Nani amsaidie Hood

Nani amsaidie Hood

fugees

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2012
Posts
2,868
Reaction score
884
Habarini wanajamvi. Leo nikiwa Morogoro nikiwa nikitafuta usafiri wa kuelekea Mbeya (ili sikukuu hii ikalike huko kwa wanyakyusa) usafiri pekee niliona kama mkombozi wa safari yangu ni Hood.

Mida ya saa mbili usiku naliona busi la Hood hapa Msamvu, mpiga debe mmoja ananiambia bro huo ndio usafiri wa mwisho huwezi pata mwingine otherwise upande IT, nikaona isiwe tabu basi ngoja niwahi siti. Kama wasemavyo waungwana kuwa Mungu si athumani hatimaye nikapata siti na kulipia nauli ya kuelekea Mbeya.

Busi likaondoka Msamvu saa mbili na nusu kuelekea ofisi zao pale mtawala, mara kondakta anasema wajameni tutumie dakika kumi tu kuchimba dawa, basi abiria wengi wakashuka na kufanya hivyo nikiwamo mimi. Baada ya kuingia ndani yaani ofisi za Hood kuchimba dawa naona Hood yule wa miaka ya 2004 - 2007 kachoka sana yaani vyoo vyenyewe ni bora mara tano ya vyoo vya jera Keko au Segerea.

Ingawa sifikii levo za kiuchumi na Hood lakini niliona huruma sana na nikawaza sana namna biashara za watu zinakufa. Ikiwa saa tatu tunaondoka Morogoro kuelekea Mbeya busi hilo la arusha mbeya nikapata taarifa kuwa gari hilo limetoka Arusha saa kumi na mbili na kuingia Moro saa mbili.

Nilishikwa na wasi sana na kuna baadhi ya abiria waasema tutafika Mbeya saa kumi kesho duh nilitahamaki nikasema bora ningepanda IT. Kwa kweli safari imekua ya hofu gari ni bovu sana yaani gali inatembea kama mtu. So ile ndoto yangu ya kuwahi Mbeya saa ikakatika pale na nikawa sina hamu ya kufika muda huo tena.

Ila kikubwa nilichokiona Hood ananafasi kubwa ya kibiashara hususani ya mabasi hapa Morogoro maana kwa jina la Hood bado ni brand kubwa kwenye biashara ya usafirishaji

USAIDIZI

Hood anahitaji muwekezaji mwingine anunue brandi na kufanya biashara yake kwa jina hilo kwa maana brandi bado ipo vizuri. Ikumbukwe wapinzani wa kibiashara katika usafirishaji hapa morogoro ni abood na bm ila ninauhakika kama hoodi angekua na muwekezaji mpya basi hoodi na abood ndio wangekua wachuanaji pekee.

Kimsingi Hood amepotea sana kwenye biashara ya usafirishaji, kwa maana sidhani hata kama anamabasi matatu barabarani.
Hivyo kama wafanyabiashara kama bile Newforce wangeweza nunua au share brand na Hood hapa Morogoro na Tanzania kwa ujumla Hood bado angekua juu katika biashara hii ya usafirishaji.

Ni haya tu wadau.
 
mtu unapanda hood mpaka leo??? tena kwenda mbeya.... bora kilimanjaro hapo sawa japo yamechokaa balaa
 
mtu unapanda hood mpaka leo??? tena kwenda mbeya.... bora kilimanjaro hapo sawa japo yamechokaa balaa
Hizi gari sijui Hood alizipata wapi, na ni kama amefunga nazo mkataba wa kufa na kuzikana. Wenzake kadir muda unavyoenda huuza mabasi chakavu moja moja na ku replace mapya moja moja, lakin yeye kang'ang'ania tu mikangafu yake miaka nenda miaka rudi.

Bus ziko toka enzi za Plate Number za TZA mpaka leo anazo tu.
 
Habarini wanajamvi. Leo nikiwa morogoro nikiwa nikitafuta usafiri wa kuelekea mbeya (ili sikukuu hii ikalike huko kwa wanyakyusa) usafiri pekee niliona kama mkombozi wa safari yangu ni Hood.

Mida ya saa mbili usiku naliona bus la hood hapa msamvu, mpiga debe mmoja ananiambia bro huo ndio usafiri wa meisho huwezi pata mwingine otherwise upande IT, nikaona isiwe tabu basi ngoja niwahi siti.

Kama wasemavyo waungwana kuwa Mungu si athumani hatimaye nikapata siti na kulipia nauli ya kuelekea mbeya

Bus likaondoka msamvu saa mbili na nusu kuelekea ofisi zao pale mtawala, mara kondakta anasema wajameni tutumie dakika kumi tu kuchimba dawa, basi abiria wengi wakashuka na kufanya hivyo nikiwamo mimi.

Baada ya kuingia ndani yaani ofisi za hood kuchimba dawa naona hood yule wa miaka ya 2004 - 2007 kachoka sana yaani vyoo vyenyewe ni bora mara tano ya vyoo vya jera keko au segerea.

Ingawa sifikii levo za kiuchumi na hood lakini niliona huruma sana na nikawaza sana namna biashara za watu zinakufa. Ikiwa saa tatu tunaondoka morogoro kuelekea mbeya busi hilo la arusha mbeya nikapata taarifa kuwa gari hilo limetoka arusha saa kumi na mbili na kuingia moro saa mbili.

Nilishikwa na wasi sana na kuna baadhi ya abilia waasema tutafika mbeya saa kumi kesho duh nilitahamaki nikasema bora ningepanda IT.

Kwa kweli safari imekua ya hofu gari ni bovu sana yaani gali inatembea kama mtu. So ile ndoto yangu ya kuwahi mbeya saa ikakatika pale na nikawa sina hamu ya kufika muda huo tena.

Ila kikubwa nilichokiona hood ananafasi kubwa ya kibiashara hususani ya mabasi hapa morogoro maana kwa jina la hood bado ni brand kubwa kwenye biashara ya usafirishaji

USAIDIZI

Hood anahitaji muwekezaji mwingine anunue brandi na kufanya biashara yake kwa jina hilo kwa maana brandi bado ipo vizuri!

Ikumbukwe wapinzani wa kibiashara katika usafirishaji hapa morogoro ni abood na bm ila ninauhakika kama hoodi angekua na muwekezaji mpya basi hoodi na abood ndio wangekua wachuanaji pekee!

Kimsingi hoodi amepotea sana kwenye biashara ya usafirishaji, kwa maana sidhani hata kama anamabasi matatu barabarani.
Hivyo kama wafanyabiashara kama bile newforce wangeweza nunua au share brand na hood hapa morogoro na tanzania kwa ujumla hood bado angekua juu katika biashara hii ya usafirishaji.

Ni haya tu wadau.
Acha tu wajifie hawa, walinipotezea mzigo wangu wa thamani 2014 kizembe sana Hood hawa! Sitaki kabisa kuwasikia kuwa bado wako barabarani maluuni hawa!
 
Ngoja niwarudishe nyuma kidogo kwa wahenga wenzangu.mnazikumbuka bus za SABCO zilikuwa zinakwenda Dar Tunduma Dar Kyela Dar Mbeya moja ilifanya ajari ikamuua mkata viuno maarufu wakati ule SHENAZ walikuwa wakitoka Tunduma kuwahi mechi ya Taifa Stars chini ya Maximo na Blazir.sasa zile SABCO ndio zilikuwa bus za Said Mtoto wa kwanza wa Hood alizaa na mswahili na ndio Mtoto mkubwa na ndie aliyeisimamisha Hood ya wakati ule ikawa ipo juu sana badae Hood Watoto wake walipokuwa wakaanza migogoro Said akajitoa akaanzisha Sabco.nae aliacha biashara ya ma bus amekuwa msimamizi wa Azania niliwahi kufanya biashara ya bus nawafahamu vzr ila Hood hawezi kurudi sababu hawaamini ktk kukopa bank
 
Hizi gari sijui Hood alizipata wapi, na ni kama amefunga nazo mkataba wa kufa na kuzikana. Wenzake kadir muda unavyoenda huuza mabasi chakavu moja moja na ku replace mapya moja moja, lakin yeye kang'ang'ania tu mikangafu yake miaka nenda miaka rudi.

Bus ziko toka enzi za Plate Number za TZA mpaka leo anazo tu.
Nadhani anakula tu faidaa badala ya kuwekezaa...!! Hood kachoka sana sijui why Root ya Mbeya Kilimanjaro ni yeye tu anatawalaa...
 
Kikubwa kuhusu kutembea Hood munamuonea, nchi nzima sheria ni 80 kwa 50 kwa sasa!

Hood anatakiwa akalale Makambako ajabu kuna siku askari wa Mafinga bila sababu wakaamua kulizuia Mafinga likalala hapo. So kwa upande mwingine Hood anadhibitiwa, wamwache uone Mbeya anavyotoboza saa moja usiku!!

Kiukweli magari kwa sasa pia yamechoka!! Ofisi zimechoka, wafanyakazi wamechoka!! Sheria za sasa na zimemchosha!!

Watu wa karibu wajaribu kuongea nae penbine anahitaji ushauri lakini haina maana hakopesheki! Au ameamua kuua biashara ya basi kwa sasa
 
Hizi gari sijui Hood alizipata wapi, na ni kama amefunga nazo mkataba wa kufa na kuzikana. Wenzake kadir muda unavyoenda huuza mabasi chakavu moja moja na ku replace mapya moja moja, lakin yeye kang'ang'ania tu mikangafu yake miaka nenda miaka rudi.

Bus ziko toka enzi za Plate Number za TZA mpaka leo anazo tu.
Kuna scania zake Marcopolo Torino,nilizipanda miaka ya 1998-99,naziona hadi leo.Ajabu sana
 
mtu unapanda hood mpaka leo??? tena kwenda mbeya.... bora kilimanjaro hapo sawa japo yamechokaa balaa
Yaan tena mtu katoka arusha anathubutu kupanda hood huo n uwendawazim wa kiwango cha lami wakat kuna gar za kupita dom zinaitafuta mbeya saa nne Au tano tena pamoja na vts hii ya sasa
 
Back
Top Bottom