Najiandaa kugombea urais 2030

Onambali

Member
Mar 11, 2011
67
10
WanaJf,

Kwanza nawasalimu.

Naomba maoni yenu katika kusudi langu la kutaka kuwa rais wa Tz mwaka 2030 kama Mungu akinipa uhai.

Ninachotarajia kufanya nitakapopata uraisi ni pamoja na:

1. Kuvunja mpango wa muda mrefu wa wazungu (walioanzisha pale Berlin mwaka 1884) ambao hadi sasa unatawala kifkra za mwafrika na kufanya vipaji na mazuri ya muafrika kutoendelezwa. Natarajia kuongoza Taifa letu lijenge watu huru wanaojiamini na kufurahia utaifa wao.

2. Kuweka mpango wa muda wa miaka 500 wa Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo mfano miundombinu, kilimo na ufugaji, utunzaji wa maji ambayo yanaendelea kutoweka kutoka katika vyanzo vyetu vya maji, elimu itakayoongozwa na utashi na vitendo, afya, makazi na mipango miji itakayo kidhi haja ya miaka hiyo 500 mbeleni (sio kujenga na kubomoa bomoa kama ilivyo sasa), kutunza na kuhifadhi mbuga zetu za wanyama ili kutufaidisha sisi na vizazi vijavyo, kuanzisha mtindo wa kujengea wananchi makazi bora, kutunza na kuendeleza fukwe zetu za bahari na maziwa ili kuimarisha utalii, na mengineyo kama nitakavyoshauriwa na wanachi.

3. Kuondoa utegemezi wa misaada kutoka nje ya chi kwa maana ya kutumia kwa uangalifu pato letu la Taifa kwa kuondoa matumizi ya yasiyo ya lazima mfano magari ya kifahari serekalini, kuziba mianya yote ya rushwa kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali za walio-wanaona watakaotuibia na kuwasweka gerezani.

4. Kutoa heshima inayostahili kwa wataalamu wetu ikiwa ni pamoja na kuwalipa mishara mizuri itakayowafaya wasiondoke nchini, pia kuwawezesha kutumia taaluma zao katika kujenga nchi badala ya kuleta wataalamu kutoka nje.

5. Kuwalinda, kuwapenda, kuwaheshimu na kuwakuza katika maadili mema watoto wetu ili waipende nchi yao na kufurahi kuzaliwa Tanzania

6. Kuwa mtumishi wa wanachi na sio kuwa mtawala wa wanachi

7. Kuwa msikivu na mtendaji wa matokeo ya tafiti za wataalamu wetu katika kuijenga nchi yetu


Hitimisho

Taaluma mbalimbali zinazotolewa Tz hazijaweza kumfanya mtanzania (kwa wastani) akomboke kutoka kwenye umaskini wa akili na ushirikina. Nafahamu miaka 19 ijayo ni mingi na mambo mengi yatakuwa yamebadilika ila ni vizuri nijinoe kuanzia sasa. Moyoni mwangu nina nia njema kabisa ya kuongoza taifa letu katika kuweka na kuanza kuainisha jinsi ya kufikia malengo ya miaka 500 ijayo.

NB. Mimi ni mwananchi wa kawaida na sijawa mwanachama wa chama chochote cha siasa.

Ee Mwenyezi Mungu naomba uibariki nchi yetu Tanzania.
 
dah!!! safari njema mkuu!! .. endelea kutupa updates ...
 
sio kila cku 2naingia net,kwahiyo jina hili ndilo utakalolitumia kuombe kura? Ili 2kiliona jina hili tukupe na wewe KULA!
 
Kweli mwisho wa dunia umewadia, naona watu mmeanza KUNENA KWA LUGHA.

Lugha zenyewe wanazonenea ni za roho anayetoka kuzimu lakini wanatenda miujiza. Kweli mwisho wa dunia unakaribia. Gamba Jipya sikuzingine unaamka umelivua kabisa gamba la zamani kama leo hii.
 
Gamba Jipya na Lincolinmtz,

Wakati mwingine mkikosa cha kusema katika thread zinazotolewa hapa jamvini nyamazeni
 
Hapana mkuu, hapa natumia nickname. Nalitumia kama wasifu wa mtazamo nilionao

Pia wewe washawasha, acha kufikiri nataka kula, fikiria mbali acha kuwa na mawazo hayo. Angalia hoja zangu nilizotuma kama zinafaa au la. Usiochukulie kila kitu kirahisirahisi na kishabiki. Tulia na angalia mambo ya msingi
 
WanaJf,

Kwanza nawasalimu.

Naomba maoni yenu katika kusudi langu la kutaka kuwa rais wa Tz mwaka 2030 kama Mungu akinipa uhai.

Ninachotarajia kufanya nitakapopata uraisi ni pamoja na:

1. Kuvunja mpango wa muda mrefu wa wazungu (walioanzisha pale Berlin mwaka 1884) ambao hadi sasa unatawala kifkra za mwafrika na kufanya vipaji na mazuri ya muafrika kutoendelezwa. Natarajia kuongoza Taifa letu lijenge watu huru wanaojiamini na kufurahia utaifa wao.

2. Kuweka mpango wa muda wa miaka 500 wa Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo mfano miundombinu, kilimo na ufugaji, utunzaji wa maji ambayo yanaendelea kutoweka kutoka katika vyanzo vyetu vya maji, elimu itakayoongozwa na utashi na vitendo, afya, makazi na mipango miji itakayo kidhi haja ya miaka hiyo 500 mbeleni (sio kujenga na kubomoa bomoa kama ilivyo sasa), kutunza na kuhifadhi mbuga zetu za wanyama ili kutufaidisha sisi na vizazi vijavyo, kuanzisha mtindo wa kujengea wananchi makazi bora, kutunza na kuendeleza fukwe zetu za bahari na maziwa ili kuimarisha utalii, na mengineyo kama nitakavyoshauriwa na wanachi.

3. Kuondoa utegemezi wa misaada kutoka nje ya chi kwa maana ya kutumia kwa uangalifu pato letu la Taifa kwa kuondoa matumizi ya yasiyo ya lazima mfano magari ya kifahari serekalini, kuziba mianya yote ya rushwa kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali za walio-wanaona watakaotuibia na kuwasweka gerezani.

4. Kutoa heshima inayostahili kwa wataalamu wetu ikiwa ni pamoja na kuwalipa mishara mizuri itakayowafaya wasiondoke nchini, pia kuwawezesha kutumia taaluma zao katika kujenga nchi badala ya kuleta wataalamu kutoka nje.

5. Kuwalinda, kuwapenda, kuwaheshimu na kuwakuza katika maadili mema watoto wetu ili waipende nchi yao na kufurahi kuzaliwa Tanzania

6. Kuwa mtumishi wa wanachi na sio kuwa mtawala wa wanachi

7. Kuwa msikivu na mtendaji wa matokeo ya tafiti za wataalamu wetu katika kuijenga nchi yetu


Hitimisho

Taaluma mbalimbali zinazotolewa Tz hazijaweza kumfanya mtanzania (kwa wastani) akomboke kutoka kwenye umaskini wa akili na ushirikina. Nafahamu miaka 19 ijayo ni mingi na mambo mengi yatakuwa yamebadilika ila ni vizuri nijinoe kuanzia sasa. Moyoni mwangu nina nia njema kabisa ya kuongoza taifa letu katika kuweka na kuanza kuainisha jinsi ya kufikia malengo ya miaka 500 ijayo.

NB. Mimi ni mwananchi wa kawaida na sijawa mwanachama wa chama chochote cha siasa.

Ee Mwenyezi Mungu naomba uibariki nchi yetu Tanzania.

Onambali kweli unaona mbali sana. 500 years! Safi sana. Kuliko wanaoangalia ahadi za uchaguzi unaofuata. Pia umeongea mambo ya msingi sana: (1) Umuhimu wa kujitambua na kukuza uzalendo (2) Umuhimu wa kuthamini watoto na kuwajenga kuwa raia wa maana kwa nchi yao na dunia (3)Umuhimu wa elimu na kuthamini wataalamu na utafiti (4) Umuhimu wa uongozi bora, kwamba wewe utakuwa mtumishi wa watu na si vinginevyo. Kila lakheri.
 
Onambali kweli unaona mbali sana. 500 years! Safi sana. Kuliko wanaoangalia ahadi za uchaguzi unaofuata. Pia umeongea mambo ya msingi sana: (1) Umuhimu wa kujitambua na kukuza uzalendo (2) Umuhimu wa kuthamini watoto na kuwajenga kuwa raia wa maana kwa nchi yao na dunia (3)Umuhimu wa elimu na kuthamini wataalamu na utafiti (4) Umuhimu wa uongozi bora, kwamba wewe utakuwa mtumishi wa watu na si vinginevyo. Kila lakheri.

Nashukuru sana.

Naamini itawezekana
 
Gamba Jipya na Lincolinmtz,

Wakati mwingine mkikosa cha kusema katika thread zinazotolewa hapa jamvini nyamazeni

Mkuu uvumilivu wa siasa utauweza kweli, kubali kutokukubaliana ndiyo demokrasia.

If we all think alike, the someone's not thinking at all.
 
WanaJf,

Kwanza nawasalimu.

Naomba maoni yenu katika kusudi langu la kutaka kuwa rais wa Tz mwaka 2030 kama Mungu akinipa uhai.

Ninachotarajia kufanya nitakapopata uraisi ni pamoja na:

1. Kuvunja mpango wa muda mrefu wa wazungu (walioanzisha pale Berlin mwaka 1884) ambao hadi sasa unatawala kifkra za mwafrika na kufanya vipaji na mazuri ya muafrika kutoendelezwa. Natarajia kuongoza Taifa letu lijenge watu huru wanaojiamini na kufurahia utaifa wao.

2. Kuweka mpango wa muda wa miaka 500 wa Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo mfano miundombinu, kilimo na ufugaji, utunzaji wa maji ambayo yanaendelea kutoweka kutoka katika vyanzo vyetu vya maji, elimu itakayoongozwa na utashi na vitendo, afya, makazi na mipango miji itakayo kidhi haja ya miaka hiyo 500 mbeleni (sio kujenga na kubomoa bomoa kama ilivyo sasa), kutunza na kuhifadhi mbuga zetu za wanyama ili kutufaidisha sisi na vizazi vijavyo, kuanzisha mtindo wa kujengea wananchi makazi bora, kutunza na kuendeleza fukwe zetu za bahari na maziwa ili kuimarisha utalii, na mengineyo kama nitakavyoshauriwa na wanachi.

3. Kuondoa utegemezi wa misaada kutoka nje ya chi kwa maana ya kutumia kwa uangalifu pato letu la Taifa kwa kuondoa matumizi ya yasiyo ya lazima mfano magari ya kifahari serekalini, kuziba mianya yote ya rushwa kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali za walio-wanaona watakaotuibia na kuwasweka gerezani.

4. Kutoa heshima inayostahili kwa wataalamu wetu ikiwa ni pamoja na kuwalipa mishara mizuri itakayowafaya wasiondoke nchini, pia kuwawezesha kutumia taaluma zao katika kujenga nchi badala ya kuleta wataalamu kutoka nje.

5. Kuwalinda, kuwapenda, kuwaheshimu na kuwakuza katika maadili mema watoto wetu ili waipende nchi yao na kufurahi kuzaliwa Tanzania

6. Kuwa mtumishi wa wanachi na sio kuwa mtawala wa wanachi

7. Kuwa msikivu na mtendaji wa matokeo ya tafiti za wataalamu wetu katika kuijenga nchi yetu


Hitimisho

Taaluma mbalimbali zinazotolewa Tz hazijaweza kumfanya mtanzania (kwa wastani) akomboke kutoka kwenye umaskini wa akili na ushirikina. Nafahamu miaka 19 ijayo ni mingi na mambo mengi yatakuwa yamebadilika ila ni vizuri nijinoe kuanzia sasa. Moyoni mwangu nina nia njema kabisa ya kuongoza taifa letu katika kuweka na kuanza kuainisha jinsi ya kufikia malengo ya miaka 500 ijayo.

NB. Mimi ni mwananchi wa kawaida na sijawa mwanachama wa chama chochote cha siasa.

Ee Mwenyezi Mungu naomba uibariki nchi yetu Tanzania.

Hizo ndoto zako zitakufanya uvuliwe gamba hivi karibuni! Wote wenye ndoto kama za kwako na kuzionyesha waziwazi kiboko yao ni kuvuliwa gamba tu!
 
Back
Top Bottom