Shenzi kabisa. Simba hainyenyekei mchezaji kwasababu Simba sio Yanga. Msimu uliopita tumecheza fainali za Shirikisho bila Chama. Hatumuhitaji!Kwa ufupi sana.
Simba wamemkosa Feisal pendekezo la kocha Fadlu, lakini pia uwezekano wa kumpata Allan Okello ni mgumu.
Fadlu ameonesha bado anahitaji mchezji wa kuamua mechi kubwa na kutengeneza nafasi ndani ya 18.
Clatous Chota Chama bado anao uwezo wa kufanya mambo makubwa pale simba "kiufundi zaidi".
Mrudisheni CHAMA
Kwa mbinu za Fadlu amekosa mtu mwenye matumizi makubwa ya akili na miguu kama CHAMANi sahihi bado hatujapata namba 10 wa kutema mate kushoto na akapita kulia, ikishindikana amjaribu na mpanzu.. ana skills za namba 10 shida anapenda sana mbio, kitu kinachomfanya aonekane ni winger zaidi ya AM
Both answers are true, but Chama, NO! Kama wewe unampenda Chama anzisha klabu msajili Chama peke yake ufurahie mpira!Unapenda mpira au Simba?
Huenda kwenye uwanja wa mazoezi Mavambo hakutosha kucheza namba 10 ila kwa uchezaji wake niliona anastahili kucheza juu kuliko alipokua anachezeshwa, bado uwezo wa CHAMA ni mkubwa kushinda Mutale na Ahoua hada kutengeneza nafasi.Badala ya kumuacha, Simba ingempa muda zaidi Fernandez kwa kumsogeza mbele kidogo. Msimu mmoja zaidi kwa nafasi hiyo wangejua kama anatosha au hapana ila nadhani angewashangaza wengi.
Wameweka imani zaidi kwa Janshalewa ambaye sitegemei ufanisi wake kubadilika sana. Hata kwenye faulo hana ufanisi wa kutosha wa kuzitumia hizo nafasi kama anavyosifiwa.
Binafsi sishauri wamrudishe Chama, ni afadhali wamtumie Mpanzu. Mutale akituliza wenge anaweza saidia ila apunguze vipasi vifupifupi na afocus kupiga pasi mpenyezo za mwisho.
Nilimkataa yule Morice na inaonyesha kocha naye hajaridhika naye. Maema naye ni sajili za sifa tu ila siyo zenye faida.
Nilikuwa na doubt taarifa kwamba kocha ndiye anayesajili wachezaji na kwa jinsi ambavyo bado haridhiki, inaonyesha sio yeye anayewachagua na kuwasajili hawa wachezaji.
PS. Nadhani kuna uwezekano wa Simba kumsajili Okello kwa nafasi ya Mutale au hata Mukwala.
Simba walifanya jambo sahihi kuachana na Chama na hawatakiwi kurudi nyuma. Inafika wakati inabidi ukubali mchezaji alichokupa hakiwezi tena kuzidi pale, inabidi utafute kwingine kupata zaidi hata kama utarudi kwanza hatua moja nyuma. Chama kaondoka tu, Simba imefika fainali ya CAF na hao hao kina Janshalewa, hapo inakwambia nini?Huenda kwenye uwanja wa mazoezi Mavambo hakutosha kucheza namba 10 ila kwa uchezaji wake niliona anastahili kucheza juu kuliko alipokua anachezeshwa, bado uwezo wa CHAMA ni mkubwa kushinda Mutale na Ahoua hada kutengeneza nafasi.
Sijawahi kuamini kuwa Fadlu amesajili hao wachezaji mwenyewe. Hajawahi kutamka hilo yeye mwenyewe, zaidi hayo maneno yanapenyezwa kwa wachambuzi na machawa wa viongozi ili mambo yakibuma wao wawe salama.Kama kweli Fadlu anatafuta namba 10 mwingine basi wanachama na mashabiki wa Simba waanze kuandika maumivu mapema kabisa. Na Fadlu atakuwa anatafuta kichaka cha kujificha ikitokea mambo yameenda tofauti. Ana Ahoua na Mutale halafu kawasajili Neo Maema, Morice Abraham na Bajaber sasa anataka nini tena wakati dirisha linaedna kufungwa hivi karibuni. Bado Mpanzu na Nabby Camara wanaweza kucheza hiyo namba 10 vizuri tu. Na tuliambiwa kuwa mwaka huu kasjili tena sasa mlio wa nini?
Fadlu kasema bado anahitaji mtu mwe x factor za kuamua mechi, mtu ambaye alimkosa msimu uliopita hasa kwenye mechi ya fainali CAF na ile ya Yanga. Tafsiri yake ni nini hasa?Simba walifanya jambo sahihi kuachana na Chama na hawatakiwi kurudi nyuma. Inafika wakati inabidi ukubali mchezaji alichokupa hakiwezi tena kuzidi pale, inabidi utafute kwingine kupata zaidi hata kama utarudi kwanza hatua moja nyuma. Chama kaondoka tu, Simba imefika fainali ya CAF na hao hao kina Janshalewa, hapo inakwambia nini?
Ndiyo maana hata Zimbwe ilikuwa sahihi naye kuachana naye ingawa kwa mtazamo wangu kiasi walichelewa kufanya uamuzi huo.
Chama alivoondoka Simba, hawajapata mchezaji mbunifu eneo la mwisho kama yeye au kuzidi yeye.Ni kweli simba inakosa mtu mwenye football IQ kama chama hata huyo sowah ni suala LA muda tutamuona si kitu kwa nature ya no 10 yetu
Arudi tu
Hichilema mkuu nakumbuka nilikuambia kua sajili za hao watu ni mbovu..ona watu wa football wanasema hapa...mutale, maema, morice, bajaber, Hawa wote hawana maana wangeuzwa anunuliwe mtu angalau anaefanana na brilliance ya chama...kwenye football Saivi hauitaji kukimbia ovyo ovyo unaitaji brilliance...Kama kweli Fadlu anatafuta namba 10 mwingine basi wanachama na mashabiki wa Simba waanze kuandika maumivu mapema kabisa. Na Fadlu atakuwa anatafuta kichaka cha kujificha ikitokea mambo yameenda tofauti. Ana Ahoua na Mutale halafu kawasajili Neo Maema, Morice Abraham na Bajaber sasa anataka nini tena wakati dirisha linaedna kufungwa hivi karibuni. Bado Mpanzu na Nabby Camara wanaweza kucheza hiyo namba 10 vizuri tu. Na tuliambiwa kuwa mwaka huu kasjili tena sasa mlio wa nini?