Naishi na mke ambaye sina mapenzi nae nifanyeje?

USHOROBA

Member
Jul 22, 2012
5
0
Habari ndg zangu wadau wa JF, ndg zangu ni takribani miaka miwili ss naishi na mwanamke ambae nilizaa nae tangu mwaka 2006 kabla sijajiunga na chuo kikuu, baada ya kumpa ujauzito niliamua kumtolea barua ya posa kipindi kiukweli nilikuwa nampenda kwa kiasi fulani nikiwa na imani kuwa nitaishi nae km mume na mke hapo baadae. Wakati mwenzangu alikuwa ameshaacha shule baada ya kufeli mtihani wa kidato cha pili na tayari nilikuwa nimemaliza kidato cha sita. Hatimaye 2007 nilifanikiwa kujiunga UDSM na muda wote wa masomo yangu sijahi kufikiria kuachana na huyu msichana kabisa. Lkn baada ya kuhimu chuo na kuja kuonana nae huko kijijini nilikomwacha ktk maongezi ndani ya siku kadhaa nikaanza kugundua nilifanya makosa sana kumkeep hasa baada ya kugundua kuwa ana mapungufu mengi ambayo pengine hayawezi kulekebishika kabisa kiasi cha kunifanya niendelee kuamini kuwa lilikuwa chaguo sahihi kwangu. Hata hivyo nililazimika kumchukua na kuishi nae mjini baada ya kugundua wanakijiji walishaanza kuwa na mtazamo hasi kwangu, hivyo nikamchua ili kuwaridhisha wanajamii. Vibaya zaidi nazidi kuyaona mapungufu zaidi na zaidi, kiasi cha kunifanya nisiwe na furaha ya kuendelea kuishi nae na mara nyingine najikuta namfanyia vituko vya kukosa upendo kabisa kwake. Kumrudisha naona noma kwani km mjuavyo watu watasema coz tumepishana elimu kiasi kikubwa. Naishi nae simpendi kutoka moyoni. Wadau naomba ushauri kwani hili ni suala zito sana kwangu sijafunga nae ndoa.................
 
Mkuu, au ww ndo ulimwachisha shule? Kama kweli, dhambi itakukaa maisha. Kama sivyo, fanya tu namna ya kuachana naye lest akakuzalia tena. By the way, tunda mwala??
 
Tutakushauri nn ndugu yangu uamuzi unao mwenyewe kumbuka una mtoto naye huwezi kumwacha funga naye ndoa to..
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana uliamua kuishi kwa kuogopa wana kijiji.

Me naona humtendei haki huyo dada sababu ungesema mapema.

Unasikitisha sana hadi mtu una zaa nae ulitegemea nini sasa,
 
namuonea huruma sana huyo binti mana hajui ukiwazacho akilini mwako umtizamapo......
yani hapo najua manatofautiana hadi na uwezo wa kufikiri,kuwazua na kutatua mambo....pole kwa hilo ila huwezi kujilazimisha sana muhimu muambie ukweli na usizidi kum use zaidi........na fata ushauri wa THE BOSS hapo juu
 
alaaaa!,basi ww sio msomi,tumia elimu yako kumshape,mbona cmple tu,kwani ww unashindwana nae wapi?
 
Golden Rule:-
'To be happy with a man, love him little and understand him a lot.To be happy with a woman,love her a LOT and DO NOT TRY to understand her :)" sasa inaonekana we upendo hakuna na unakazana kumuelewa zaid pole, kazi unayo kaka, hawakukosea waliosema A good marriage would be between a Blind wife and a deaf husband.
 
Elimu yako ndo imekufanya umuone hafai. Ila watu huwa mnakimbilia sana kuoa,form six unatoa posa?
La muhimu usiangalie watt, angalia maisha yako. Watu husema kila kitu, jema na baya.
 
Habari ndg zangu wadau wa JF, ndg zangu ni takribani miaka miwili ss naishi na mwanamke ambae nilizaa nae tangu mwaka 2006 kabla sijajiunga na chuo kikuu, baada ya kumpa ujauzito niliamua kumtolea barua ya posa kipindi kiukweli nilikuwa nampenda kwa kiasi fulani nikiwa na imani kuwa nitaishi nae km mume na mke hapo baadae. Wakati mwenzangu alikuwa ameshaacha shule baada ya kufeli mtihani wa kidato cha pili na tayari nilikuwa nimemaliza kidato cha sita. Hatimaye 2007 nilifanikiwa kujiunga UDSM na muda wote wa masomo yangu sijahi kufikiria kuachana na huyu msichana kabisa. Lkn baada ya kuhimu chuo na kuja kuonana nae huko kijijini nilikomwacha ktk maongezi ndani ya siku kadhaa nikaanza kugundua nilifanya makosa sana kumkeep hasa baada ya kugundua kuwa ana mapungufu mengi ambayo pengine hayawezi kulekebishika kabisa kiasi cha kunifanya niendelee kuamini kuwa lilikuwa chaguo sahihi kwangu. Hata hivyo nililazimika kumchukua na kuishi nae mjini baada ya kugundua wanakijiji walishaanza kuwa na mtazamo hasi kwangu, hivyo nikamchua ili kuwaridhisha wanajamii. Vibaya zaidi nazidi kuyaona mapungufu zaidi na zaidi, kiasi cha kunifanya nisiwe na furaha ya kuendelea kuishi nae na mara nyingine najikuta namfanyia vituko vya kukosa upendo kabisa kwake. Kumrudisha naona noma kwani km mjuavyo watu watasema coz tumepishana elimu kiasi kikubwa. Naishi nae simpendi kutoka moyoni. Wadau naomba ushauri kwani hili ni suala zito sana kwangu sijafunga nae ndoa.................

Ulikuwa unampenda sio......? halafu nani alisema upendo wa mume na mke huendelea automatically hata baada ya kuoana? Kama kuna mtu atasema mambo yake yamemnyookea kwenye ndoa bila matatizo huyo ni mwongo kabisa. Na tunaona wanalia humu na wengine wanabaki na maumivu yao na wengine wanapona na maisha yanaendelea.

Kuna mapungufu uliyaona ndio...mbona huyasemi? kama ni mwaminifu kwako ila tu hawezi kupika vizuri, kuongea kisomi kama wewe, kuishi kama wanawake wa mjini uliowazoea kwa nini usim-shape..............Au ulitegemea mwanamke unaemuota kwenye kichwa chako? Ambaye pengine hawezi ku-exist?

Nimeuliza maswali mengi ili mleta thread aweze kufanya maamuzi sahihi, majibu ya haraka kwenye situation kama hii hayawezi kumsaidia mleta uzi sanasana yanaishia kumuumiza huyo mwenzi wake. Hebu mlio-side naye The Boss, nimeona like ya nyumba kubwa n.k msaidie hii zahma.
 
Last edited by a moderator:
Man i can feel you ... inatokea sana hiyo mwanzoni watu mnakuwa na mapenzi mipango mingi alafu baadaye one side inaanza kupoteza mapenzi etcl ... mi nakushauri tafuta umpedaye kwa dhati ila usikimbie majukumu ya kutunza mtoto .. nakumbuka mzee wangu aliwahi kunambia usijaribu ku promise future mwanamke ambaye ni wapenzi tu badi mnasomana tabia.

mwisho - Acha uzinzi...
 
Hayo mapungufu hayawezi kubadilishwa mpe muda wa kujirekebisha kama itashindikana bora tu muachane. Endelea kutunza mtoto maana kuishi pamoja ni kupotezeana majira, hii kitu ni mbaya sana.
 
Back
Top Bottom