kinyamkela mahaba
JF-Expert Member
- May 4, 2022
- 1,180
- 1,599
Hii ni historia ya jinsi nilivyokutana na huyu Mchagga na kilichoendelea mpaka kufilisika vibaya.
Wengi humu JF mmekuwa mkinichukulia mtu asiyeeleweka na masikini mno. Hasa baada ya kusema nilikusanya 8000 kwa karibu miezi minne kwa kusave sehemu ya hela nilizopata(sio uongo ni kweli nili save na nauza karanga kwa sasa). Hiki ndicho kilichonitokea,,
Ngoja nianzie hapa:
Mwaka 2010 nilikutana na huyu Mzungu raia wa Sweden visiwani Zanzibar, yeye akiwa ni Mhandisi wa kampuni fulani ya simu HQ. Na alikuwa amekuja Zanzibar kutalii na kupumzika.
Tumuite Linda. Wakati Linda akiwa mapumzikoni Zanzibar, nilikuwa na rafiki yangu aliyeitwa Mick(sio jina halisi) na ndiye aliniunganisha na huyu Mzungu mara baada ya huyu dada kuvutiwa na mimi. Wakati huo nilikuwa nahudumu kama kibarua niliyelipwa kwa siku hapo hotelini.
Na tenda hii pia nilipewa na huyu huyu Mick. So ilikuwa rahisi kwa mimi kukutana na Linda mara kadhaa ingawa sikuwa najua kuwa alinipenda.
Tukaanzisha mahusiano ya mapenzi na kwa kweli kwao hela ilikuwepo. Baba yake mzazi alikuwa na jumba kubwa la kifahari Masaki. Naye alikuwa na pesa.
Nilibahatika kupata naye watoto wawili wa kiume wakati tulipohamia Sweden wote. Alinishughulikia kila kitu kuhusu nyaraka za kupata uraia halali wa Sweden.
Nilikuwa nakaa kule miezi hata miwili naruka nakuja TZ nakaa hata miezi 2 au zaidi na kurejea tena. Hela hizi mil 2 sijui 3 nilikuwa nazichezea mno na zilikuwa kama za mboga kwa wakati huo.
Mama yangu alikuwa akiishi dsm na alikuwa na shamba la hekari 1 Mkuranga. Linda alinitumia hela takribani 90M nakumbuka. Ilikuwa kwa ajili ya kumnunulia mama hekari zaidi ya 30 za mashamba huko Mkuranga na zingine nilimpa kwa matumizi yake. Pia Linda aliniambia nigawe kiasi ninunue pick up kwa ajili ya mama kwenda shambani.
Nikiri nilianza kuingiwa na roho ya usaliti ingawa huyu mama watoto wangu aliniheshimu na kunijali


alinyenyekea na hakuwahi kunikosea heshima hata siku moja.
Nilianza kum cheat mara kadhaa ukizingatia nilishapata marafiki wengi, pindi nikija huku TZ ilikuwa ni kujirusha na starehe za anasa.
Nakumbuka nilikuwa naweka 1M juu ya meza bar nikiwa na rafiki zangu na kuwaambia 'hiyo hela iishe leo', na walishindwa kuimaliza mara kadhaa.
Niliota mapembe na sikusikia la kaka yangu wala nani. Nilijiona mjanja na kujiuliza nilichelewa wapi. Nikaanza hata kuwatongoza rafiki zake Linda(mke wangu) bila aibu.
Heshima niliyopewa na Linda ilinipa kiburi. Nikaanza kumuona bibi na kinyaa, ingawa hakuwa bibi. Nilihonga sana watoto wa mjini. Itoshe kusema kama starehe nilifanya mno na hela nilichezea sana.
Nakuja kuendelea, leo hii nimekumbuka mbali sana


Wengi humu JF mmekuwa mkinichukulia mtu asiyeeleweka na masikini mno. Hasa baada ya kusema nilikusanya 8000 kwa karibu miezi minne kwa kusave sehemu ya hela nilizopata(sio uongo ni kweli nili save na nauza karanga kwa sasa). Hiki ndicho kilichonitokea,,
Ngoja nianzie hapa:
Mwaka 2010 nilikutana na huyu Mzungu raia wa Sweden visiwani Zanzibar, yeye akiwa ni Mhandisi wa kampuni fulani ya simu HQ. Na alikuwa amekuja Zanzibar kutalii na kupumzika.
Tumuite Linda. Wakati Linda akiwa mapumzikoni Zanzibar, nilikuwa na rafiki yangu aliyeitwa Mick(sio jina halisi) na ndiye aliniunganisha na huyu Mzungu mara baada ya huyu dada kuvutiwa na mimi. Wakati huo nilikuwa nahudumu kama kibarua niliyelipwa kwa siku hapo hotelini.
Na tenda hii pia nilipewa na huyu huyu Mick. So ilikuwa rahisi kwa mimi kukutana na Linda mara kadhaa ingawa sikuwa najua kuwa alinipenda.
Tukaanzisha mahusiano ya mapenzi na kwa kweli kwao hela ilikuwepo. Baba yake mzazi alikuwa na jumba kubwa la kifahari Masaki. Naye alikuwa na pesa.
Nilibahatika kupata naye watoto wawili wa kiume wakati tulipohamia Sweden wote. Alinishughulikia kila kitu kuhusu nyaraka za kupata uraia halali wa Sweden.
Nilikuwa nakaa kule miezi hata miwili naruka nakuja TZ nakaa hata miezi 2 au zaidi na kurejea tena. Hela hizi mil 2 sijui 3 nilikuwa nazichezea mno na zilikuwa kama za mboga kwa wakati huo.
Mama yangu alikuwa akiishi dsm na alikuwa na shamba la hekari 1 Mkuranga. Linda alinitumia hela takribani 90M nakumbuka. Ilikuwa kwa ajili ya kumnunulia mama hekari zaidi ya 30 za mashamba huko Mkuranga na zingine nilimpa kwa matumizi yake. Pia Linda aliniambia nigawe kiasi ninunue pick up kwa ajili ya mama kwenda shambani.
Nikiri nilianza kuingiwa na roho ya usaliti ingawa huyu mama watoto wangu aliniheshimu na kunijali



alinyenyekea na hakuwahi kunikosea heshima hata siku moja.Nilianza kum cheat mara kadhaa ukizingatia nilishapata marafiki wengi, pindi nikija huku TZ ilikuwa ni kujirusha na starehe za anasa.
Nakumbuka nilikuwa naweka 1M juu ya meza bar nikiwa na rafiki zangu na kuwaambia 'hiyo hela iishe leo', na walishindwa kuimaliza mara kadhaa.
Niliota mapembe na sikusikia la kaka yangu wala nani. Nilijiona mjanja na kujiuliza nilichelewa wapi. Nikaanza hata kuwatongoza rafiki zake Linda(mke wangu) bila aibu.
Heshima niliyopewa na Linda ilinipa kiburi. Nikaanza kumuona bibi na kinyaa, ingawa hakuwa bibi. Nilihonga sana watoto wa mjini. Itoshe kusema kama starehe nilifanya mno na hela nilichezea sana.
Nakuja kuendelea, leo hii nimekumbuka mbali sana


