Namtumia Pompeo

Namtumia Pompeo

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
15,819
Reaction score
40,326
Habari njema...

Hamuwezi amini ila imeanza ku work.

Kwa muda wa siku mbili humu kumekuwa na post za utani na nyingine za kweli zikitishia kutuma video za matukio ya uhalifu kwenda kwa pompeo au Bibi bensouda.

Mara ya kwanza nilipuuzia ila aisee mbinu hi imeanza kuprove effectiveness wale jamaa wanaovaa kijani mmoja wao ni rafiki yangu amenidokeza kwamba Kuna mahali wameambiwa kwamba wanapofanya vitendo vya kukihami au kukitetea chama kwa tafsiri yao basi ni vema kusiwe na utambulisho unaowadefine wao ni kina Nani ili kuepuka kurekodiwa kwa pics na video hizo kwenye mitandao ya kijamii.

Nikamuuliza kwann mbona hizi ni siasa za miaka yote akasema chama kimeanza kuwa na wasiwasi na matukio ya kweli yanayorekodiwa Kama ushahidi na mwisho wa siku yatatumiwa dhidi Yao.

Natoa wito kwa wapenda haki popote walipo wakusanye ushahidi wa kweli bila kumsingizia watu kama ule wa heri James na ule wa bulembo aliesema zitto auwawe.

Kusanyeni ushahidi huu msiufute utatufaaa Sana badae.

#hashtagnamtumiapompeo# imewaogopesha Sana.
 
Hivi walifikiri upinzani kukubali kushiriki chaguzi zilizonajisiws na CCM walikua wajinga. Walikuwa wanakusanya evidence. Na ile ya RC kubebwa na polisi baada ya Mwikabe kushinda kwa magumashi
Aiseee akili kubwa Sana ilitumika nimeamini upinzani Kuna majasusi yaliyokubuhu Yani maccm yameingia kwenye mtego na yamenasa kweli na ni doa kubwa sana ule uchaguzi maana tayari umeshaingia kwenye rekodi mbaya sana duniani.
 
Aiseee akili kubwa Sana ilitumika nimeamini upinzani Kuna majasusi yaliyokubuhu Yani maccm yameingia kwenye mtego na yamenasa kweli na ni doa kubwa sana ule uchaguzi maana tayari umeshaingia kwenye rekodi mbaya sana duniani.
Meko alijisifu Sana eti "hata kususia uchaguzi nayo Ni demokrasia" kumbe wametegwa.
 
Lakin bado haitasaidia!!!Mbowe organise vijana waingie msituni!!Operation Dai Demokrasia (ODD)!Angalau mtaitikisa serekali!!!!
 
Watanzania tujirudi na kujithamini uzalendo wetu ukoje! Haingiii akilini kujisifia kwa kufanya kitendo cha kuiabisha nchi yako nchi za nje. Ukiwa ni mzalendo wa nchi yako pendwa huku unajitambua ni muhimu kutoidhalilisha nchi huko nje eti unajifanya kutetea demokrasia.

Tanzania ni ncji huru hivyo yabidi itokeapo misuguano na mtafaruku ndani ya nchi busara na hekima mapungufu yote yamalizwe kwa kutumia vyombp vya usuluhishi vilivyopo Tanzania.

Huyo Pompeo hawasaidii watz kujenga nchi yetu kwa vile kamwe hana uchungu na Tanzania. Tuachane na mabeberu hawana nia ya kutusaidia bali watazidi kutudhoofisha jitihada zetu kuelekea uchumi wa viwanda hatimaye Tanzania kuwa donor country. Watz tujitambue ipasavyo, wakati ni huu. superbug,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom