Nampenda ila kumuambia naogopa.....

Nampenda ila kumuambia naogopa.....

Kuna demu nilimwambia nampenda alichonijibu [emoji22] [emoji4] [emoji3]
Hicho ndio naogopaga mwenzetu. Hii midada kama haijakupenda halafu umtamkie nakupenda atavyokutazama hivyo unaweza dhani umepakaa mavi..
 
Kama umesema
bint ambae imetokea kumpenda ila nahisi nikimuambia hatanikubali.. Nitumie njia zipi ili nimshawishi anikubali?????

Yann ushaurii
Ndio naomba njia za kuweza kumshawishi anikubali. Nampenda
 
Nafikiri hapa kinachokupa shida ni ikiwa hata kukubalia kwa sababu mbalimbali ikiwamo kuwa tayari kwenye mahusiano au kutokuwa tayari kuingia kwenye mahusiano.

Kumwambia hisia zako ni jambo muhimu sana. Lazima uwe jasiri. Jambo LA msingi, uwe tayari kiakili, unaweza kukutana na hali nilizozieleza hapo juu. Ukikataliwa, Kubali na ruhusu maisha yako yaendelee. Amino utakutana na mwingine na unaweza kujikuta una mahabs mazito zaidi.

Kama una nia ya dhati kabisa, tafuta njia nzuri ya kumueleza. Njia ya kwanza ningeshauri ukutane naye mwenyewe. Huna sababu ya kuwa na hofu kwani umeshajiandaa kisaikolojia.

Ukiona huwezi kukutana naye mwenyewe, basi tafuta rafiki yake wa karibu, akufikishie ujumbe. Pia, unaweza kumdodosa huyo rafiki ili kujua hali yake ya mahusiano, hii itakusaidia.

Kila LA kheri ndugu.
Ahsante kwa ushaur mkuu oltung'anyi
 
Back
Top Bottom