Nani atalikomboa taifa la Tanzania?

Aman Ng'oma

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
954
510
Watanzania wengi tumekaa zaidi kishabiki,mambo ya msingi tunayaacha,wanasiasa wanaiharibu nchi yetu tunashindwa kuwakemea, tunawatazama tu na tunapojaribu kufanya hivyo,hatufanyi kwa dhati,zaidi kinachoonekana ni ushabiki ambao kimsingi hauna tija kwa taifa letu.Wanasiasa wanatutumia kama ngazi kwa ajili kuwanufaisha wao na familia zao,wanashindwa kutuletea maendeleo ya ukweli yatakayomfanya kila mtanzania afurahi kuishi na kuwa mtanzania.Lakini ajabu wanasiasa wanajipendelea wao tu huku watanzania wakibaki masikini wa kutupwa hoehae.Viongozi wetu hawana huruma hata kidogo,kiongozi anakubali alipwe 7,000,000 kwa mwezi ilihali kuna mfanyakazi mwingine analipwa 150,000.Jamani mwanasiasa gani Tanzania ni mzalendo tumkabidhi nchi kisha atutoe kwenye huu umasikini?Asiwe mwenye hulka ya kujipendelea,awe na uchungu na Tanzania na watanzania kwa ujumla.
Nawasilisha.
 
hakuna mwanasiasa mzalendo ,mwanasiasa ni mwanasiasa tu!hii nchi iende mikononi mwa jeshi tu.
 
Mtanzania anayefaa ni Bwana William Erio wa PPF.

Huyu anauchungu sana na wanachama wa PPF hivyo atakuwa na uchungu pia na watanganyika pindi tukimpa nchi aiongoze.

Huyu hulipwa kamshahara kadogo tu kama Milioni 12 kwa mwezi, Landcruiser VX V8 na dereva, housing allowance ya shs milioni 4 kwa mwezi. Fuel allowance ya shs. 1.2 milion japo ana fully fueled VX, kila baada ya miaka mitatu hulipwa vijisenti vichache kama Group Endowment shs 540 milioni, gratuity shs 108million na samani za nyumbani tshs 60milion.

Huyu anajitahidi sana kutosafiri sana nje ya nchi, anamzidi kidogo sana Rais wa sasa, 50% ya muda wake wa ajira yuko nje ya nchi na perdiem yake sio kubwa kihivyo, ni analipwa Tshs 1,820,000 (usd 810X1.25X1800) kwa siku kuanzia siku ya kuondoka hadi ya kurudi.

Safari za ndani ya nch analipwa Tshs 500,000 kwa siku hata kama ni Bagamoyo. Ni kiongozi mzuri atakaye tufaa watanganyika.

Uzuri mwingine ni ana gene ya uongozi maana ni mjomba wa Rais mstaafu, Bw. Benjemini William Mkapa, kwa hiyo atatufaa wadanyika

Nawasilisha pendekezo langu.



Watanzania wengi tumekaa zaidi kishabiki,mambo ya msingi tunayaacha,wanasiasa wanaiharibu nchi yetu tunashindwa kuwakemea, tunawatazama tu na tunapojaribu kufanya hivyo,hatufanyi kwa dhati,zaidi kinachoonekana ni ushabiki ambao kimsingi hauna tija kwa taifa letu.Wanasiasa wanatutumia kama ngazi kwa ajili kuwanufaisha wao na familia zao,wanashindwa kutuletea maendeleo ya ukweli yatakayomfanya kila mtanzania afurahi kuishi na kuwa mtanzania.Lakini ajabu wanasiasa wanajipendelea wao tu huku watanzania wakibaki masikini wa kutupwa hoehae.Viongozi wetu hawana huruma hata kidogo,kiongozi anakubali alipwe 7,000,000 kwa mwezi ilihali kuna mfanyakazi mwingine analipwa 150,000.Jamani mwanasiasa gani Tanzania ni mzalendo tumkabidhi nchi kisha atutoe kwenye huu umasikini?Asiwe mwenye hulka ya kujipendelea,awe na uchungu na Tanzania na watanzania kwa ujumla.
Nawasilisha.
 
mtanzania anayefaa ni bwana william erio wa ppf.

Huyu anauchungu sana na wanachama wa ppf hivyo atakuwa na uchungu pia na watanganyika pindi tukimpa nchi aiongoze.

Huyu hulipwa kamshahara kadogo tu kama milioni 12 kwa mwezi, landcruiser vx v8 na dereva, housing allowance ya shs milioni 4 kwa mwezi. Fuel allowance ya shs. 1.2 milion japo ana fully fueled vx, kila baada ya miaka mitatu hulipwa vijisenti vichache kama group endowment shs 540 milioni, gratuity shs 108million na samani za nyumbani tshs 60milion.

Huyu anajitahidi sana kutosafiri sana nje ya nchi, anamzidi kidogo sana rais wa sasa, 50% ya muda wake wa ajira yuko nje ya nchi na perdiem yake sio kubwa kihivyo, ni analipwa tshs 1,820,000 (usd 810x1.25x1800) kwa siku kuanzia siku ya kuondoka hadi ya kurudi.

Safari za ndani ya nch analipwa tshs 500,000 kwa siku hata kama ni bagamoyo. Ni kiongozi mzuri atakaye tufaa watanganyika.

Uzuri mwingine ni ana gene ya uongozi maana ni mjomba wa rais mstaafu, bw. Benjemini william mkapa, kwa hiyo atatufaa wadanyika

nawasilisha pendekezo langu.

yaani hii nchi ni hakika aina mwenyewe. Hivi hata vitu kama hivi tunashindwa kuyadhibiti? Hivi ni kweli kama yanafanyika na yanafumbiwa macho? Nafikiri imefika kipindi hii nchi itawaliwe na dikteta lkn mwenye uzalendo na kujua nini cha kufanya kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.
 
Nguvu ya Umma tuuuuuuuu!!!! Na hakika siku ikifika nawaambia hapatatosha!! Na raia watampa raia mwenye UZALENDO nchi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom