Sijaelewa mantiki ya kuita kituo cha daladala eti SIMU2000 Kisa pale kulikuwa na coy husika na aliyofisadi mapesa kibao enzi za mkapa.
Unavyoanzisha jina la biashara au sehem linatokana na urahisi wa kutamkwa na watu wa pale, wazawa n.k, leo nilikuwa kwenye NIDA kuchukua national ID idadi ya watu wasio jua kusoma na kuandika ni kubwa sanaaaa....
Hoja yangu kwanini kituo husika wasikite MAWASILIANO kama watu na makonda wengi wanavyokiita wao leo nilikuwa ubungo muda nimewasikia sana baada ya kupata news ya kusitishwa mdahalo nikiwa nimefika, wakiite kama ilivyokuwa makumbusho au wakiite TANESCO majina mepesi kuliko jina hili ambalo alina mvuto eti "simu elfu mbili".
Pia kituo kiko poa sanaaa, ila maingilio yake toka shekilango na mandela road kuna vumbi ya maana.
Nawasilisha.
Ofcoz natural name ya hiko kituo ni Mawasiliano...
vibaka walikuwa wakikwapuo simu kule ubungo stand wanakimbilia kwenye hiko kituo na si unajua tena biashara ya mali ya wizi inapochelewa kununuliwa bei inavyoshuka mishowe simu ikaanza kuuzwa tsh 2000 ili kibaka akapate kete moja ya dawa ya kulevya.hivyo hapo simu ilikuwa ikiuzwa 2000.jibu safi na makini
Sasa nimeona gari wameandika SIMU2000 nikashanga sanaaaa, ata uzinduzi walisema hilo jina.
naona mnadanganyana sasa!Hee kumbe ndo hiko kituo...mi nilikuwa sijui
siku hizi ubungo kuna mataa? :sorry: :laugh::laugh::laugh:!!!Nilipoona daladala imeandikwa simu2000 nikajuwa kuna tatizo, kumbe wana maanisha mawasiliano.
Waandikwe tu mawasiliano hata kwa kifupi.
Pia waambieni kuwa watu tunaotoka na kwenda shamba tunateseka sana na foleni.
Unakaa foleni ambayo haitembei mara mbili;
Iwapo wameamua kupeleka magari ya shamba mawasiliano watutafutie njia ya kutokea na kuingilia bila kuingia tena kwenye foleni ya kwenye mataa ya ubungo.
siku hizi ubungo kuna mataa? :sorry: :laugh::laugh::laugh:!!!
shehe ka pime malariavibaka walikuwa wakikwapuo simu kule ubungo stand wanakimbilia kwenye hiko kituo na si unajua tena biashara ya mali ya wizi inapochelewa kununuliwa bei inavyoshuka mishowe simu ikaanza kuuzwa tsh 2000 ili kibaka akapate kete moja ya dawa ya kulevya.hivyo hapo simu ilikuwa ikiuzwa 2000.jibu safi na makini
naona mnadanganyana sasa!
SIMU 2000 ilikuwa ni kampuni iliyokuwa inahodhi mali za serikali wakati wa ubinafsishaji awamu ya tatu ya ben mkapa, hii kampuni ilimaliza kazi zake mwishoni wa awamu ya tatu na kazi zake nafikiri siku hizi zinafanya na consolidate holding corporation wapo pale mirambo st opposite na ofisi za world bank tanzania ,pia nilisikia CHC muda wake wakufanya kazi ulitakiwa uishe mwaka huu wa fedha,pia kulikuwa na kampuni nyingine zinazofanana na SIMU 2000 kama LART, ATHCO
kwa hiyo kile kituo kipya cha mabasi kilikuwa kinaodhiwa na hiyo kampuni inayoitwa SIMU 2000 Tanzania ltd ndio maana bado panatambulika kama eneo la kampuni tajwaa iliyohodhi eneo hilo
hilo swala la vibaka kuiba simu na kuuza shilingi 2000 wapate pesa ua unga ni uongo mkubwa,
unaweza kupata info za kampuni ya SIMU 2000 kupitia tovuti ya ::CHC Homepage::