Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,504
- 28,694
Imeandikwa sehemu gani kwamba vitu vya ufunuo viuzwe?
Ninachofahamu mimi ni kuwa mafuta yalitumiwa na manabii na makuhani, kwa ajili ya kazi maalum tu, haikuwa kuyauza wala kuyatangaza kama biashara hapo ni kinyume kabisa na maandiko.
Sasa watumishi wa leo wamegeuza hiyo huduma ni biashara kitu ambacho si sahihi kabisa; Na mkumbuke kitu cha ufunuo kinatumika kwa muda maalum na kwa wakati maalum, na siyo kwa kila mtu, na si kila mahali, angalia Yesu alipomwambia yule kipofu apake matope kwenye macho, hakufanya hivyo kwa kila kipofu, wengine aliwashika macho tu, wengine alitamka tu wakapona.
Tusemeje kwa Nabii Elisha kila mwenye ukoma angemwambia aende Yordan akajichovye mara 7, maana hata hivyo, kulikuwa na wakoma wengi katika Israeli zama hizo wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu pekee. [Luka 4:27].” Na wala Elisha hakuchukua malipo ya pesa, na mtumwa wake aliyemzunguka Elisha na kuchukua hizo pesa, alipatwa na ukoma. Basi tungetegemea manabii watumie hiyo kanuni ya kuchovya watu kwenye maji wapone ukoma, lakini hilo hatulioni zaidi ya kuona mafunuo mengine ya uponyaji.
Lakini kinachoshangaza watumishi wa leo wamegeuza hivyo vitu vya kimafunuo kama biashara, na mbaya zaidi wanauza, Mungu akikupa kitu kwa mafunuo ukitumie kumponya mtu huwezi kukiuza, na huwezi kulinganisha eti mbona Biblia inauzwa, biblia ni kitabu kimepitia hatua nyingi sana mpaka kuandikwa, na wamishionari walio leta injili Africa enzi hizo walikuwa wanagawa bure, hata leo maeneo ambayo injili haijawafikia watu Biblia inagawiwa bure mfano huko Korea Kaskazini na China na sehemu mbalimbali za dunia. Hata mimi mda mwingine nagawa Biblia bure sehemu zile ambazo Injili haijafika na kwa baadhi ya watu wasio na uwezo wa kununua na wengine nawapa kama zawadi. Mtume Paulo anasema hivi,
“Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila GHARAMA, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili. [1 Wakorintho 9:18].”
NITAITOA INJILI BILA GHARAMA: Huu msingi Mtume Paulo alipokea kutoka kwa Bwana, kuwa, “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; MMEPATA BURE, TOENI BURE. [Mathayo 10:8].”
Hivyo wanajitetea ya kwamba, sasa bila kufanya hivyo hatutaweza kulipa umeme, kununua vyombo, kulipia kumbi na mavitu mengi. Rafiki kwani Luku/stima mnalipia bei gani? Maana tunaona ibada ya wazi mnafanya jumapili tu tena kwenye uwanja wa wazi, na hivyo vyombo vya muziki mnavinunua kila siku?. Kwahiyo mnauza mafuta, maji, chumvi kwa vigezo hivyo? Kama ndicho kigezo nawaambia iliyo kweli acheni uongo, semeni tu mnapiga dili la upako. Kwani hamna matolea na sadaka, mbona waumini wanatoa sadaka na zaka! Au hazitoshi mpaka uanze kuuza na chumvi na mafuta?
Halafu ni wewe tu ndio unapokea, na kudai ni huduma yako isiyo na kamati ya fedha, isiyohojiwa. Wenzenu wa zama za Yesu walikuwa wanauza Njiwa za upako hekaluni, Walifukuzwa na Yesu na meza zao kupinduliwa na kukemewa kwamba,
“Je! Haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. [Marko 11:17].”
Hukumu ya Mungu itakuwa juu yenu enyi wapotoshaji. Imeandikwa kwamba,
“Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini. [Marko 9:42].”
Mungu akufumbue macho utambue upo wakati gani na nini sasa unachopaswa kufanya kwa habari ya wokovu wako.
Ninachofahamu mimi ni kuwa mafuta yalitumiwa na manabii na makuhani, kwa ajili ya kazi maalum tu, haikuwa kuyauza wala kuyatangaza kama biashara hapo ni kinyume kabisa na maandiko.
Sasa watumishi wa leo wamegeuza hiyo huduma ni biashara kitu ambacho si sahihi kabisa; Na mkumbuke kitu cha ufunuo kinatumika kwa muda maalum na kwa wakati maalum, na siyo kwa kila mtu, na si kila mahali, angalia Yesu alipomwambia yule kipofu apake matope kwenye macho, hakufanya hivyo kwa kila kipofu, wengine aliwashika macho tu, wengine alitamka tu wakapona.
Tusemeje kwa Nabii Elisha kila mwenye ukoma angemwambia aende Yordan akajichovye mara 7, maana hata hivyo, kulikuwa na wakoma wengi katika Israeli zama hizo wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu pekee. [Luka 4:27].” Na wala Elisha hakuchukua malipo ya pesa, na mtumwa wake aliyemzunguka Elisha na kuchukua hizo pesa, alipatwa na ukoma. Basi tungetegemea manabii watumie hiyo kanuni ya kuchovya watu kwenye maji wapone ukoma, lakini hilo hatulioni zaidi ya kuona mafunuo mengine ya uponyaji.
Lakini kinachoshangaza watumishi wa leo wamegeuza hivyo vitu vya kimafunuo kama biashara, na mbaya zaidi wanauza, Mungu akikupa kitu kwa mafunuo ukitumie kumponya mtu huwezi kukiuza, na huwezi kulinganisha eti mbona Biblia inauzwa, biblia ni kitabu kimepitia hatua nyingi sana mpaka kuandikwa, na wamishionari walio leta injili Africa enzi hizo walikuwa wanagawa bure, hata leo maeneo ambayo injili haijawafikia watu Biblia inagawiwa bure mfano huko Korea Kaskazini na China na sehemu mbalimbali za dunia. Hata mimi mda mwingine nagawa Biblia bure sehemu zile ambazo Injili haijafika na kwa baadhi ya watu wasio na uwezo wa kununua na wengine nawapa kama zawadi. Mtume Paulo anasema hivi,
“Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila GHARAMA, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili. [1 Wakorintho 9:18].”
NITAITOA INJILI BILA GHARAMA: Huu msingi Mtume Paulo alipokea kutoka kwa Bwana, kuwa, “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; MMEPATA BURE, TOENI BURE. [Mathayo 10:8].”
Hivyo wanajitetea ya kwamba, sasa bila kufanya hivyo hatutaweza kulipa umeme, kununua vyombo, kulipia kumbi na mavitu mengi. Rafiki kwani Luku/stima mnalipia bei gani? Maana tunaona ibada ya wazi mnafanya jumapili tu tena kwenye uwanja wa wazi, na hivyo vyombo vya muziki mnavinunua kila siku?. Kwahiyo mnauza mafuta, maji, chumvi kwa vigezo hivyo? Kama ndicho kigezo nawaambia iliyo kweli acheni uongo, semeni tu mnapiga dili la upako. Kwani hamna matolea na sadaka, mbona waumini wanatoa sadaka na zaka! Au hazitoshi mpaka uanze kuuza na chumvi na mafuta?
Halafu ni wewe tu ndio unapokea, na kudai ni huduma yako isiyo na kamati ya fedha, isiyohojiwa. Wenzenu wa zama za Yesu walikuwa wanauza Njiwa za upako hekaluni, Walifukuzwa na Yesu na meza zao kupinduliwa na kukemewa kwamba,
“Je! Haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. [Marko 11:17].”
Hukumu ya Mungu itakuwa juu yenu enyi wapotoshaji. Imeandikwa kwamba,
“Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini. [Marko 9:42].”
Mungu akufumbue macho utambue upo wakati gani na nini sasa unachopaswa kufanya kwa habari ya wokovu wako.