Mungu ni mwema siku zote!
Nilianza chuo hapa dar es salaam(chuo Fulani)
Tangu naanza chuo mpaka nimepostpone mwaka wa Pili sikuwai kutumia pesa ya Boom!
Nilikuwa najihusisha na uvuvi, kuuza mtumba kuuza samaki nk.
Ndoto Zangu Ni kufanikiwa kupitia vyombo ya usafiri!
Sasa baada ya kupata hiyo fedha! Nimeenda bank kuchukua mkopo wa Bajaj! Nina uhakika baada ya mwaka mmoja nitamaliza mkataba.
Na Nina uhakika nitakopa kadri ya uwezo wangu!
Nimefanikiwa kununua heka Tano za shamba huko mkoani Tabora!
Malengo yangu mwaka huu nilime heka Tano za mpunga!
Pesa nitakayo ipata kwenye kilimo! Kinachofuata Ni kufungua duka la huduma za kifedha. Airtel money! Bank nk.
Baada ya hapo! Nimepata connection ya fundi wa vitanda vya mninga! Huko Tabora huko anauza laki mbili na nusu!
Vile vitanda huku dar naweza kuuza hata laki Saba.
Shemeji yenu Ni supportive Sana na ananipenda!
Pia hapo badae nitakuwa natoa samaki kambale naleta dar.
Yani Mambo Ni mengi Sana muda mchache.
Naiona Safari yangu ya Kuwa Tajiri
Chuo ntarudi mwakani
Ushauri wowote.