MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 793
Wakati unaingia CCM hukufahamu kwamba Sokoine alifariki kipindi cha Nyerere?
Wewe umeingia CCM kwa wrong reasons za kumfuata Nyerere badala ya kufuata sera za Chama na kama unaenda Chadema kumfuata Slaa ndugu yangu na huko ujue utatoka soon.
Samahani sana kama ntakuhudhi, haya ni maoni yangu toka moyoni na sikushawishiwa na mtu yoyote:
Nikili kwamba mimi ni Mwanachama hai wa CCM na si utani. Chama nilikipenda toka moyoni, Ila kwa kwa sasa nabwaga manyanga Rasmi mimi si mwanachama tena wa CCM. Nilijiunga na CCM Mwaka 1999 nikiwa Form 4 hapo jijini DSM tena kwa Moyo mmoja kwa kadi No.1267...., tena kutokana na Mapenzi yangu ya dhati kwa Mwl. JK NYERERE. Na alipokufa nilisikitika sana tena sana, nakumbuka kipindi hicho nilikuwa najiandaa na Mitiana ya Form 4 na tena nilikuwa naumwa typhod kali sana na kidogo iniue! Ila nilijikongoja toka kitandani mpaka pale maeneo ya sanyansi enzi hizo pakijulikana Maji machafu kushuudia mwili wa mwalimu JK NYERERE ukipitishwa hapo. Kiukweli nililia sana na nkazidiwa na kukimbizwa hospital baada ya kuzidiwa ghafla na jua kali lililokuwa limenichapa. Nashukuru mungu aliniepusha na kifo.
SABABU ZA KUTOKA CCM:
1. Jana nimepata tena mshutuko wa ajabu baada ya kusikia kuwa chama changu (CCM) kilihusika katika kifo cha Mshawishi wangu wa kujiunga na CCM (JK NYERERE), kweli nimeumia sana.
2. Hii imepelekea nianze kuanimi maneno ya wapinzani kuwa CCM ni chama cha wauaji, achilia mbalil maswala ya UFISADI, maana Tanzania bila ufisadi haiwezekani, ndo maana kila mtu ni fisadi katika ofisi yake, na hakuna anayeweza kulipinga, maana bila ufisadi hakuna hata mmoja nayeweza kujenga kwa kutumia mishahara yetu. Nisingependa kuegemea katika swala la ufisadi.
3. Hii imenipele niamini kuwa chanzo cha vifo vya watu mbali mbali ndani ya CCM ni Mkono wa CCM wenyewe! Ntatoa mifano Hai:-
(a) Kifo cha Kigoma Malima, Utata Mtupu mpaka leo..........Mhusika ni CCM
(a) Kifo cha Kombe, Utata Mtupu mpaka leo......................Mhusika ni CCM
(b) Kifo cha Sokoine, Utata mtupu mpaka leo....................Mhusika ni CCM
(c) Kifo cha Daudi Balal, Utata Mtupi mpaka leo...................Mhusika ni CCM
(d) Kifo cha Halima Chifupa Utata mtupu mpaka leo............Mhusika ni CCM
(e) Kifo cha JK NYERERE nacho leo wanasema ...................Mhusika ni CCM
Na sasa kuna mameno mengine juu ya ugonjwa wa Dr. Mwakyembe na Prof Mwandosya kuwa chanzo ni CCM, Jamani kwanini niendelee kuwa mwanachama wa chama hiki? Tafadhali wana CCM Mliokuwa wenzangu nipeni ushawishi wa kutosha wa kwanini nibaki katika hiki chama na Wapinzani nipeni sela zenye mashiko ya kujiunga na chama chenu la sivyo nakaa bila kuwa mwanachama wa chama chochote katika maisha yangu yote kuanzia leo.
"NIMEUMIA SANA NA HABARI HII YA MKAPA KUHUSIKA KATIKA KIFO CHA JK.NYERERE NA IMENITOA RASMI CCM"
"MUNGU MLAZE PEMA MWL. JK NYERERE NA TUNAMPENDA SANA, WOTE WALIOHUSIKA WATAHUKUMIWA HAPA HAPA DUNIANI NA UMPE NGUVU MAMA MARIA NYERERE NA FAMILIA YAKE ASIDANGANYIKE KUUKANA HUU UKWELI MAANA WATAMWANDAMA SANA KUPITIA TBC ILI AYAKANE NA KUMKANA V. NYERERE KUWA SI MWANA FAMILA NA AMEKURUPUKA"
MyTake: Changia bila kutukana.
Huyu jamaa ni mzima wa afya njema, hajafa. Kwasababu zifuatazo:-Kaka tulitangaziwa na chama na serikali yetu kuw jamaa amekufa, hapo tumwamini nani?
Samahani sana kama ntakuhudhi, haya ni maoni yangu toka moyoni na sikushawishiwa na mtu yoyote:
MyTake: Changia bila kutukana.
Mnapoleta tuhuma nzito kama hizi ambatisheni na ushahidi. Sasa ukiniambia Nyerere aliuawa na Mkapa bila evidence nitatofautishaje maneno yako na yale ya walevi? Maana walevi wanaweza kusema lolote lililo akilini mwao na kuliapia bila hata kulijua ukweli wake. Na wewe ni kama hao? Leta evidence, alimuuaje na kwanini?
Mnapoleta tuhuma nzito kama hizi ambatisheni na ushahidi. Sasa ukiniambia Nyerere aliuawa na Mkapa bila evidence nitatofautishaje maneno yako na yale ya walevi? Maana walevi wanaweza kusema lolote lililo akilini mwao na kuliapia bila hata kulijua ukweli wake. Na wewe ni kama hao? Leta evidence, alimuuaje na kwanini?
Jifungie ndani ulie weeee ukija kunyamaza utakuwa unajiskia nafuu badala ya kupaka Chama Chako Mavi
Huyu jamaa ni mzima wa afya njema, hajafa. Kwasababu zifuatazo:-
1. Kifo chake kilitangazwa tu na serikali ya CCM, baada ya kuhojiwa na CCMISS. Hakuna hospital yoyote nchini marekani iliyothibitisha kifo chake.
2. Katika daftari la vizazi na vifo, hajaandikwa huko marekani alikofia wala Tanzania alipozaliwa.
3. Mpaka leo hakuna tangazo la mirathi lililotolewa na mahakama yoyote (reason: hakuna cheti cha kifo)
4. Ndio msiba wa usiri zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Tanzania (Hakuna ndugu yoyote aliyeruhusiwa kuuona mwili wa marehemu).
5. Wakati wa kuwekwa kaburini (kama lipo) hakuruhusiwa mwanafamilia yoyote kushuhudia.
6. Katika hali ya kushangaza zaidi, mama wa marehemu (hewa) alifungiwa ndani, ni ilikuwa ni kwa kibali maalum toka Ikulu (c/o BOT) ndipo mtu aliweza kumwona na kumpa pole chini ya uangalizi wa CCMISS.
7. Waandishi wa habari hawakuruhusiwa kuonana na ndugu, ila kwa kibali maalum na chini ya usimamizi mkali.
IWAPO WATANZANIA WALIWEZA KUPATA FURSA YA KUUAGA MWILI WA MAREHEMU BABA WA TAIFA, KULIKONI KWA MWIZI WAO MKUU DAUDI BALALI. KULIKUWA NA UNYETI GANI KWA MWILI HUO KIASI KWAMBA HATA MAMA YAKE MZAZI ALIKATALIWA KUUONA? BALALI YU HAI.
nadhan mtoa mada akifa atasema CCM IMEMUUA KWA KUJITOA KWAKE Kwenye chama.
CCM OYEEEEEE!
Mnapoleta tuhuma nzito kama hizi ambatisheni na ushahidi. Sasa ukiniambia Nyerere aliuawa na Mkapa bila evidence nitatofautishaje maneno yako na yale ya walevi? Maana walevi wanaweza kusema lolote lililo akilini mwao na kuliapia bila hata kulijua ukweli wake. Na wewe ni kama hao? Leta evidence, alimuuaje na kwanini?
kamugisha nakpata vzr sana,we ni mweupe au mtupu kichwani!weka namba yako ya uanachama hapa ya ccm,acha porojo,
unachokataa ndicho unachokifanya.Nimekwambia changia bila kutukana! Kweli unawaza kwa kutumia M>A>S>A<B>U<R>I
Duh mwenzetu ulitumia ujanja gani hadi ukawa mhaya???C lazima niiandike yote, ndo maana nkatoa nafasi ya wao kunishawishi nibaki kuwa vitendo hivyo havikufanywa na ccm, na nikatoa nafasi kwa wapinzani wanishawishi, nadhani umenielewa.
Na kwa taarifa yako, hakuna Mhaya yeyote yule ambae ni Mweupe kichwani hata kama hajaenda shule na kwa taharifa yako tu mimeshapita kwenye ngazi za degree, sawa dogo. Hivyo si mweupe kichwani kama unavyofikiria.