WA-UKENYENGE
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 2,918
- 1,233
Mkuu unaona eee! Yaani nilishaliona nikuamua tu kuweka ubabe chini na kuridhika huku ukimtunza vizuri na kumwelewesha vizuri uliyenaye!! Hakuna kitu kizuri kama kumtoa ushamba uliyenaye na hatimaye akaja kuwa msaada kwako, you must be proud and respect one another. Huyu mkuu amepost lakini hajasema ni kitu gani kinachomfanya asimpende, pengine ni ule ushamba wa kijijini ambapo wakati mwingine mke wake mpendwa anayaacha nje manyonyo bila kuyasitili au anakuwa mchafu mchafu kiaina huku yeye mwenyewe haionyeshi kukereka. Kama anasoma huu uzi wake, ajitahidi kumuweka sawa huku akinunulia vitu vikali na kumpa outing za nguvu kila weekend akimuonyesha wanawake wengine wanaonekanaje!!wa ukenyege unajua hawa vijana kabla ya kuoa huwa kunakuwa na expectation sasa wakizikosa wanaanza kulalamika.no perfect marriage in this world.
Hapo ndo nahisi msingi wa tatizo ulipo!! Huyu jama ningepata bahati ya kukutana asijaribu kumuacha!! May be he is still too young kiasi kwamba kauzoefu kamahusiano kanamsumbua!!Mkuu nafikiri tatizo lako umeanza kufanya compare and contrast.itakusumbua sana hiyo attitude uliyoitengeneza kichwani mwako baada ya kutoka chuo.ila waulize kwanza wenye wake walioenda shule na mkwanja na stutus yao iko juu wakuambie.inshort kuna watu wanatamani miaka irudi nyuma akajiolee kabint ka kijijini awe anakaa nyumbani na kumlelea wanae tu kutokana na maisha ya ndoa anayoishi. ninachoweza kukushauri ni kuwa jitahidi kumweka mwenzio hiyo level unayofikiri kwako ndio sahihi na ndio kigezo cha mwanamke unayemwazia kwa sasa.
Wewe ni mtu wa ajabu sana uliamua kuishi kwa kuogopa wana kijiji.
Me naona humtendei haki huyo dada sababu ungesema mapema.
Unasikitisha sana hadi mtu una zaa nae ulitegemea nini sasa,
mkuu, umeshawahi kusoma kitabu cha 'song of Lawino song of Ocol'?
Piga chini mkuu....kumbuka ndoa ni for life mkuu,huwezi kukaa na mtu ambaye moyo hauridhiki for the rest of your life.....inauma na huwezi kumweleza mtu akakubali,lakini kuzidi kuchelewa unaongeza tatizo....BWANA NDOA NI KTU KINGINE...UNATAKIWA UWE 100% SATISFIED KABLA HUJAMUOA MTU....ASIKUDANGANYE MTU!!!
mkuu majany uje upate kinywaji. Nakuunga mkono. Kweli linapofika suala la ndoa inabidi uridhike na huyo mtu kwanza. Mshkaji inawezekana alipofika chuo akaanza mambo mengi, kurudi bush anamuona wake yupo tofauti na wale wa chuo. Kama anaweza jifunza kumpenda tena ni bora afanye hivyo otherwise apige chini fasta.
Habari ndg zangu wadau wa JF, ndg zangu ni takribani miaka miwili ss naishi na mwanamke ambae nilizaa nae tangu mwaka 2006 kabla sijajiunga na chuo kikuu, baada ya kumpa ujauzito niliamua kumtolea barua ya posa kipindi kiukweli nilikuwa nampenda kwa kiasi fulani nikiwa na imani kuwa nitaishi nae km mume na mke hapo baadae. Wakati mwenzangu alikuwa ameshaacha shule baada ya kufeli mtihani wa kidato cha pili na tayari nilikuwa nimemaliza kidato cha sita. Hatimaye 2007 nilifanikiwa kujiunga UDSM na muda wote wa masomo yangu sijahi kufikiria kuachana na huyu msichana kabisa. Lkn baada ya kuhimu chuo na kuja kuonana nae huko kijijini nilikomwacha ktk maongezi ndani ya siku kadhaa nikaanza kugundua nilifanya makosa sana kumkeep hasa baada ya kugundua kuwa ana mapungufu mengi ambayo pengine hayawezi kulekebishika kabisa kiasi cha kunifanya niendelee kuamini kuwa lilikuwa chaguo sahihi kwangu. Hata hivyo nililazimika kumchukua na kuishi nae mjini baada ya kugundua wanakijiji walishaanza kuwa na mtazamo hasi kwangu, hivyo nikamchua ili kuwaridhisha wanajamii. Vibaya zaidi nazidi kuyaona mapungufu zaidi na zaidi, kiasi cha kunifanya nisiwe na furaha ya kuendelea kuishi nae na mara nyingine najikuta namfanyia vituko vya kukosa upendo kabisa kwake. Kumrudisha naona noma kwani km mjuavyo watu watasema coz tumepishana elimu kiasi kikubwa. Naishi nae simpendi kutoka moyoni. Wadau naomba ushauri kwani hili ni suala zito sana kwangu sijafunga nae ndoa.................
hahahaaaaa...CAtherine ntapitia bwana...niandalie ndovu bariiiidiiiiiii...lakini ukweli ndio huo.....