Ukishaoa ukitulize...sio uoe ubaki macho juu juu.....
Makundi na marafiki wa ajabu punguza na delete
Shikamana na mkeo mfikie ndoto zenu na kujenga familia bora
Hakikisheni nyumba yenu inatawala upendo, uvumilivu, kusameheana, kuheshimiana, kusaidiana, kuchukuliana, kuaminiana na mumtangilize Mungu kwenye kila jambo.....wanandoa msichoke kuombeana
Tabia ya kurudi usiku mwingi acha..... dharau na kauli mbovu zisiwepo....
Mwisho mke hapigwi ngumi.....anapigwa na Vanguard au Fortuner
hongera mkuu.. usibishane na mwanamke
januari 8 naingia katika ndoa panapo majaliwa nataka ushauri pamoja na nasaha.
Bali afanyeje?
Hongera sana kaka kwanza muheshimu mkeo pili kubaki njia kuu ndo mpango mzima ukichepuka tu. Utaona ndoa chungu.
Nategemea kadi Ya mwaliko Wa harusi yako ili nije nikushaur vizur.
hii si sehemu nzuri kuomba ushaur wa kuoa.....kama huamini subir
Nimelia kwa uchungu. Kuna mdogo wangu alimaliza elimu yake vizuri na kupata kazi katika moja ya taasisi nyeti Serikalini. Akaomba ushauri anataka kuoa, kaka zake tukamsihi umri ulikuwa bado avute subira ayajue mambo ya mabinti wa zama hizi za Wasapu na Ista. Alioa May mwaka huu na ndoa imevunjika November mwaka huu. Kisa ni vigisu za kwenye ndoa na nature ya kazi ya bwana mdogo. Ingia kwa akili sana mdogo wangu, otherwise Utatuletea kilio humu.
Je kama alimpata kwenye Pombe? Kuna mdada nliachana nae Sept nae anaolewa tar 8 ya kwako ni wapi mkuu ili nikupe ushauri vzr.
Una umri gani,?
Mkuu, mengi yamesemwa ila kumbuka wazazi wako pia walio kusaidia kukufikisha hapo ulipo.
Ndoa ni agano tafatifu, jaribu kuwa mtakatifu kabla ya kuingia huko.
Kila la kheri mkuuu...
Sawa mkuu usicheze mbali
Hahaha hahah usijali nitamtunza kwa uwezo wangu wote.usimpige wala kumtukana dada yetu. Tutahakikisha unaenda kunyea debe.
Ndoa raha sana,
Mkipendana kwa dhati,
Mkisikilizana,
Mkishauriana,
Mkijuana tabia,
Pendelea kusema ahsante hata akikubusu,
Ukiona hana raha mfariji na kama umemkosea wahi kusema samahani inayotoka ndani ya moyo wako,
Ndoa ni nzuri, coz ni maisha kama maisha uliyokua unaishi na dada au kaka zako,
Utani, ucheshi, kuelimishana, kuchokozana, kudekezana n.k
Kila la kheir katika safari yako ingine ya maisha.
By the way hakuna kadi ya mwaliko jamani.
Dah pole kwa mkasa uliokupata nategemea kwangu itakuwa tofauti Mungu anisaidie..