STRUGGLE MAN
JF-Expert Member
- May 31, 2018
- 8,638
- 16,568
Pelosi: Kumzuia Trump kuanzisha vita dhidi ya Iran ni kwa maslahi ya Wamarekani
Feb 14, 2020 12:01 UTC
[https://media]
Spika wa Bunge la Wawakilishi katika Kongresi ya Marekani, Nancy Pelosi, ametoa taarifa baada ya kupitishwa azimio la Baraza la Seneti la kumuwekea vizingiti rais wa nchi hiyo kuhusu kuanzisha vita dhidi ya Iran.
Katika taarifa yake, Pelosi amesema: "Bara la Seneti kwa kupitisha azimio kuhusu uwezo wa kuanzisha vita, limeungana na Baraza la Wawakilishi na limetekeleza majukumu yetu kama Kongresi ya Marekani kwa lengo la kulinda usalama wa watu wa Marekani."
Pelosi ameongeza kuwa: "Uamuzi huo ambao unaweka vizingiti kuhusu kuanzisha uhasama na Iran bila kushauriana na Kongresi pia utalinda maisha ya wanajeshi, wanadiplomaisa na maafisa wengine wa Marekani."
Pelosi amesema hivi sasa zaidi ya wanajeshi 100 wa Marekani wamepata majeraha mabaya ya ubongo baada ya Iran kuvurumisha makombora katika kituo cha jeshi la Marekani cha Ainul Assad nchini Iraq lakini Donald Trump anasema kilichowasibu wanajeshi wa Marekani ni maumivu ya kichwa tu.
[https://media]Baraza la Seneti
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani amesema Trump anapaswa kusikiliza matakwa ya Kongresi na watu wa Marekani kwani Marekani na dunia haiwezi kustahamili vita tena.
Siku ya Alhamisi Baraza Seneti la Marekani lilipitisha azimio la kupunguza uwezo wa Trump kuanzisha vita dhidi ya Iran. Azimio hilo lilipitishwa kwa kura 55 za ndio huku wajumbe 45 wakilipinga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Feb 14, 2020 12:01 UTC
[https://media]
Spika wa Bunge la Wawakilishi katika Kongresi ya Marekani, Nancy Pelosi, ametoa taarifa baada ya kupitishwa azimio la Baraza la Seneti la kumuwekea vizingiti rais wa nchi hiyo kuhusu kuanzisha vita dhidi ya Iran.
Katika taarifa yake, Pelosi amesema: "Bara la Seneti kwa kupitisha azimio kuhusu uwezo wa kuanzisha vita, limeungana na Baraza la Wawakilishi na limetekeleza majukumu yetu kama Kongresi ya Marekani kwa lengo la kulinda usalama wa watu wa Marekani."
Pelosi ameongeza kuwa: "Uamuzi huo ambao unaweka vizingiti kuhusu kuanzisha uhasama na Iran bila kushauriana na Kongresi pia utalinda maisha ya wanajeshi, wanadiplomaisa na maafisa wengine wa Marekani."
Pelosi amesema hivi sasa zaidi ya wanajeshi 100 wa Marekani wamepata majeraha mabaya ya ubongo baada ya Iran kuvurumisha makombora katika kituo cha jeshi la Marekani cha Ainul Assad nchini Iraq lakini Donald Trump anasema kilichowasibu wanajeshi wa Marekani ni maumivu ya kichwa tu.
[https://media]Baraza la Seneti
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani amesema Trump anapaswa kusikiliza matakwa ya Kongresi na watu wa Marekani kwani Marekani na dunia haiwezi kustahamili vita tena.
Siku ya Alhamisi Baraza Seneti la Marekani lilipitisha azimio la kupunguza uwezo wa Trump kuanzisha vita dhidi ya Iran. Azimio hilo lilipitishwa kwa kura 55 za ndio huku wajumbe 45 wakilipinga.
Sent using Jamii Forums mobile app