Namna TRA inavyomhujumu Rais wetu mpendwa

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
Inaumiza sana kwa hizi hujuma za wazwaz kabisa ambazo TRA inafanya. Kuwachonganisha wafanyabiashara na Mh Rais. Ionekane serikali yake inaonea na kunyanyasa wafanya biashara. Ionekane haiwajali.

1. TRA walianza na kukusanya Kodi. Hapa hatukuwa na shida ndiyo ilikuwa kazi yao. Wakasifiwa sana kwa ukusanyaji, wakamaliza.

2. Wakaja mara ya pili wakaanza kukusanya MITAJI yetu. Hapo ndo wengi tumejikuta tumefunga biashara.

3. Mara ya Tatu wanakuja kukusanya Mali tulizobaki nazo. Hapa tumejikuta wengine tunaamua kuziuza tu hasara ili tubaki bila kitu. Ijulikane moja.

4. Mara ya NNE sasa wanakuja KUTUKUSANYA SISI. Ole wetu sisi. Ole wetu. Ingetufaa zaidi tufungwe jiwe la kusagia na kutupwa baharini.

Mh. Rais unahujumiwa. Wametukamua maziwa, sasa wanatukamua Damu. Wanategemea tutaishi vipi?
 
TRA ndiyo wanatunga wao hizi sheria mbovu mbovu? Yeye mwenyewe ana shangilia kila siku kuwa amevunja ukusanyaji wa mapato.
 
Anahujumiwa vipi ilihali kila siku anawasifia wanavuka lengo la ukusanyaji?, usidhani hajui yanayoendelea yeye na serikali yake wamebariki haya yanayoendelea.
Wanavuka lengo ee? Mwishoe hakuna makusanyo kabisa.
 
Anahujumiwa vipi ilihali kila siku anawasifia wanavuka lengo la ukusanyaji?, usidhani hajui yanayoendelea yeye na serikali yake wamebariki haya yanayoendelea.
... shamba boy kaingia zizini kama ilivyo kawaida kukamua. Badala ya kukuletea maziwa, katoka humo na damu ndoo mbili na wewe unamsifu! Utakuwa mtu wa ajabu kweli.
 
Lazima tukubali kuwa hili jambo ni matokeo ya sheria na kanuni zilizo wekwa hivyo TRA wanazitekeleza hizo. Hakuna anaye muhujumu Rais.... kwanini Rais na viongozi vingine wasiingilie kati kama si maelekezo yao?
Mimi naomba wachukue ushauri wa Nape warekebishe hakuna anaye hujumu mtu
 
Tangu 2015, TRA haijabadilika, kilichobadilika ni Serikali.

TRA ya sasa inatekeleza matakwa ya Serikali ya Magufuli.

Ukiona TRA wanavyofanya, ndiyo ujue kuwa huo ndiyo utawala wenyewe wa Magufuli.

Ukiona Polisi wanavyofanya, ndiyo ujue kuwa huo ndio utawala wenyewe wa Magufuli.

Ukiona wasiojulikana wanavyoteka watu na kuwapoteza, ujue kuwa huo ndio utawal wenyewe wa Magufuli.

Ukiona DPP anavyowabambikia watu kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, ujue kuwa huo ndio utawala wenyewe wa Magufuli.

Tusipindishe, wala kuwalaumu wasiohusika, haya yote mabaya yanayoendelea kwenye uchumi na biashara, chanzo ni Magufuli. Wengine wote mnawaonea.
 
4. Mara ya NNE sasa wanakuja KUTUKUSANYA SISI. Ole wetu sisi. Ole wetu. Ingetufaa zaidi tufungwe jiwe la kusagia na kutupwa bahari
Amin Amin nakuambia... Mara ya tano wataanza kujikusanya wao wenyewe. . . maana watajikuta wenyewe tu eneo la kukusanyia... hivo ili wamfurahushe mzee baba itabidi waanze kupelekana wao kwa wao.
 
Nilishandika humu kuwa Rais aliwahi kuwapiga siasa wafanyabiashara katika kikao cha nje, baada ya muda mfupi akawa na kikao cha ndani na wakuu wa TRA, alichowaambia ndani ni kuwa “Mimi ninachotaka ni kodi” (kwa ile lafudhi yake) Bado mleta mada unadhani kuna mtu anahujumiwa na TRA? TRA wenyewe wana stress za kufikisha na kuvuka lengo 😀
 
Nilishandika humu kuwa Rais aliwahi kuwapiga siasa wafanyabiashara katika kikao cha nje, baada ya muda mfupi akawa na kikao cha ndani na wakuu wa TRA, alichowaambia ndani ni kuwa “Mimi ninachotaka ni kodi” (kwa ile lafudhi yake) Bado mleta mada unadhani kuna mtu anahujumiwa na TRA? TRA wenyewe wana stress za kufikisha na kuvuka lengo 😀
Inatisha kiasi kwamba tunaogopa kuanzisha biashara maana ukianzisha tu tayari unafuatwa ni mgogoro nao kodi kodi.
 
Inaumiza sana kwa hizi hujuma za wazwaz kabisa ambazo TRA inafanya. Kuwachonganisha wafanyabiashara na Mh Rais. Ionekane serikali yake inaonea na kunyanyasa wafanya biashara. Ionekane haiwajali.

1. TRA walianza na kukusanya KODI. Hapa hatukuwa na shida ndiyo ilikuwa kazi yao. Wakasifiwa sana kwa ukusanyaji, wakamaliza.

2. Wakaja mara ya PILI wakaanza kukusanya MITAJI yetu. Hapo ndo wengi tumejikuta tumefunga biashara.

3. Mara ya TATU wanakuja kukusanya MALI TULIZOBAKI NAZO.hapa tumejikuta wengine tunaamua kuziuza tu hasara ili tubaki bila kitu. Ijulikane moja.

4. Mara ya NNE sasa wanakuja KUTUKUSANYA SISI. Ole wetu sisi. Ole wetu. Ingetufaa zaidi tufungwe jiwe la kusagia na kutupwa baharini.


Mh. Rais unahujumiwa. Wametukamua maziwa, sasa wanatukamua Damu. Wanategemea tutaishi vipi?
It is his own making.
 
Back
Top Bottom