Nani kawaroga watanzania kwamba Demokrasia ni uadui?

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Najaribu kujiuliza kama sio utapiamlo wa uelewa kumbe ni kitu gani hiki? Mbona kinachoendelea kwenye siasa zetu ni uadui ule wa weusi na makaburu enzi zile za Afrika ya kusini?

Kwani ACT wakishinda Zanzibar watanzania watafutwa kwenye kitabu cha uzima? Au CHADEMA wakishinda bara ardhi yetu itapoteza rutuba? Madini yetu yatayeyuka yasionekane? Mlima Kilimanjaro utahamia Kenya. Au mbuga zetu za wanyama zitaibukia Uchina?

Hivi kwa mfano CCM wao wakishindwa hawatakuwa ni mawazo mbadala yapendwayo na watanzania dhidi ya serikali itakayokuwepo madarakani? Hivi kweli tumeshindwa kuelewa lengo la demokrasia ya vyama vingi?

Kwani nani kawadanganya CCM kwamba watatawala nchi hii milele? Au nani kawaongopea wapinzani kwamba wakiingia madarakani hawatatolewa siku wakiboronga?

Kwanza ikitokea Upinzani umeshinda na kutawala, mimi nitahamia CCM watakaokuwa wapinzani.

Kwangu mimi Demokrasia ni upambanishi wa hoja na si mapambano ya watu. Ukiona chama cha siasa kinachukia hoja na kurukia viroja ujue hicho ni kitu kingine.

Hivi ingelikuwa demokrasia ni vita kama wadhaniavyo wengine; sidhani kama mwalimu Nyerere angewaachia wajukuu zake hicho kitu.

Ujue mpaka sasa tayari tumeshapanda mbegu za chuki, ubaguzi, na magomvi. Ndiyo maana ukiwaangalia watu wamekaa mkao wa kusubiria mavuno yake!

Ndugu waTz kama siasa zenyewe ni hizi za kuchukiana mpaka kuuana kuna haja gani ya kuendelea nazo?

Hivi kweli sisi kama taifa tumeshindwa kustaarabika kiasi tufanye siasa za kistaarabu.

Mpaka lini tutaendelea kugombania utawala kama manyani yanavyogombania na wenzao huko maporini?

Hapana, nadhani hii njia tunayopitishwa siyo nzuri kwa mustakabari wa Taifa hili.
Hivi nani alituroga kiasi cha kujali vyama vyetu kuliko taifa letu. Hadi tunaona ni aheri taifa zima lisambaratike kuliko chama chetu kishindwe kwenye uchaguzi.

Ee mama Tanzania, nani atakayekuhurumia, akuponye na maradhi yanayokukabiri?
 
Mkuu umeandika Jambo la msingi Sana ,binafsi sijawai kua na kadi ya chama chochote,ila Nina marafiki wengi wa wenye mlengo wa vyama tofauti ikiwemo CHADEMA na CCM hua tunakaa tukajadili ,tunafurahi,japo changamoto ninayopata ni ushawishi wao kujiunga kwenye vyama vyao,Mimi ni mpigaji kura mzuri tu,ila hua naangalia sera za chama husika basi siendagi kwa mkumbo hata siku moja
 
Mkuu, ujue mimi hivi vyama navichukulia kama fimbo ya kumrekebishia mtoto.
Sasa shida ni pale tunapoifanya fimbo iwe muhimu kuliko mtoto mwenyewe!
Mkuu umeandika Jambo la msingi Sana ,binafsi sijawai kua na kadi ya chama chochote,ila Nina marafiki wengi wa wenye mlengo wa vyama tofauti ikiwemo chadema na ccm hua tunakaa tukajadili ,tunafurahi,japo changamoto ninayopata ni ushawishi wao kujiunga kwenye vyama vyao,Mimi ni mpigaji kura mzuri tu,ila hua naangalia sera za chama husika basi siendagi kwa mkumbo hata siku moja
 
Ninachokiona tatizo kubwa ni CCM ambao wao wanaamini Tanzania ni mali yao na wengine wanachukuliwa kama raia wa nchi jirani.

Ukiangali CCM namna wanavyowatreat wapinzani wanawachukulia kama maadui zao.


Sent from my A37f using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, hata wakiokuwa upinzani wakatoka huwa wako hivyohivyoSasa sijui ni uelewa au vipi.
Wewe jamaa.
, inawezekana Vyama vya Siasa bora viko vingi. Maana kuna watu wangetembea uchi kwasababu hawaelewi,

Utawala wa chama kimoja ulikua ni ku Order tu;

1. Atembee uchi

2. Fukuza kazi

3. Chana nguo

4. Lazima anipende mimi sio yule

5. Hatakiwi kuoa/kuolewa

6. Afikirishwe ujamaa peke yake

7. Hafikiri tena

8. Tunataka moyo

9.Tunataka ini

10. Error Team


Watu wanatekeleza kwasababu ni raha kuwa karibu na kiongozi
 
Najaribu kujiuliza kama sio utapiamlo wa uelewa kumbe ni kitu gani hiki? Mbona kinachoendelea kwenye siasa zetu ni uadui ule wa weusi na makaburu enzi zile za Afrika ya kusini?

Kwani ACT wakishinda Zanzibar watanzania watafutwa kwenye kitabu cha uzima? Au Chadema wakishinda bara ardhi yetu itapoteza rutuba? Madini yetu yatayeyuka yasionekane? Mlima Kilimanjaro utahamia Kenya. Au mbuga zetu za wanyama zitaibukia Uchina?

Hivi kwa mfano CCM wao wakishindwa hawatakuwa ni mawazo mbadala yapendwayo na watanzania dhidi ya serikali itakayokuwepo madarakani? Hivi kweli tumeshindwa kuelewa lengo la demokrasia ya vyama vingi?

Kwani nani kawadanganya CCM kwamba watatawala nchi hii milele? Au nani kawaongopea wapinzani kwamba wakiingia madarakani hawatatolewa siku wakiboronga?

Kwanza ikitokea Upinzani umeshinda na kutawala, mimi nitahamia CCM watakaokuwa wapinzani.

Kwangu mimi demokrasia ni upambanishi wa hoja na si mapambano ya watu. Ukiona chama cha siasa kinachukia hoja na kurukia viroja ujue hicho ni kitu kingine.

Hivi ingelikuwa demokrasia ni vita kama wadhaniavyo wengine; sidhani kama mwalimu Nyerere angewaachia wajukuu zake hicho kitu.

Ujue mpaka sasa tayari tumeshapanda mbegu za chuki, ubaguzi, na magomvi. Ndiyo maana ukiwaangalia watu wamekaa mkao wa kusubiria mavuno yake!

Ndugu watz kama siasa zenyewe ni hizi za kuchukiana mpaka kuuana kuna haja gani ya kuendelea nazo?

Hivi kweli sisi kama taifa tumeshindwa kustaarabika kiasi tufanye siasa za kistaarabu.

Mpaka lini tutaendelea kugombania utawala kama manyani yanavyogombania na wenzao huko maporini?

Hapana, nadhani hii njia tunayopitishwa siyo nzuri kwa mustakabari wa Taifa hili.
Hivi nani alituroga kiasi cha kujari vyama vyetu kuliko taifa letu. Hadi tunaona ni aheri taifa zima lisambaratike kuliko chama chetu kishindwe kwenye uchaguzi.

Ee mama Tanzania, nani atakayekuhurumia, akuponye na maradhi yanayokukabiri?
Hao hao unaowapigia chapuo ndiyo wanaopandikiza hiyo chuki...

Usidhani Watanzania hatuna akili. Tunaukataa ushetani kwa nguvu zote.
 
Kama wanaipandikiza wao, nani aliyeihifadhi mbegu hiyo akawapatia waipande?
Hao hao unaowapigia chapuo ndiyo wanaopandikiza hiyo chuki...

Usidhani Watanzania hatuna akili. Tunaukataa ushetani kwa nguvu zote
 
kwa matusi ya huyu Binti wa cdm, nadhan zile kesi zake ni za kuskilzia haraka sana! laiti kama tungepata chama chenye sera ya kushawishi umma, uchaguzi huu ungenoga sana
 
Back
Top Bottom