Hi nyie wenzetu uelewa wenu hua ukoje!? Magazeti yanayoshabikia ccm yapo mengi, Raiamwema, raia Tanzania, Dira nk. Mleta huja si kwamba hajayaona hayo, ameyaona but hayo ni magazeti ya watu. Hata Uhuru likifanya hivyo hakuna atakae uliza cause ni gazeti la ccm lakini sio Habari leo, Daily news na Sunday news, hata TBC haipaswi kufanya hayo inayoyafanya kwasababu hivi ni vyombo vya umma; unataka kunambia we hulioni hilo!? Mwanahalisi linamilikiwa na Sead Kubenea, mgombea ubunge kwa Chadema pale Ubungo, Tanzania daima linamilikiwa na familia ya Mbowe ambaye ndiye mwenyekiti wa Chadema, ulitegemea iwaje!? Ndio maana UKAWA wanasema kipaumbele chao cha kwanza ni Elimu, uelewa wa kupambanua mambo wa Watanzania wengi uko chini sana.
Jana nimerudi toka kazini napata habari kwamba jirani yangu ananitambia kwamba atanizomea sana UKAWA ikishindwa uchaguzi (hua tunatanian anae sana tu) nikamwambia mimi hata nikiumwa ugonjwa wowote pamoja na familia yangu hua hatutibiwi na hospitali za serikali, mwajiri wangu anachukua jukumu hilo, na wewe je!? Ukweli watu wengi wanadhani kushabikia vyama hivi kwenye hu uchaguzi ni kama kushabikia YANGA na SIMBA, yote hi ni kwasababu ya ELIMU. Unaweza kusona but namna yako ya kupambanua mambo ikawa chini sana. Sorry kwa maneno yangu mengi, nasikia kugadhabika kwasababu mtu mwenye uwezo wa kutumia internet naye hajui kutofautisha magazeti ya serikali na magazeti ya watu binafsi.