Nampenda ila simuelewi

Nampenda ila simuelewi

marriam

New Member
Joined
Jan 30, 2013
Posts
1
Reaction score
0
Habari wana JF, Nina mpenzi ambaye nampenda sana na tumeanza chini sana akiwa hana hata kitanda,leo hii ana kila kitu amenibadilikia na anasema anakwenda oa kwao coz kachaguliwa mke na wazazi wake.Nashindwa nifanyeje na ukizingatia vitu vyote vya ndani tumenunua wote,ushauri wenu wapendwa.
 
kha!! nawe umeingizwa mujini....wanaume wabaya...wanakaa na wewe kumbe hawana mpango wowote wakukuoa. pole sana. kwani jamaa mmedumu nae miiaka mi ngapi?
 
Ndio tatizo la kuwa too nice mara nyingi mnakuwa not appreciated. Ungekuwa pasua kichwa uone kama asingekuhangaikia!
Halafu mnanunua vitu jointly bila mkataba (ndoa), kweli mnajua kupenda!
 
huyo hana msimamo chukua vyako temana nae!

Ni rahisi kuchukuwa vitu kuondoka lakini si rahisi kumpata mwingine mliyezoeana kama huyo mliyekaa muda mrefuu kwa kuaandaana. Kumbuka miaka hii ukikwaza hata akija mwingine mwenye uso unaoona aibu huwezi mwamini hivyo usiwe mwepesi kushauri kitu ulichokifanya wewe mahusiano yana mengi...

Kuondoka kwenye mahusiano uliyo/mliyoyaanda wenyewe ni rahisi ila kuyapata huko uendako ni ndoto.
 
Pole..lkn kama anafanya hivyo huyo si riziki..ondoka japo inauma lkn utapona na utampata anayestahili
 
Habari wana JF, Nina mpenzi ambaye nampenda sana na tumeanza chini sana akiwa hana hata kitanda,leo hii ana kila kitu amenibadilikia na anasema anakwenda oa kwao coz kachaguliwa mke na wazazi wake.Nashindwa nifanyeje na ukizingatia vitu vyote vya ndani tumenunua wote,ushauri wenu wapendwa.

Pole mdada... Wanaume hawa.... wakiwa hawana kitu huwa wanyenyekevu sana kiasi cha kuweza hata kukulamba miguu... Akishapata weeee UTALIJUA JIJI....
 
Ni rahisi kuchukuwa vitu kuondoka lakini si rahisi kumpata mwingine mliyezoeana kama huyo mliyekaa muda mrefuu kwa kuaandaana. Kumbuka miaka hii ukikwaza hata akija mwingine mwenye uso unaoona aibu huwezi mwamini hivyo usiwe mwepesi kushauri kitu ulichokifanya wewe mahusiano yana mengi...

Kuondoka kwenye mahusiano uliyo/mliyoyaanda wenyewe ni rahisi ila kuyapata huko uendako ni ndoto.

Atapata tu.... Kwani huyo mwanaume ni ngozi ati alizaliwa naye?????? Tupa kule
 
Binafsi nakushauri achana naye maana anazidi kukupotezea muda. Chukua kilicho chako kaanze maisha mapya. Maisha ni safari.
 
pole sana kama ameamua hivyo chukua vilivyo vyako ondoka
 
Habari wana JF, Nina mpenzi ambaye nampenda sana na tumeanza chini sana akiwa hana hata kitanda,leo hii ana kila kitu amenibadilikia na anasema anakwenda oa kwao coz kachaguliwa mke na wazazi wake.Nashindwa nifanyeje na ukizingatia vitu vyote vya ndani tumenunua wote,ushauri wenu wapendwa.
Endelea kupenda hivyo vitu mlivyonunua pamoja utashangaa ndo kitakuwa chanzo cha ugomvi wenu,maana ndo vinakuweka bila hivyo angesha kupiga teke maana kwa kauli hiyo in red,jamaa ameshahamisha kambi.....
 
Pole shosti,yalinikuta mimi hayo afadhali wewe vitu mie nilichukua mkopo nikampa ili aongeze biashara kujua nii mume mtarajiwa alikwenda kuoa mtoto wa shangazi yake eti kisa familia walimshikilia, sikufichi niliumia SANA,lakini nashukuru
deni nilimaliza nikapata mume nikaolewa maisha yanaeledelea,sikumdai hata senti moja na niliapa kua sitotaka story nae
wala mazowea na kama yatakuwepo ni salam basi, kama unavyojua jasho la mtu halipotei baada ya miaka mi3 walifumaniana
na mke duka likaibiwa kachukua mkopo bank nyumba ikachukuliwa na bank sasaivi anakaa vijiwe vya kahawa,akiniona anaona haya ananikimbia,kamtuma mpaka mamake aje kumuombea nikamwambia mie nishamsahau hasa wala sijui kama nilikua na kituko kile...kwahiyo usidai songa mbele utapata vyengine usijishushe thani kwa fridge au kitanda hata kama umenunua wewe muache achukue....
 
Habari wana JF, Nina mpenzi ambaye nampenda sana na tumeanza chini sana akiwa hana hata kitanda,leo hii ana kila kitu amenibadilikia na anasema anakwenda oa kwao coz kachaguliwa mke na wazazi wake.Nashindwa nifanyeje na ukizingatia vitu vyote vya ndani tumenunua wote,ushauri wenu wapendwa.

Hapo ndipo mnapokoseaga, si kila uhusiano lazima uzae ndoa ... hebu wewe mwenyewe jiangalie na jiulize, unastahili kuwa mke?Jiangalie vizuri ndani mpaka nje! Then, kumbuka mkataba wenu ulikuwa ni wa ndoa au baada ya 'show' ukaleta ujanja wa kumganda mshkaji mazima? Mwisho, huwa mnapenda sana hii kitu ya "Alikua hana kitu, vitu vyote tumenunua wote" Mmmh????95% huwa mnakuza mambo, sidhani kama vitu VYOTE mmenunua wote ....

Ushauri wangu, kama kweli una amini, wewe ni 'kifaa' chapa lapa, MUNGU anakuona, utang'aa mbele kwa mbele ....
 
pole..lkn kama anafanya hivyo huyo si riziki..ondoka japo inauma lkn utapona na utampata anayestahili
mambo ya joint venture yamesanuka,hivi unanunuaje vitu na mwanaume hata kwao hupajui?
Je ukifa ghafla .mimi viotu vyangu nimemuandika baba yangu na my late mother ,unanunua vitu na mwanaume kiwanja ,nyumba ukifa ghafla anafaidi huko ndugu zako hawapati chochote...wanawake sometimes sisi mbuzi sana
 
hapo ndipo mnapokoseaga, si kila uhusiano lazima uzae ndoa ... Hebu wewe mwenyewe jiangalie na jiulize, unastahili kuwa mke?jiangalie vizuri ndani mpaka nje! Then, kumbuka mkataba wenu ulikuwa ni wa ndoa au baada ya 'show' ukaleta ujanja wa kumganda mshkaji mazima? Mwisho, huwa mnapenda sana hii kitu ya "alikua hana kitu, vitu vyote tumenunua wote" mmmh????95% huwa mnakuza mambo, sidhani kama vitu vyote mmenunua wote ....

Ushauri wangu, kama kweli una amini, wewe ni 'kifaa' chapa lapa, mungu anakuona, utang'aa mbele kwa mbele ....
ishakula kwake,kamegwa bure na vitu kamnunulia jamaa
 
Pole mdada achana nae songa mbele hao ndio magumegume.....
 
Usiumize kichwa, ni kweli unampenda. Sema naye kwa upya, ikishindikana usilazimishe huenda kuna kitu chako kizuri kinakuja. Kuna wengi yalliwakuta ila baadae wakapata watu na kusema bora waliachana na wale wa awali.
 
Back
Top Bottom