Najiandaa kwenda Kufanya Mtihani mchana na nimeambiwa hili Swali lipo hivyo naomba mnipe majibu ili nifaulu

Bila shaka ni ukweli usiopingika, wahitimu wengi wa vyuo afrika kwa ujumla magonjwa yafuatayo yanawatafuna;
1. Kukariri
2. Kusoma kwaajili ya kuajiriwa
3. Kusoma kwaajili ya kufaulu vyuoni
4. Ukimuuliza swali lolote la kada aliyosomea atakwambia hiyo atukufundishwa

Kuna mmoja kahitimu chuo cha NIT mechanical engineering, kuna mashine ndogo nlimuonyesha aitengeneze tupige pesa, alichonijibu nilisikitika sana eti anasema wamefundishwa kutengeneza mashine kubwa tuu.

Nkajiuliza kama mtu anashindwa kutengeneza mashine ambayo haizidi kilo mbili atawezaje kubuni au kutengeneza mashine inayozidi tani moja.

ELIMU YETU HAINA MSAADA
mtoa mada ni mmoja ya wasomi uliowaongelea hapo
 
Sisi tunasoma kwa sababu tumekuta watu wanasomaga tuuu! Tena tunakariri ili tu tushinde mitihani wala hatuhitaji kuelewa. Na ndio maana tuko tayari hata kuwaibia mitihani watoto wetu ili tu waonekane wameshinda na kufauli bila kujali nini kipo kwenye vichwa vyao! Utamanaduni wa vitabu tunauonaga tu kwenye movie.... wala hatunaga tabia ya kujisomea! Hata ukikuta kipande cha gazeti kimefungiwa bidhaa huna muda wa kudadisi kimeandikwa nini. Sie kwetu kusoma ni keroooo tena ni majanga!

Kuna mtu alisemaga sie tunajua kucheza ngoma tu! Kwakweli kusoma ingekuwa ngoma, mbona tungekuwa wa kwanza duniani! Angalia mitaala yetu ya elimu.... ipo ili tusindikize wanaosoma hadi vyuo vikuu.... haipo ili tuwe wasomi wenye uelewa.... ni kiasi cha kukamilisha vidato...

Bwana eeee.... nishachoka mie, si unajua elimu yetu hata kuandika para 3 tu sheeda! bila shaka utapata kanusu pointi hapa!
 
NUSU YA MAISHA YA MTANZANIA YANAISHIA DARASANI.....MPAKA UJE UFANIKIWE UZEE UNAPIGA HODI.... TUBADILI MIFUMO YA ELIMU LAIVYO TUTAISHIA KUJENGA MASHULE WAZUNGU WAJENGE VIWANDA.
 
Ni kweli mkuu, wahitimu wengi wa vyuo vikuu katika nchi za Africa huishia kufa masikini kutokana na kutokuwa na mfumo rafiki wa elimu ambao unaweza kumwandaa na kumjenga kijana tokea ngazi za awali.

Mifumo yetu ya elimu imejijenga katika kuwajanza wanafunzi hard disk zao kwa mambo mengi yasiyokuwa na msingi wala maana yoyote kwenye maisha yao. Chukulia masomo kama History yanafundishwa ili iweje?

Pia, kusoma bila focus nalo ni tatizo kubwa. Kwetu sisi wa Africa ni fahari zaidi kusoma na kumaliza madarasa lakini wenzetu huwa wana focus kwenye fani fulani na kubobea na pale anapohitimu mtu anakuwa na ujuzi wa hali ya juu na kuweza kujiajiri katika fani husika au hata kuajiriwa na kuleta mchango chanya.

Elimu ya nchi zilizoendelea imejikita zaidi kumpa uwezo mhitimu akimaliza masomo yake aweze kujiendeleza mwenyewe na ndio maana utaona wasomi wengi huweza kuanzisha makampuni yao kutokana na ubunifu walioupata kutoka kwenye vyuo.

Hata wale ambao hawakufanikiwa kumaliza shahada zao nao huwa tayari wana ujuzi mwingi kutokana na mfumo wa elimu kuwa rafiki toka ngazi za chini.

Mfano akina Zuckerberg, Bill Gate hawakufanikiwa kumaliza elimu zao za juu lakini walikuwa na uwezo na ubunifu wa kufanya mambo makubwa na kuwa ma CEO wakubwa duniani.

Naweza kuandika kitabu hapa lakini kufupisha tu nashauri serikali zetu kufanya ammendments katika sera za elimu na mifumo ya elimu ili ziweze kuendana na mabadiliko yaliyomo kwenye karne hii ya 21.

Mitaala mingi tunayotumia tumenakili kutoka kwa wenzetu ambao tayari walishaizika zamani kutokana na kukosa feasibility katika dunia ya sasa. Ubaya ni kuwa sisi bado tumeikumbatia na ndio chanzo cha kuzidi kuachwa na wenzetu ambao wanazidi ku advance kila siku na kufanya mambo ambayo kiakili za kibinadamu ni kama ndoto.. Refer Elon Musk (Space X and Mars Colonizatio e.t.c

Bila kuifumua mifumo ya elimu na serikali kuwekeza ziaidi kwenye sekta hiyo hakika hakuna jipya tutakaloliona.

Tuache kuwapa watahiniwa majibu ili tujisifie ufaulu. Ni upumbavu.
Utaanzia wapi kuifumua wakati wakoloni weusi wako kazini?
Tangu miaka ya 1978 watafiki wameongea jambo hili kwamba kumfundisha mtu kwa lugha asiyoielewa ni sawa na kumuandaa ashindwe kile anachofundishwa; lakini wameendelea na mfumo huo huo; kila mwaka wanadai ufahuru umeongezeka asilimia kadhaa; wakijua kabisa watanzania wengi hata hiyo hesabu ya asilimia hawaijui.
Kwa mwendo huu hatuchomoki ng'ooooooooooo
 
1. Nenda kwenye vilinge vya waganga wa kienyeji, wateja wengi Africa huku ni wasomi wasaka madaraka na utajiri.
2. Kuna nchi moja inaitwa Port Rico Profesa alilia asitumbuliwe eti ana familia inamtegemea na hana pakwenda.
3. Huko huko Africa tena kuna nchi inaitwa Porto Rico kuna Professa hana kazi anashinda kwenye ofisi za chama zilizopo sokoni.
4. Ni Africa pekee kwenye siasa utakuta wasomi weengi lakini utashangaa baaadhi ya vyuo havina malecturer.
5. Ni Africa pekee shule zina uhaba wa walimu lakini wahitimu wa vyuo vikuu hawana kazi..

6. Nitarudi baadaye.
 
1.Mitaala ya elimu ni kutoka ulaya (uingereza)
2. Nadharia
3. Uwezo wa wakufunzi
4. Siasa shule/ vyuo.
5. Miundo mbinu.
6. Ngono
 
Hii ni matokeo ya kuamini kupima uwezo wa mtu kupitia alichokipresent kwenye karatasi, pasipo kutumia njia sahihi ya kupima uwezo halisi wa mtu alionao. Hili si tatizo la Elimu kwa Afrika pekee bali dunia nzima, isipokuwa wenzetu wametuzidi katika kutambua uwezo halisi alionao mtu. Katika recruitment sisi tunaangalia unajua nini badala ya unaweza kufanya nini!

Nitakupa mfano wa kijana mmoja. Huyu kijana alisoma mwaka mmoja tu katika fani fulani ya uhandisi, alikuwa discontinued kutokana na kufeli. Lakini katika huo mwaka alipoenda field alijipenyeza katika kampuni hiyo hadi akabaki hapo, na watu wakampenda kutokana na uwezo wake wa kufanya kazi. Kampuni hiyo wakaamua kufanya recruitment, watu wakampenyeza hadi kwenye interview kuona kama anaweza kufanya lolote na kufikiriwa na watoa uamuzi. Kijana alifaulu vizuri interview kuliko walio na vyeti hata vya abroad. Lakini cha ajabu watoa uamuzi wamemdisqualify kwa sababu hana certifying papers. We don't recognize the real human potential. We measure people on memory basis. Hivyo tunapoteza vipaji vya kweli.

Changamoto kubwa katika usomi wetu Africa tunashindwa kutafsiri kile tulichokisoma darasani katika Ulimwengu halisi.
 
Hii ni matokeo ya kuamini kupima uwezo wa mtu kupitia alichokipresent kwenye karatasi, pasipo kutumia njia sahihi ya kupima uwezo halisi wa mtu alionao. Hili si tatizo la Elimu kwa Afrika pekee bali dunia nzima, isipokuwa wenzetu wametuzidi katika kutambua uwezo halisi alionao mtu. Katika recruitment sisi tunaangalia unajua nini badala ya unaweza kufanya nini!

Nitakupa mfano wa kijana mmoja. Huyu kijana alisoma mwaka mmoja tu katika fani fulani ya uhandisi, alikuwa discontinued kutokana na kufeli. Lakini katika huo mwaka alipoenda field alijipenyeza katika kampuni hiyo hadi akabaki hapo, na watu wakampenda kutokana na uwezo wake wa kufanya kazi. Kampuni hiyo wakaamua kufanya recruitment, watu wakampenyeza hadi kwenye interview kuona kama anaweza kufanya lolote na kufikiriwa na watoa uamuzi. Kijana alifaulu vizuri interview kuliko walio na vyeti hata vya abroad. Lakini cha ajabu watoa uamuzi wamemdisqualify kwa sababu hana certifying papers. We don't recognize the real human potential. We measure people on memory basis. Hivyo tunapoteza vipaji vya kweli.

Changamoto kubwa katika usomi wetu Africa tunashindwa kutafsiri kile tulichokisoma darasani katika Ulimwengu halisi.
Dah noma sana ndomana hata asiesomea hiyo fani akitafuta cheti basi kamaliza hata kama ajajifunza kitu atajulia humo humo kazini inauma sana unaweza kuta alopewa hiyo kazi cheti cha kufoji sio cha ukweli.
 
Mkuu nisamehe maana sikuuona uzi wako mapema. Muda huu nadhani umeshamaliza kujibu.

Ni matumaini yangu kuwa utapata marks za kutosha kama mimi nilivyopata baada ya kulijibu swali hili hili mwaka 2015.

Sa hivi namiliki viwanda vya kuiongeza dunia kadiri ya maagizo ya Muumbaji.
 
Ubovu wa mitaala na mengineyo kama.
1) Nasoma tu ila siipendi hii fani
2) Maeneo mengi yenye resource yametegwa kwa ajili ya hifadhi wasomi mfano sekta ya madini inabidi wawe wapole
3) sera za ukale kwa wenye mamlaka
4) Kupoteza mda mrefu class na kamda kiduchu field
 
Kama wewe ni muelewa tayari majibu yapo hapo juu kwenye hizo comments...... No kuzikusanya tu......
 
Back
Top Bottom