Naliona anguko la mbunge wa Mbeya Mjini

Naliona anguko la mbunge wa Mbeya Mjini

thatha

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2011
Posts
15,340
Reaction score
1,571
Mheshiwa Sugu ni miongoni mwa wabunge waliochaguliwa kwa kishindo kiasi kwamba wananchi walifulika eneo la kuhesabia kura kulazimisha matokeo yatangazwe halaka na ikawa hivyo Sugu akawa mbunge.

Tangu aingie bungeni impact yake kwenye jimbo lake la uchaguzi haijaonekana na pengine imefika mahala baadhi ya watu wameanza kufikiria tofauti juu ya mbunge huyo na pengine kusema wazi kuwa hana anachofanya zaidi ya kubishana bungeni kwa mambo ambayo hayana msaada kwa jimbo lake la uchaguzi.

Kikubwa kinachosubiriwa Mbeya Mjini ni uchaguzi mkuu ili wakazi wa Mbeya waamue vinginevyo na uzuri wa watu wa Mbeya wanachagua mtu si chama kwa hiyo itategemea Sugu atapambana na nani toka vyama vingine ktk uchaguzi mkuu ujao.
 
umetimiza wajibu m-pesa tayari imeshajaa bhana!
 
Nipo Mbeya naishi mbembela,unayosema hayana mashika,kama upo Mbeya utajua ni jinsi gani TISS wametumia siku4 kuwabembeleza vijana wa bodaboda na bajaji ili waunge mkono,vikao zaidi ya vinne na posho za elfu hamsini walau wahudhulie kwenye maandamano ya may mosi!!!!Nakupa changamoto moja nenda Uyole ukaseme hivyo!!!
 
Ifike kipindi Nape naye atafute vijana waongo zaidi, manake kama huyu mtoa mada hana msaada kabisa kwa CCM. Ni mdhaifu sana!
 
Mtaalamu mmoja wa lugha aliwahi kusema kuwa watu wengi hasa waafrika hawataki watu wao wasemwe kwa chochote hata kama wanamapungufu ndicho ninachokiona kwa baadhi ya watu humu jf.
 
Kaka kama kunamtu mbeya asiye na ushabiki ukiongea naye atakupa clear picha.
mkuu mi natokea Mbeya maeneo ya Samora Secondary ? Na sina ushabiki ila sielewi labda uniambie ilitakiwa afanye nini zaidi ya aliyoyafanya au toa mfano wa jimbo ambalo linafaa kuwa mfano wa kuigwa ukilitofautisha na lilipokuwa chini ya Mpesya ?
 
Ifike kipindi Nape naye atafute vijana waongo zaidi, manake kama huyu mtoa mada hana msaada kabisa kwa CCM. Ni mdhaifu sana!
Hata kadi ya ccm siijui inafananaje wasiwasi wako tu sipo huko unapofikiria ila kwa sababu ccm ndo wanafanya usilale shauri yako,nambie uzaifu up wa viungo au wa kitu gani jipambanue siyo unaandika vipande vidogo kama mazoea mitomingi.
 
Umeandika sawasawa mkuu, hata mimi iki kitu nakiona, na sio Sugu tu, na wengine wengi wa CHADEMA hawatarudi 2015 pale bungeni.
 
Mheshiwa sugu ni miongoni mwa wabunge waliochaguliwa kwa kishindo kiasi kwamba wananchi walifulika eneo la kuhesabia kura kulazimisha matokeo yatangazwe halaka na ikawa hivyo sugu akawa mbunge.tangu aingie bungeni impact yake kwenye jimbo lake la uchaguzi haijaonekana na pengine imefika mahala baadhi ya watu wameanza kufikiria tofauti juu ya mbunge huyo na pengine kusema wazi kuwa hana anachofanya zaid ya kubishana bungeni kwa mambo ambayo hayana msaada kwa jimbo lake la uchaguzi.kikubwa kinachosubiliwa mbeya mjini ni uchaguzi mkuu ili wakaazi wa mbeya waamue vinginevyo na uzuri wa watu wa mbeya wanachagua mtu si chama kwa hiyo itategemea sugu atapambana na nani toka vyama vingine ktk uchaguzi mkuu ujao.

ulikuwa unataka kusema nini mkuu?hivi hizi tafiti huwa zinafanywa wapi?au mtu ukimka tu mawazo yako yanakuwa ya wapiga kura 60,000.hivi hao wabunge wa ccm kipindi chote walichokuwa na jimbo walifanya nini?na kwanini hawakuchaguliwa?
 
mi naishi block t,jiran na makao ya Sugu na Mary Mwanjelwa,kiukweli sion tofauti ya Sugu na Mpesya,wote chenga tu..
 
mkuu mi natokea mbeya maeneo ya samora secondary ? Na sina ushabiki ila sielewi labda uniambie ilitakiwa afanye nini zaidi ya aliyoyafanya au toa mfano wa jimbo ambalo linafaa kuwa mfano wa kuigwa ukilitofautisha na lilipokuwa chini ya mpesya ?
Vema mkuu mimi pia natokea mbeya nafundisha sinde sekondari,mwanjelwa ndo mitaa yetu skani kwa mama joni nadhani unapapata tulimchagua sugu kwa imani kubwa hamna alichofanya nini kaka,pengine kamudu kutuliza maandamano ya wamachinga tu basi,kwenye vikao anatukana tu,ilitokea kwenye kikao cha kuchagua wanafunzi w kwenda sekondari alitoa matusi hatukuamini halafu akaondoka.
 
Back
Top Bottom