Namtafuta baba yangu na ukoo wake

Namtafuta baba yangu na ukoo wake

yamadonga

Member
Joined
Nov 15, 2016
Posts
32
Reaction score
28
Habari wana jamvini !!

Mim ni kijana wa miaka kadhaa sahiv. Lengo langu kuu mim kuingia humu ni kumtafuta baba yang na ukoo wake namfahamu kwa jina tu la ALEXANDER SESELELA.. Lakin maisha yang yote sikuwahi kumuona na mtu ambaye angeweza kunisaidia mimi kumfahamu ni mama yangu ambaye ni marehemu tokea nipo mdogo.. kwa yeyote atakaye kuwa anamfahamu au anaelewa kuhusu huo ukoo naomba ani PM..

Natanguliza shukrani

Maelezo Zaidi

Mama yangu alikuwa n askari magereza..tulikuwa tunaishi mimi na yeye Tabora kabla ya mwaka 2001 kuamia Mbeya na 2002 yey kufariki.. Sijawahi kusikia chochote kuhusu Baba wala kumuona

Mama alikuwa anaitwa Marietha Zacharia na alikuwa ni Mfipa.. kuhusu upande wa Baba sifaham chochote
 
Kila la kheri chief,kuwa rahisi zaidi ungeongeza labda na kabila au mara ya mwisho kupata taarifa zake alikuwa mkoa gani nk
Nashukuru sana Mkuu.. ili mimi sina chochote ninachofahamu kuhusu yeye zahid ya jina lake
 
Pole ndugu....umeonesha nia kutafuta na kujua CHIMBUKO LAKO......Naomba wana JF kwa pamoja tukupe USHIRIKIANO wa kutosha.


Ni wachache wenye ujasiri kama wako. Nikiwa naamini pengine ni 30℅ ya watoto hukimbiwa na wazazi (Baba) wao.
 
Huu Ukoo kama wakina Seselela upo sana South Africa.

Kwa hii mitandao utampata mkuu.
 
Ongeza ongeza nyama mkuu kwa mf. Baba/huo ukoo ni wenyeji wa wapi, mara ya mwisho wewe kusikia walikuwa mkoa gani??
 
Ukifanikiwa Ukimpata utuletee mrejesho mkuu...nitafurahi kusikia hivyo..
 
Vyema ungeongezea maelezo, mama yako alikuwa akiishi wapi..na ni miaka ipi..na enzi hizo hata kwa kusikia baba na mama yako walikuwa mkoa gani? Tia tia vitu ambavyo vitaleta maana.

Hatujala na hata tukila hatushibi.
 
ndgu taarifa hazijitoshelez mbona,jalibu kuorodhesha yafuatayo
taalifa za mama
i.yy aliitwa nan
ii.kabila gan na alikuwa mkaz wa wap
iii.alikwambia alikutana wap na baba yako
iv.marafik wa mama yako ambao baba yako anaeza kuwa anawafaham
v.mama alikuwa na mwonekano gan na haiba gani

taarifa za baba pia angalau weka
i.kabila lake
ii.mama kakwambia baba alipendelea maeneo gan hapa tz
iii.baba alikuwa anajishughulisha na kaz gan
iv.alikwambia baba anaonekana vp
v.taja angalau rafk yyte wa baba ambaye mama alikwambia iki kama baba hayupo angalau rafiki akupeleke ukaone kaburi na ufaham ndguzo
vi.waliishi wap na je mama aliwah kukwambia kwann baba aliondoka!!!
mungu akutangulie katika juhudi zako za kutafta ndguzo
 
Back
Top Bottom