Nakusihi usije mjini

ndonilivyo

Member
Joined
Sep 9, 2022
Posts
33
Reaction score
39
~ Mchele kilo 3,000, ukila robo inakuhitaji 5kg kwa mwezi ambayo ni sawa na 15,000 (siyo ulaji wa kila siku).

~ Unga wa ugali kilo 2,000, unahitaji kilo 5 - 10 kwa mwezi ambayo inagharimu 20,000 kwa mwezi.

~ Mafuta ya kupikia 1litre 6,000 - 9,500.

~ Bajeti ya mboga na viungo vyake 3,000 kwa mwezi 90,000.

~ Gas 25,000 - 28,000

~ Nauli 2,000 - 5,000 KWA mwezi tufanye 100,000.

~ Expenses 100,000 eg sabuni, mafuta ya kupaka, umeme, maji n.k.

Hayo ni matumizi ya mtu bachelor, hapo hajaumwa wala kuhonga, hajatuma pesa nyumbani wala kununua nguo, hujamwagilia moyo, hasomeshi, yaani hayo ni maisha basic kabisa ya yeye kusavaivu.

Mwisho wa mwezi anakunja 300,000 - 500,000 mshahara basic kwa kampuni nyingi hapa mjini Daslamu bila kodi wala makato mengine.

Ni kipato cha machinga, fundi selemala, mwashi, cherehani, garage, dereva n.k, baada ya kutoa matumizi ya office.

Eti jamani, mnatuona tuliokuwa Daslamu tunafaidi eeh?
 
Mbona we huhami?
 
Kwamba hizo bei ni za daslam peke yake?
 
Ndo maana ikaitwa bongo. Hili no jiji la wanaume kwelikweli sio watoto wa mama.
 
Kwetu Kenya hivi ndivyo Mambo yalivyo;

1 kg sugar=KSh 180
1ltr salad=KSh 150
1kg bar soap=ksh 240
1kg rice=KSh 180
1ltr milk=KSh 60
1kg maize flour=ksh100
 
hujajipanga tu ila town maisha mbona simple tu.

ukiona unafanya kaz alaf unapiga bajeti zakichovu hivyo bas acha hyo kazi bora ukachimbe vyoo
 
Ndo maana ikaitwa bongo. Hili no jiji la wanaume kwelikweli sio watoto wa mama.
usidanganye watu maisha kila mtu anavyoyapanga jiji la wanaume kweli na hao mashoga mbona tunakaa nao mpka tunawakimbia
 
Hata kama mchele kilo itafika 10000tzs Wali utaliwa tu chamsingi pambana na Hali yako tu
 
usidanganye watu maisha kila mtu anavyoyapanga jiji la wanaume kweli na hao mashoga mbona tunakaa nao mpka tunawakimbia
Unadhani mpaka mwanaume anaamua kuwekwa mchezo? Huyo nae sio mtoto wa mama ndugu ni mtu anayethubutu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…