Nani anajali? Hakuna...!

Nikukumbushe

JF-Expert Member
Jun 4, 2013
2,602
408
Kila kukicha mauaji,mlipuko wa mabomu,watu kuumizwa vibaya,umasikini uliokithiri,ufisadi,rushwa,wizi,utoroshwaji wa maliasili kama wanyama hai,udini,ukabila n.k.
Lakini katika haya yote nani anajali si rais,si ccm,si serikali,rais yupo KIMYA kama hasikii vile na haoni vile,yupo na safari zake tu nje ya nchi,akipungiana mkono angani na rais wa chini akiwa na furaha ya kupora raslimali zetu(tanzanite),yeye akiwa na cherehani na net.
Wanapongezana kwa kuua raia ikiwemo kupandishana vyeo(kamuhanda),kuongezeana umri wa kufanya kazi baada ya kuondoka kwa kashfa(kama vile ubalozi) n.k.
Tume zinaundwa kuchunguza matukio haya yote majibu yake hakuna,rais yupo KIMYA. AU NDIYO ILE SLOGANI YA KUWA NI UPEPO UTAPITA?
NASHINDWA NISEME NINI LAKINI RAIS WETU JAMANI UKIMYA HUU HAPANA,MMMMMM! Yaani hata kumwajibisha hata mmoja ili awe mfano rais yuko KIMYA.
LAKINI MWISHO WA YOTE UTAJULIKANA TU,CCM HAMUWEZI KUTAWALA MILELE IPO SIKU MTAKUWA CHAMA CHA UPINZANI: Kwa hiyo uovu wote utaweka hadharani,Hamuwezi kutawala milele hata kidogo NEVER!!
Poleni sana watu wa Arusha-hii ndiyo CCM bwana inayounda serikali SIKIVU hii ni dharau,kejeli na unafiki kwa wananchi.
 
Inasikitisha sana mahali hii nchi yetu Tanzania ilipofikia,naiona AMANI ikichezewa. Mwenyezi Mungu atunusuru na hili janga.
 
Back
Top Bottom