusaidiwa mawazo na kuondolewa kodi n.k; au kuwa chini ya uangalizi wa jopo fulani...kama wanavyofanya kwa mabenki

mtu anaposhindwa kulipa kodi akafungiwa, kinaangaliwa kodi tu! hawaangalii ajira na faida zingine zinazopotea

lengo iwe kupata hela hata kama itachukua miaka 5!

kuuza kitu cha 20bn ukauza kwa 2bn, ni ujinga na ufisadi mpya
 
Ni upumbavu mkubwa sn Duniani Mkusanya kodi kuwa na Dalali!!!

Loan Board (HESLB) walikuwa na madalali wa kukusanya Mikopo nchi nzima. JPM akapiga marufuku.

Iweje hii YONO yenyewe iendelee tena ikifanya kazi za TRA? Upuuzi mkubwa sn kuwahi kutokea.
 
Halafu kisheria inakaa VIP kampuni ya yono kuwa na nguvu kuliko TRA, ukiangalia wafanyakazi wao hawana ethics wao ni nguvu nguvu tu mabavu mabavu tu ingia ndani toa vitu vya watu kinguvu nguvu tu wao ndo uita press conference wanazungumza watakavo,tungeeleweshwa wao wapo kisheria kama nani ili kutuondolea mikanganyiko.
 
Vitu vya mnada huwa si vizuri kiimani sababu unadhulumu haki ya MTU aliyosotea wakati ingeweza tumika busara kumpatia mwenye Mali haki yake.
 
siku Tanzania itakapoendelea ni ile siku siasa itaachwa isimame kivyake na serekali isimame kivyake
 
Kamati ya bunge imeamuru NSSF iifahamishe TRA kampuni ya Yono Mart usimamishe mpango wa kuuza nyumba za mradi wake wa Dege Eco Village baada ya mkandarasi wa mradi huo wa ujenzi Mutluhan kutoka nchini Uturuki kudaiwa deni la kodi la bilioni 45.
Hivi inaingia akilini kuuza mradi wa NSSF ulioitia hasara ya bilioni 270 kwa shirika hilo kwa kufidia deni la mkandarasi la bilioni 45.
TRA na Yono Mart pia walishindwa kuuza nyumba za Lugumi baada kuonekana kampuni ya Lugumi inadaiwa bilioni 13 na lakini wanataka kuuza nyumba kwa bei ambayo sio kwa thamani halisi ya nyumba hizo. Serikali itupie macho hii kampuni ya Yono Mart ambayo itailetea hasara kubwa wenye mali (wadaiwa) na TRA katika harakati zake za kupenda kupiga mali mnada kwa haraka kwa maslahi ya kampuni hiyo.
Yono Mart inashughulika na mini? Ipo kampuni moja ya udalali inaitwa Yono Auction Mart sijui ndiyo unayoituhumu ila labda tatizo elimu?
 
Hawa madalali watu wabaya sana..ukikaona kale kamama kanavyosema utafikiria kuna haki. Matunguli yana mwisho wake. Amuulize Majembe. Wasione raha kusumbua watu wasio na hatia.
Madalali, watoza ushuru and the like, wote waliishalaaniwa, hebu rejea vitabu vitakatifu.
 
Hivi inaingia akilini kuuza mradi wa NSSF ulioitia hasara ya bilioni 270 kwa shirika hilo kwa kufidia deni la mkandarasi la bilioni 45.
Kodi ya TRA wa mturuki haihusiana wala kufungamana na NSSF,kama wamepata hasara ya B200 ni wao
TRA na Yono Mart pia walishindwa kuuza nyumba za Lugumi baada kuonekana kampuni ya Lugumi inadaiwa bilioni 13 na lakini wanataka kuuza nyumba kwa bei ambayo sio kwa thamani halisi ya nyumba hizo. Serikali itupie macho hii kampuni ya Yono Mart ambayo itailetea hasara kubwa wenye mali (wadaiwa) na TRA katika harakati zake za kupenda kupiga mali mnada kwa haraka kwa maslahi ya kampuni hiyo.
Sheria za kodi zina mipaka na kanuni zake,huwezi kuacha kuzuia mali ya mdaiwa sugu kisa eti thamani yake ni ndogo,itauzwa mali na mdaiwa ataendelea kudaiwa ikiwemo kufunguliwa jinai
 
Yono Mart inashughulika na mini? Ipo kampuni moja ya udalali inaitwa Yono Auction Mart sijui ndiyo unayoituhumu ila labda tatizo elimu?
Yono Mart inashughulika kuuza mifugo ya kwenu. Halafu kuna Yono Mart inauza mali kupitia TRA hiyo ndio elimu yangu
 
Yono Auction mart ni kampuni ya mwanasisiemu aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Njombe magharibi enzi hizo akiitwa Stanley Kevela Yono.
Wanufaika ni CCm na vitambi vyao.

Kumbe...

Nadhani ni muda muafaka TRA wakawa na kitengo maalum cha kudai madeni na kupiga minada mali za wadaiwa sugu kuliko haya makampuni ya binafsi ya udalali..
TRA bila shaka hili wanaweza sijui kwnn hadi wanakodi makampuni ya udalali ambayo sio mazuri kabisa sbb ni gharama kubwa kuyalipa makampuni haya.. TRA iwe na kitengo kidogo cha kufuatilia madeni ya wadaiwa sugu na kupiga mnada mali zao... Sio kutumia makampuni binafsi which is very expensive to pay them..
 
Kumbe...

Nadhani ni muda muafaka TRA wakawa na kitengo maalum cha kudai madeni na kupiga minada mali za wadaiwa kuliko haya makampuni ya binafsi ya udalali..
TRA bila shaka hili wanaweza sijui kwnn hadi wanakodi makampuni ya udalali ambayo sio mazuri kabisa sbb ni gharama kubwa kuyalipa makampuni haya.. TRA iwe na kitengo kidogo cha kufuatilia madeni ya wadaiwa sugu na kupiga mnada mali zao... Sio kutumia makampuni binafsi which is very expensive to pay them..
TRA tayari wana kitengo cha kudai na kukusanya madeni kinachotuumiza mkuu 10 %.
 
Kwa jinsi ulivyo mpumbavu, sipati picha mumeo atakuwa wa aina gani..
Dizaini ni kama ya wezi wa vyeti vya taaluma vile.

Eeeeeeeh
Kama mkeo yupo hivyo basi usifikiri wote.. pia inaelekea umekua na wanawake walio hivyo. Huoni aibu kujionyesha jinsi unavyoisoma namba hadi meno yanaisha kwa kusagiga... maneno machafu inaonyesha umejaa uchafu..
 
Back
Top Bottom