Namna ya kutengeneza Sambusa

Nov 14, 2013
67
42
Viamba vya upishi

1. Manda za sambusa kiachi 40 -50
2. Mafuta ya kukaangia lita moja
3. Nyama ya kuku iliyosagwa kilo moja
4. Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja
5. Pilipili mbichi iliyosagwa kiasi kama utapendelea
6. Pilipili manga kijiko kikoja cha mezani
7. Bizari nyembamba ya unga kijiko kimoja cha chai
8. Bizari ya mchuzi kijiko kimoja cha chai
9. Juisi ya ndimu kijiko kimoja cha mezani
10. Mbogamboga mchanganyiko kikombe kimoja cha chai
11. Chumvi kiasi
12. Vitunguu maji vilivyokatwakatwa kikombe kimoja
13. Kotmiri iliyokatwa vijiko viwili

Jinsi ya kupika
1. Pika nyama ya kuku ya kusagwa kwa kutia chumvi, kitunguu saumu na tangawizi, pilipili, ndimu na bizari zote.

2. Ikikaribia kuiva tia mboga za mchanganyiko. Changanya vizuri kisha ipua na weka pembeni halafu weka vitunguu na kotmiri. Chukua manda zako na weka mchanganyiko wa nyama na kisha funga.

3. Baada ya hapo weka mafuta jikoni na yakishapata moto anza kuweka sambusa zako jikoni na kanga hadi ziwe za hudhurungi. Ipua na weka pembeni.

Sambusa zako zitakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kula sambusa na kinywaji cha aina yeyote na kufurahia ladha yake.

kufunga.jpeg
 
Huko giningi kwenu kuna sambusa ?siyo ulojo
Viamba vya upishi

Manda za sambusa kiachi 40 -50
Mafuta ya kukaangia lita moja
Nyama ya kuku iliyosagwa kilo moja
Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja
Pilipili mbichi iliyosagwa kiasi kama utapendelea
Pilipili manga kijiko kikoja cha mezani
Bizari nyembamba ya unga kijiko kimoja cha chai
Bizari ya mchuzi kijiko kimoja cha chai
Juisi ya ndimu kijiko kimoja cha mezani
Mbogamboga mchanganyiko kikombe kimoja cha chai
Chumvi kiasi
Vitunguu maji vilivyokatwakatwa kikombe kimoja
Kotmiri iliyokatwa vkijiko viwili

Jinsi ya kupika


Pika nyama ya kuku ya kusagwa kwa kutia chumvi, kitunguu saumu na tangawizi, pilipili, ndimu na bizari zote.
Ikikaribia kuiva tia mboga za mchanganyiko. Changanya vizuri kisha ipua na weka pembeni halafu weka vitunguu na kotmiri. Chukua manda zako na weka mchanganyiko wa nyama na kasha funga.
Baada ya hapo weka mafuta jikoni na yakishapata moto anza kuweka sambusa zako jikoni na kanga hadi ziwe za hudhurungi. Ipua na weka pembeni. Sambusa zako zitakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kula sambusa na kinywaji cha aina yeyote na kufurahia ladha yake.
 
Wana jf chef naombeni mnaofahamu haya mapishi tushirikishane yaani mapishi ya sambusa, kababu nk.
 
nimeikuta mahala
Vinavyohitajika
·Nyama ya kusaga ½ kilo
·Vitunguu maji 4 vikubwa
·Kotmiri ¼
·Pilipili nzima 2 lakini sio kali
·Bizari nzima iliyosagwa kijiko 1 cha chakula
·Pilipili manga kijiko 1 cha chakula

·Kaki za sambusa (unaweza kununua zilizokuwa tayari zimeshakatwa kwa ajili ya sambusa au kama utanunua zile sheet pana utazikata kwa inchi 4 upana wa ruler yaani upate mistari 3 kwa kila sheet)

·Thomu na tangawizi iliyosagwa kijiko 1 cha chakula
·Mafuta ya kupikia kiasi
·Unga wa ngano vijiko 4 vya chakula au ute wa yai(kwa ajili ya kufungia sambusa)

Namna ya kutayarisha na kupika
·Kausha nyama ya kusaga kwa thomu na tangawizi pamoja na chumvi mpaka ikauke vizuri
·Iwache ipoe
·Kata kata majani ya kotmiri weka upande
·Kata kata vitungumaji vipande vidogo vidogo(chop)
·Zikate pilipili zako slice za mviringo vidogo vidogo

·Wakati ukimaliza matayarisho haya na nyama yako itakuwa ishapoa kabisa hapo ndio utachanganya,bizari nzima pamoja na pilipili manga pamoja na vitu vyote ulivyokwisha vitayarisha

·Koroga unga ndani ya kibakuli au ute wa yai

·Weka kaki kwa mfungo wa triangle yani pembe tatu kama kofia na weka mchanganyiko wa nyama yako kiasi na uanze kuzifunga sambusa zako na ukifika mwisho hapo ndipo upake unga wako kwa ajili ya kuifunga isifunguke wakati wa kuchoma, pendelea kutumia kaki 2 kwa kila sambusa moja

·Kuchoma kwake ikiwa unazifanya na kuzichovya hapo hapo mafuta lazima yawe baridi (ninakusudia uweke mafuta na uzitie sambusa kabla hayajapata moto)

·Na ikiwa uliziweka kwenye friji zikaganda basi unatakiwa uzichome kwa mafuta ya moto

Kidokezo
Kufunga sambusa kidogo kuna usumbufu lakini jaribu mara kwa mara mpaka utafanikiwa inshaaAllah kiasi cha mikono kuzowea tu kuifuatisha ile triangle.
 
SAMBUSA ZA KUKU
Mahitaji

1. Kidari cha kuku 1 kilo
2. Thomu, tangawizi iliyosagwa 1 kijiko cha supu
3. Kitunguu kilichokatwa vipande vidogo 1
4. Pilipili mbichi 1
5. Pilipili manga 1 kijiko cha chai
6.Bizari upendayo 1 kijiko cha chai
7. Siki 1 kijiko cha supu
8. Mayai 4 – 5
9. Mafuta Kiasi ya kukaangia
10. Sosi
11.Mafuta 3 vijiko vya supu
12. Vitunguu vilivyokatwa (chopped) 2
13. Nyanya zilizosagwa 3
14. Nyanya ya kopo 1
15. Pilipili manga 1 kijiko cha chai
16. Chumvi kiasi
17. Kotmiri iliyokatwa (chopped)

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kababu
1. Chemsha kidari cha kuku kwa siki, thomu, kitunguu kilichosagwa, pilipili mbichi bizari zote na kufunika kipikike bila ya maji hadi kikauke.

2. Tia katika mashine ya kusagia (blender) na usage bila ya kuta maji, kitasagika wenyewe.

3. Tia katika bakuli na upige mayai na kuchanganya. Mchanganyiko uwe unaweza kufanya viduara vya kababu. Kama umekuwa laini ongeza mayai.

4. Katika karai tia mafuta kiasi kidogo tu ya kuweza kugeuza geuza kababu zipikike.

5. Epua na weka katika sufuria.


Sosi
1. Kaanga vitunguu kisha tia nyanya, nyanya ya kopo, pilipili manga, chumvi na endelea kukaanga iwe sosi.

2. Tia kotmiri, kisha mwagia katika sufuria iliyokuwemo kababu.

3. Pika katika moto mdogo kababu zitokote kidogo hadi ziwive vizuri.

4. Epua na pakua katika bakuli, mwagia kotmiri kidogo.

Tayari kwa kuliwa.
 
Nazipenda mno zile ndude akitokea mtaalam nitakuwa muonjaji
Napenda sana sambusa na kikombe cha kahawa ya maziwa yaliyokolea vizuri
 
Mahitaji ya manda(ule mkate wa sambusa):
1. Unga wa ngano 1/4 kg
2. mafuta ya kupikia kiasi
3. maji ya joto la kawaida kiasi
4. Chumvi kiasi


Jinsi ya kutengeneza manda:

  • Changanya unga na maji kidogokidogo mpaka upate donge la unga,hakikisha haushikani.Kata vidonge vidogo vidogo vingi.
  • Sukuma hivo vidonge utengenze vichapati vidogovidogo vingi
  • Kisha weka chapati chini,paka mafuta ienee mafuta vizuri,weka nyingine juu paka mafuta mpaka ziishe,OBS:ile chapati ya mwisho ya juu haipakwi mafuta
  • Pasha chuma cha chapati moto.
  • Ule mlima wa vichapati usukume utengeneze chapati moja kubwa,kwahio utakuwa kama na layers nyingi za chapati.
  • Pasha moto kama dakika tano kila upande.
  • Kata ncha kutoka kwenye hio chapati,
  • Igawe mara tatu/nne inategemea na jinsi utakavyozikunja.
  • Chambua manda ziwe moja moja ,zinatakiwa ziwe nyepesi kwahio unahitajika umakini kwenye kuzichambua au unaweza kuziharibu,
  • Zifunge/zihifadhi kwenye kitambaa ili zisikauke.

Nyama ya sambusa mahitaji:
1. Nyama ya kusaga kilo 1
2. Vitunguu maji 3 vikubwa
3. kitunguu swaumu kijiko kimoja cha supu
4. Tangawizi kijiko kimoja cha supu
5. Chumvi kiasi
6. Pilipili manga kiasi
7. Giligilani fresh(Coriander)
8. Mafuta ya kukaangia 1 liter

Unaweza kuweka mbogamboga nyingine kama unapendelea mfano karoti,viazi,pilipili hoho ila inabidi vichanganywe na nyama ili viive kwanza

Jinsi ya kuandaa

  • Kata kitunguu maji(vipande vidogovidogo/boxes)
  • Kaanga nyama weka chumvi,pilipili manga,tangawizi na kitunguu swaumu,ikoroge ichanguke,isifanye madonge
  • Nyama ikiiwa weka kitunguu maji,Pasha moto kwa dakika 2 na mwishowe weka giligilani ukishaiepua nyama.
Unga wa kufungia sambusa/Gundi
  • Weka unga nusu kikombe cha kahawa kwenye bakuli,changanya na maji mpaka ufanye urojo mzito unaovutana.

Jinsi ya kufunga sambusa:

  • Weka mafuta kwenye karai yapate moto,Usiweke moto mkali.
  • Choma sambusa mpaka zibadilike rangi na ziwe rangi ya gold
  • Sambusa tayari kwa kuliwa.Serve na vipande vya ndimu au limau.
 
Daaaa cmchez hvi haya maujuz mnayatoa wapi jaman we mimi49 na mwenzio Farkhina hv wenzi wenu wanakulagawkwa mama ntilie kwel
 
Last edited by a moderator:
Mahitaji ya manda(ule mkate wa sambusa):
Unga wa ngano 1/4 kg
mafuta ya kupikia kiasi
maji ya joto la kawaida kiasi
Chumvi kiasi

Jinsi ya kutengeneza manda:



  • Changanya unga na maji kidogokidogo mpaka upate donge la unga,hakikisha haushikani.Kata vidonge vidogo vidogo vingi.

  • Sukuma hivo vidonge utengenze vichapati vidogovidogo vingi

  • Kisha weka chapati chini,paka mafuta ienee mafuta vizuri,weka nyingine juu paka mafuta mpaka ziishe,OBS:ile chapati ya mwisho ya juu haipakwi mafuta

  • Pasha chuma cha chapati moto.

  • Ule mlima wa vichapati usukume utengeneze chapati moja kubwa,kwahio utakuwa kama na layers nyingi za chapati.




  • Pasha moto kama dakika tano kila upande.

  • Kata ncha kutoka kwenye hio chapati,
  • Igawe mara tatu/nne inategemea na jinsi utakavyozikunja.
  • Chambua manda ziwe moja moja ,zinatakiwa ziwe nyepesi kwahio unahitajika umakini kwenye kuzichambua au unaweza kuziharibu,




  • Zifunge/zihifadhi kwenye kitambaa ili zisikauke.


Nyama ya sambusa mahitaji:
Nyama ya kusaga kilo 1
Vitunguu maji 3 vikubwa
kitunguu swaumu kijiko kimoja cha supu
Tangawizi kijiko kimoja cha supu
Chumvi kiasi
Pilipili manga kiasi
Giligilani fresh(Coriander)
Mafuta ya kukaangia 1 liter
Unaweza kuweka mbogamboga nyingine kama unapendelea mfano karoti,viazi,pilipili hoho ila inabidi vichanganywe na nyama ili viive kwanza

My D. Uko kwenye angle zoote,daah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom