klorokwini
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 8,647
- 5,147
Kama gari si la kwako, vipi linakusumbuayou are the reason behind this, shairi lako 'from me to you' was my turning point, much respect
Vipi nipige mnada, kwa gari lisilo langu
Nilitaka tu kupanda, linifikishe mwenzangu
Kwa miguu sitakwenda, sitaki kizungu zungu
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada
vipi ningelijulia, kama ni gari makini
Waweza nisaidia, mwenzio sikubaini
Mafuta livujishiwa, sikuiona injini
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada
Kama gari si la kwako, vipi linakusumbua
Lirejeshe litokako , spea zako chukua
Gari hilo ni kituko, halifai kutumia
Tafuta lililo lako , ila hadhari chukua
Gari zima walijua , ufunguo ukitia
Mvumo huwa murua, gia laini kuingia
Resi ukikanyagia , moshi si wa kupalia
Oili kiangalia , ni nzito ilokozea.
Chungulia na mashine, uione gasketi
Zinavujisha nyengine , eneo lake la kati
Rejieta ni chengine, ujue halichemshi
Otaneta isiwe nene, ifiti na breketi
Ingia barabarani, lijaribu kwa safari
Anza spidi ya chini, kuiepuka hatari
Likanyage thamanini, ukiliona lishwari
Uzamie mvunguni , njiani likikuadhiri
Njiani likikuadhiri, uzamie mvunguni.
Kwanza urudi safari, ukatulie nyumbani
Ila ujue tayari , hilo gari si makini
Ni vyema ukaghairi, ukalitupa jaani
yangu macho , petrol 2100/litre
Kama gari si la kwako, vipi linakusumbua
Lirejeshe litokako , spea zako chukua
Gari hilo ni kituko, halifai kutumia
Tafuta lililo lako , ila hadhari chukua
Gari zima walijua , ufunguo ukitia
Mvumo huwa murua, gia laini kuingia
Resi ukikanyagia , moshi si wa kupalia
Oili kiangalia , ni nzito ilokozea.
Chungulia na mashine, uione gasketi
Zinavujisha nyengine , eneo lake la kati
Rejieta ni chengine, ujue halichemshi
Otaneta isiwe nene, ifiti na breketi
Ingia barabarani, lijaribu kwa safari
Anza spidi ya chini, kuiepuka hatari
Likanyage thamanini, ukiliona lishwari
Uzamie mvunguni , njiani likikuadhiri
Njiani likikuadhiri, uzamie mvunguni.
Kwanza urudi safari, ukatulie nyumbani
Ila ujue tayari , hilo gari si makini
Ni vyema ukaghairi, ukalitupa jaani
Big up kaka! nimeamini hata ije mseto, metakefini au fansida, klorokwini iko palepale :dance:
Much respect kwa huyu mtu he is in his own class, lakini ukumbuke ana twin brother wake Asprin ambaye nae pia ni mtaalam mkubwa wa hii fani
Big up kaka! nimeamini hata ije mseto, metakefini au fansida, klorokwini iko palepale :dance:
Gari usiangalie bodi ijaribu injini kaka, ni ngumu kupata gari mpya kwanza mimi sipendi hizo.
Kuna injini za kichina, unaangalia iko saaaaaafi, gari ipe miezi sita injini haifai, wachina wametuletea mambo
haya kaka nimekubali, Mimi nilikuwa naangalia muziki lakini wachina wametuwekea muziki mpaka kwenye bodaboda.. 'wabana pua kibao' usitafute spea usiku wafwa
Ulosema ni sawia, ya gari kujipatia
Hapa nina ridhia, nipate kusafiria
Ila hebu fikiria, ni mengi yamefojiwa
Hakuna gari jipya, mengi yameshatumika
Watuambia jipya, japani lishatumika
utajapatwa na haya, injini yachuruzika
Sisemi yote mabaya, ila mengi patashika
Hakuna gari jipya, mengi yameshatumika
Ukiliwasha lawaka, washukuru umepata
Ila haufiki mwaka, gari laleta matata
sasa ya nini mashaka, mwisho wake ni kudata
Hakuna gari jipya, mengi yameshatumika
Mchina kaleta mambo, injini kuchakachua
Nimechunguza kitambo, zitazame utajua
zimepoteza na umbo, na nyingi zinacheua
Hakuna gari jipya, mengi yameshatumika
Mkuu kloro unanikimbiza kweli, but it is good b'se that is how i'm going to grow
Mwenzenu nilitamani, gari kulisafiria
Laonyesha la thamani, kwa nje na ndani pia
Kiumbo li wastani, mfano wa gari KIA
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari hili lavutia, kwa hilo nakubalia
Rangi yake kahawia, machoni imetulia
Wengi wanaliwazia, na sifa kulisifia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kilitazama kwa mbele, pembeni limetanuka
Utapatwa na vipele, mwilini kusisimka
Natetemekwa vidole, nikipanda sita shuka
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kwa nyuma linapendeza, napenda wake mbinuko
Na mwendo likiongeza, lapepea kama puto
Ni kweli sijalikweza, gari hili moto moto
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Muda nilipo patia, gari hili nilipanda
Tena nikashikilia, katikati nikatanda
Kelele nilisikia, ila gari halikwenda
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari lilikakamaa, lilishindwa nifikisha
Pale nilipo tazama, mafuta linavujisha
Si kama nalisakama, mashineni kulitisha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Nimebaki na majuto, gari limekinaisha
Sina tena ule moto, wa gari kulipaisha
Mwili bado umzito, bora nisinge liwasha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Bora kupanda bajaji, popote wajipitia
Hazina mwingi mtaji, injini ni ndogo pia
Beteri ukisha chaji, wajitambia na njia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
KLORO na SPRINI, mwaonaje hii hoja
SHOSI naye WAKIJIJI, mchango wenu nangoja
MAGULU uko kundini, LIZZY pia tupamoja
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Na wote nisowataja, msiache kuchangia
Nipeni nyingi faraja, hoja sitapuuzia
Safari niloipanga, katu haikutimia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Malenga wenu
Sindano ya ganzi (Local anaesthesia)
Kutumika sio hoja , haya ni yangu mawazo
Kama kwako lina tija, sahau hao wa mwanzo
Na kama la reja reja, sisumbue akilizo
Jipya ukilingoja, labda la maigizo.
Hata kama metumika, muhimu lisiwe bovu
Kama safari wafika , pamoja na uchakavu
Ni vyema ukaridhika, dharura litakusevu
Dunia meharibika , mbovu zinaitwa mbivu
Hadaa ni nyingi sana, kwenye haya magari
Weka begani spana , kukagua kwa hadhari
Utaibiwa mchana , watu walivyo hodari
Toyota ya Dyna , eti nayo yaitwa Lori
Kama ni lgari la chama, wala halinisumbui
Njiani likisimama , boneti silifungui
Kama ni la kuazima, taukwepa uadui
Talirejesha salama, ila tena sichukui
hukunialika mimi kunako vitu hivi mkuu....
Poa mkuu wa ganzi, mimi mwenyewe nachomoka soonHahaha mkuu kloro nachapa usingizi nitarudi kesho tuendeleze hii mada